Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Psaumes 141.4
Bible en Swahili de l’est


Prière pour être délivré des hommes violents

1 Ee Bwana, nimekuita, unijie hima, Uisikie sauti yangu nikuitapo.
Psaumes 70.5 Psaumes 40.13 Psaumes 143.7 Psaumes 71.12 Job 7.21
2 Sala yangu ipae mbele zako kama uvumba, Kuinuliwa mikono yangu kama dhabihu ya jioni.
1 Timothée 2.8 Apocalypse 5.8 Apocalypse 8.3-8.4 Exode 29.39 Psaumes 28.2
3 Ee Bwana, uweke mlinzi kinywani pangu, Mngojezi mlangoni pa midomo yangu.
Michée 7.5 Jacques 1.26 Psaumes 39.1 Psaumes 71.8 Psaumes 34.13
4 Usiuelekeze moyo wangu kunako jambo baya, Nisiyazoelee matendo yasiyofaa, Pamoja na watu watendao maovu; Wala nisile vyakula vyao vya anasa.
Daniel 1.5-1.8 1 Corinthiens 15.33 Esaïe 63.17 1 Rois 8.58 2 Corinthiens 6.17
5 Mwenye haki na anipige, itakuwa fadhili; Anikemee, itakuwa kama mafuta kichwani; Kichwa changu kisikatae, Maana siachi kusali kati ya mabaya yao.
Proverbes 25.12 Proverbes 19.25 Galates 6.1 Psaumes 125.4 Proverbes 15.22
6 Makadhi wao wakiangushwa kando ya genge, Watayasikia maneno yangu, maana ni matamu.
1 Chroniques 11.1-11.3 2 Samuel 23.1 2 Chroniques 25.12 2 Samuel 1.17-1.27 1 Chroniques 10.1-10.7
7 Kama kupasua kuni na kuzichanja juu ya nchi, Ndivyo ilivyo mifupa yetu mdomoni pa kuzimu.
Psaumes 53.5 Apocalypse 11.8-11.9 Psaumes 44.22 Hébreux 11.37 2 Corinthiens 1.9
8 Macho yangu yanakuelekea Wewe, MUNGU Bwana, Nimekukimbilia Wewe, usiniache nafsi yangu.
Esaïe 41.17 2 Chroniques 20.12 Psaumes 25.15-25.17 Psaumes 123.1-123.2 Psaumes 102.17
9 Unilinde na mtego walionitegea, Na matanzi yao watendao maovu.
Psaumes 140.5 Psaumes 119.110 Jérémie 18.22 Luc 20.20 Psaumes 38.12
10 Wabaya na waanguke katika nyavu zao wenyewe, Pindi mimi ninapopita salama.
Psaumes 35.8 Psaumes 7.15-7.16 Psaumes 37.14-37.15 Proverbes 11.8 Esther 7.10

Cette Bible est dans le domaine public.