Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Psaumes 125.5
Bible en Swahili de l’est


Dieu, un rempart pour son peuple

1 Wamtumainio Bwana ni kama mlima Sayuni, Ambao hautatikisika, wakaa milele.
Jérémie 17.7-17.8 Psaumes 120.1 Psaumes 25.2 1 Chroniques 5.20 Abdias 1.21
2 Kama milima inavyouzunguka Yerusalemu, Ndivyo Bwana anavyowazunguka watu wake, Tangu sasa na hata milele.
Zacharie 2.5 Deutéronome 33.27 Psaumes 34.7 Lamentations 4.12 Esaïe 4.5
3 Kwa maana fimbo ya udhalimu Haitakaa juu ya fungu la wenye haki; Wenye haki wasije wakainyosha Mikono yao kwenye upotovu.
Proverbes 22.8 Psaumes 89.22 Esaïe 14.5-14.6 1 Samuel 24.10 Psaumes 103.9
4 Ee Bwana, uwatendee mema walio wema, Nao walio wanyofu wa moyo.
Psaumes 7.10 Psaumes 119.68 Hébreux 6.10 Jean 1.47 Esaïe 58.10-58.11
5 Bali wao wanaozigeukia njia zao zilizopotoka, Bwana atawaondoa pamoja na watenda maovu. Amani ikae na Israeli.
Proverbes 2.15 Psaumes 128.6 Esaïe 59.8 Galates 6.16 Psaumes 40.4

Cette Bible est dans le domaine public.