Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Ecclésiaste 12.1
Bible en Swahili de l’est


1 Mkumbuke Muumba wako siku za ujana wako, Kabla hazijaja siku zilizo mbaya, Wala haijakaribia miaka utakaposema, Mimi sina furaha katika hiyo.
Ecclésiaste 11.8 Lamentations 3.27 Proverbes 22.6 Psaumes 71.17-71.18 Psaumes 90.10
2 Kabla jua, na nuru, na mwezi, Na nyota, havijatiwa giza; Kabla ya kurudi mawingu baada ya mvua;
Esaïe 5.30 Psaumes 42.7 1 Samuel 3.2 Ecclésiaste 11.7-11.8 Genèse 48.10
3 Siku ile walinzi wa nyumba watakapotetema; Hapo wenye nguvu watakapojiinamisha; Na wasagao kukoma kwa kuwa ni haba; Na hao wachunguliao madirishani kutiwa giza;
Psaumes 90.9-90.10 Zacharie 8.4 Genèse 27.1 Genèse 48.10 Psaumes 102.23
4 Na milango kufungwa katika njia kuu; Sauti ya kinu itakapokuwa ni ndogo; Na mtu kusituka kwa sauti ya ndege; Nao binti za kuimba watapunguzwa;
2 Samuel 19.35 Jérémie 25.10 Apocalypse 18.22
5 Naam, wataogopa kilichoinuka Na vitisho vitakuwapo njiani; Na mlozi utachanua maua; Na panzi atakuwa ni mzigo mzito; Na pilipili hoho itapasuka; Maana mtu aiendea nyumba yake ya milele, Nao waombolezao wazunguka njiani.
Job 17.13 Job 30.23 Jérémie 9.17-9.20 Proverbes 16.31 Genèse 50.3-50.10
6 Kabla haijakatika kamba ya fedha; Au kuvunjwa bakuli la dhahabu; Au mtungi kuvunjika kisimani; Au gurudumu kuvunjika birikani;
Zacharie 4.2-4.3
7 Nayo mavumbi kuirudia nchi kama yalivyokuwa, Nayo roho kumrudia Mungu aliyeitoa.
Genèse 3.19 Psaumes 146.4 Genèse 2.7 Zacharie 12.1 Ecclésiaste 3.20-3.21
8 Mhubiri asema, Ubatili mtupu; mambo yote ni ubatili!
Ecclésiaste 1.2 Ecclésiaste 6.12 Ecclésiaste 4.4 Ecclésiaste 8.8 Ecclésiaste 1.14

Crainte de Dieu et obéissance

9 Walakini, kwa sababu huyo Mhubiri alikuwa na hekima, aliendelea kuwafundisha watu maarifa, naam, akatafakari, akatafuta-tafuta, akatunga mithali nyingi.
1 Rois 4.32 Proverbes 1.1 Proverbes 10.1 1 Rois 10.8 Proverbes 25.1
10 Huyo Mhubiri akatafuta-tafuta ili apate kuona maneno yapendezayo, na yale yaliyoandikwa kwa unyofu, yaani, maneno ya kweli.
1 Timothée 1.15 Colossiens 1.5 Ecclésiaste 1.1 Proverbes 16.21-16.24 Proverbes 25.11-25.12
11 Maneno yao wenye hekima huwa mfano wa michokoo; na kama misumari iliyogongomewa sana; ndivyo yalivyo maneno yao walio wakuu wa makusanyiko, ambayo yatoka kwa mchungaji mmoja.
Ezéchiel 34.23 Esaïe 22.23 Actes 2.37 Psaumes 80.1 Esaïe 40.11
12 Tena, zaidi ya hayo, mwanangu, kubali maonyo; hakuna mwisho wo wote wa kutunga vitabu vingi; na kusoma sana huuchosha mwili.
Ecclésiaste 1.18 Jean 5.39 2 Pierre 1.19-1.21 Luc 16.29-16.31 Jean 21.25
13 Hii ndiyo jumla ya maneno; yote yamekwisha sikiwa; Mche Mungu, nawe uzishike amri zake, Maana kwa jumla ndiyo impasayo mtu.
Deutéronome 10.12 Ecclésiaste 5.7 Deutéronome 6.2 Ecclésiaste 8.12 Michée 6.8
14 Kwa maana Mungu ataleta hukumuni kila kazi, pamoja na kila neno la siri, likiwa jema au likiwa baya.
Romains 2.16 1 Corinthiens 4.5 Matthieu 12.36 Ecclésiaste 11.9 Romains 14.10-14.12

Cette Bible est dans le domaine public.