Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Ecclésiaste 12.2
Bible en Swahili de l’est


1 Mkumbuke Muumba wako siku za ujana wako, Kabla hazijaja siku zilizo mbaya, Wala haijakaribia miaka utakaposema, Mimi sina furaha katika hiyo.
Ecclésiaste 11.8 Lamentations 3.27 Psaumes 34.11 Proverbes 22.6 Psaumes 71.17-71.18
2 Kabla jua, na nuru, na mwezi, Na nyota, havijatiwa giza; Kabla ya kurudi mawingu baada ya mvua;
1 Samuel 4.15 Esaïe 5.30 Psaumes 42.7 1 Samuel 3.2 Ecclésiaste 11.7-11.8
3 Siku ile walinzi wa nyumba watakapotetema; Hapo wenye nguvu watakapojiinamisha; Na wasagao kukoma kwa kuwa ni haba; Na hao wachunguliao madirishani kutiwa giza;
2 Samuel 21.15-21.17 Psaumes 90.9-90.10 Zacharie 8.4 Genèse 27.1 Genèse 48.10
4 Na milango kufungwa katika njia kuu; Sauti ya kinu itakapokuwa ni ndogo; Na mtu kusituka kwa sauti ya ndege; Nao binti za kuimba watapunguzwa;
2 Samuel 19.35 Jérémie 25.10 Apocalypse 18.22
5 Naam, wataogopa kilichoinuka Na vitisho vitakuwapo njiani; Na mlozi utachanua maua; Na panzi atakuwa ni mzigo mzito; Na pilipili hoho itapasuka; Maana mtu aiendea nyumba yake ya milele, Nao waombolezao wazunguka njiani.
Job 17.13 Job 30.23 Jérémie 9.17-9.20 Proverbes 16.31 Psaumes 71.18
6 Kabla haijakatika kamba ya fedha; Au kuvunjwa bakuli la dhahabu; Au mtungi kuvunjika kisimani; Au gurudumu kuvunjika birikani;
Zacharie 4.2-4.3
7 Nayo mavumbi kuirudia nchi kama yalivyokuwa, Nayo roho kumrudia Mungu aliyeitoa.
Genèse 3.19 Psaumes 146.4 Genèse 2.7 Esaïe 57.16 Zacharie 12.1
8 Mhubiri asema, Ubatili mtupu; mambo yote ni ubatili!
Ecclésiaste 1.2 Psaumes 62.9 Ecclésiaste 6.12 Ecclésiaste 4.4 Ecclésiaste 8.8

Crainte de Dieu et obéissance

9 Walakini, kwa sababu huyo Mhubiri alikuwa na hekima, aliendelea kuwafundisha watu maarifa, naam, akatafakari, akatafuta-tafuta, akatunga mithali nyingi.
1 Rois 4.32 Proverbes 1.1 1 Rois 8.12-8.21 Proverbes 10.1 1 Rois 10.8
10 Huyo Mhubiri akatafuta-tafuta ili apate kuona maneno yapendezayo, na yale yaliyoandikwa kwa unyofu, yaani, maneno ya kweli.
1 Timothée 1.15 Colossiens 1.5 Jean 3.11 Ecclésiaste 1.1 Proverbes 16.21-16.24
11 Maneno yao wenye hekima huwa mfano wa michokoo; na kama misumari iliyogongomewa sana; ndivyo yalivyo maneno yao walio wakuu wa makusanyiko, ambayo yatoka kwa mchungaji mmoja.
Esaïe 40.11 Jean 10.14 Ezéchiel 34.23 Esaïe 22.23 Actes 2.37
12 Tena, zaidi ya hayo, mwanangu, kubali maonyo; hakuna mwisho wo wote wa kutunga vitabu vingi; na kusoma sana huuchosha mwili.
Ecclésiaste 1.18 1 Rois 4.32 Jean 5.39 2 Pierre 1.19-1.21 Luc 16.29-16.31
13 Hii ndiyo jumla ya maneno; yote yamekwisha sikiwa; Mche Mungu, nawe uzishike amri zake, Maana kwa jumla ndiyo impasayo mtu.
Deutéronome 10.12 Ecclésiaste 5.7 Deutéronome 6.2 Ecclésiaste 8.12 Michée 6.8
14 Kwa maana Mungu ataleta hukumuni kila kazi, pamoja na kila neno la siri, likiwa jema au likiwa baya.
1 Corinthiens 4.5 Romains 2.16 Matthieu 12.36 Ecclésiaste 11.9 Romains 14.10-14.12

Cette Bible est dans le domaine public.