1 Ee Mungu, unirehemu, Sawasawa na fadhili zako. Kiasi cha wingi wa rehema zako, Uyafute makosa yangu.
Actes 3.19 Esaïe 43.25 Esaïe 44.22 Colossiens 2.14 Psaumes 106.45
2 Unioshe kabisa na uovu wangu, Unitakase dhambi zangu.
Psaumes 51.7 Apocalypse 1.5 Actes 22.16 Hébreux 10.21-10.22 Ezéchiel 36.25
3 Maana nimejua mimi makosa yangu Na dhambi yangu i mbele yangu daima.
Esaïe 59.12 Proverbes 28.13 Psaumes 32.5 Psaumes 38.18 Luc 15.18-15.21
4 Nimekutenda dhambi Wewe peke yako, Na kufanya maovu mbele za macho yako. Wewe ujulikane kuwa una haki unenapo, Na kuwa safi utoapo hukumu.Romains 3.4 Luc 15.21 Genèse 20.6 Genèse 39.9 2 Samuel 12.9-12.10
5 Tazama, mimi naliumbwa katika hali ya uovu; Mama yangu alinichukua mimba hatiani.
Job 14.4 Ephésiens 2.3 Romains 5.12 Psaumes 58.3 Genèse 8.21
6 Tazama, wapendezwa na kweli iliyo moyoni; Nawe utanijulisha hekima kwa siri,
1 Samuel 16.7 Job 38.36 Romains 7.22 Jérémie 5.3 Jérémie 32.40
7 Unisafishe kwa hisopo nami nitakuwa safi, Unioshe, nami nitakuwa mweupe kuliko theluji
Esaïe 1.18 Hébreux 9.19 1 Jean 1.7 Exode 12.22 Apocalypse 7.13-7.14
8 Unifanye kusikia furaha na shangwe, Mifupa uliyoiponda ifurahi.
Esaïe 35.10 Psaumes 6.2-6.3 Job 5.17-5.18 Matthieu 5.4 Osée 6.1-6.2
9 Usitiri uso wako usitazame dhambi zangu; Uzifute hatia zangu zote.
Jérémie 16.17 Esaïe 38.17 Psaumes 51.1 Colossiens 2.14 Michée 7.18-7.19
10 Ee Mungu, uniumbie moyo safi, Uifanye upya roho iliyotulia ndani yangu
Ezéchiel 11.19 2 Corinthiens 5.17 Ezéchiel 18.31 Matthieu 5.8 Ephésiens 4.22-4.24
11 Usinitenge na uso wako, Wala roho yako mtakatifu usiniondolee.
Ephésiens 4.30 2 Rois 13.23 Romains 8.9 Esaïe 63.10-63.11 1 Samuel 10.10
12 Unirudishie furaha ya wokovu wako; Unitegemeze kwa roho ya wepesi.
Esaïe 41.10 Esaïe 61.10 Psaumes 13.5 Jude 1.24 2 Corinthiens 3.17
13 Nitawafundisha wakosaji njia zako, Na wenye dhambi watarejea kwako.
Luc 22.32 Jean 21.15-21.17 Psaumes 19.7 Esaïe 6.10 Actes 3.19
14 Ee MUNGU, Mungu wa wokovu wangu, Uniponye na damu za watu, Na ulimi wangu utaiimba haki yako.
2 Samuel 12.9 Psaumes 35.28 Psaumes 26.9 Daniel 9.16 2 Samuel 21.1
15 Ee Bwana, uifumbue midomo yangu, Na kinywa changu kitazinena sifa zako.
Psaumes 63.3-63.5 Ezéchiel 29.21 Ezéchiel 16.63 Hébreux 13.15 Exode 4.11
16 Maana hupendezwi na dhabihu, au ningeitoa, Wewe huridhii sadaka ya kuteketezwa.
Psaumes 40.6 Hébreux 10.5-10.6 Amos 5.21-5.23 Proverbes 21.27 1 Samuel 15.22
17 Dhabihu za Mungu ni roho iliyovunjika; Moyo uliovunjika na kupondeka, Ee Mungu, hutaudharau.
Psaumes 34.18 Esaïe 66.2 Luc 18.11-18.14 Luc 15.10 Esaïe 57.15
18 Uitendee mema Sayuni kwa radhi yako, Uzijenge kuta za Yerusalemu.
Psaumes 102.16 Luc 12.32 Psaumes 137.5-137.6 Psaumes 25.22 Psaumes 122.6-122.9
19 Ndipo utakapopendezwa na dhabihu za haki, Na sadaka za kuteketezwa, na kafara. Ndipo watakapotoa ng’ombe Juu ya madhabahu yako.
Psaumes 4.5 Malachie 3.3 Psaumes 118.27 Psaumes 66.13-66.15 Romains 12.1