Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Psaumes 115.15
Bible en Swahili de l’est


À Dieu seul la gloire

1 Ee Bwana, kutukuza usitutukuze sisi, Bali ulitukuze jina lako, Kwa ajili ya fadhili zako, Kwa ajili ya uaminifu wako.
Psaumes 79.9-79.10 Esaïe 48.11 Ezéchiel 36.32 Ezéchiel 36.22 Psaumes 96.8
2 Kwa nini mataifa kusema, Yuko wapi Mungu wao?
Psaumes 42.3 Psaumes 79.10 Psaumes 42.10 Exode 32.12 2 Rois 19.10-19.19
3 Lakini Mungu wetu yuko mbinguni, Alitakalo lote amelitenda.
Daniel 4.35 Psaumes 135.6 Psaumes 103.19 Ephésiens 1.11 Matthieu 6.9
4 Sanamu zao ni fedha na dhahabu, Kazi ya mikono ya wanadamu.
Deutéronome 4.28 Jérémie 10.3-10.5 Esaïe 46.6-46.7 Esaïe 46.1-46.2 Actes 19.26
5 Zina vinywa lakini hazisemi, Zina macho lakini hazioni,
Jérémie 10.5
6 Zina masikio lakini hazisikii, Zina pua lakini hazisikii harufu,
7 Mikono lakini hazishiki, miguu lakini haziendi, Wala hazitoi sauti kwa koo zake.
8 Wazifanyao watafanana nazo, Kila mmoja anayezitumainia.
Psaumes 135.18 Habakuk 2.18-2.19 Jérémie 10.8 Esaïe 44.9-44.20 Jonas 2.8
9 Enyi Israeli, mtumainini Bwana; Yeye ni msaada wao na ngao yao.
Psaumes 62.8 Psaumes 135.19-135.20 Psaumes 37.3 Psaumes 118.2-118.4 Psaumes 130.7
10 Enyi mlango wa Haruni, mtumainini Bwana; Yeye ni msaada wao na ngao yao.
Exode 28.1 Nombres 18.7 Psaumes 118.3 Nombres 16.40 Nombres 16.5
11 Enyi mmchao Bwana, mtumainini Bwana; Yeye ni msaada wao na ngao yao.
Proverbes 14.26 Psaumes 22.23 Actes 10.35 Psaumes 147.11 Apocalypse 19.5
12 Bwana ametukumbuka, Naye atatubariki sisi. Ataubariki mlango wa Israeli, Ataubariki mlango wa Haruni,
Psaumes 136.23 Esaïe 49.14-49.16 Ephésiens 1.3 Galates 3.29 Genèse 12.2-12.3
13 Atawabariki wamchao Bwana, Wadogo kwa wakubwa.
Psaumes 112.1 Psaumes 128.1 Apocalypse 19.5 Apocalypse 11.18 Luc 1.50
14 Bwana na awaongeze ninyi, Ninyi na watoto wenu.
Deutéronome 1.11 Actes 2.39 Jérémie 32.38-32.39 Jérémie 30.19 Jérémie 33.22
15 Na mbarikiwe ninyi na Bwana, Aliyezifanya mbingu na nchi.
Genèse 1.1 Psaumes 96.5 Genèse 14.19 Apocalypse 14.7 Ephésiens 1.3-1.4
16 Mbingu ni mbingu za Bwana, Bali nchi amewapa wanadamu.
Psaumes 89.11 Genèse 1.28-1.30 Psaumes 8.6 Jérémie 27.5-27.6 Genèse 9.1-9.3
17 Sio wafu wamsifuo Bwana, Wala wo wote washukao kwenye kimya;
Psaumes 6.5 Psaumes 31.17 Psaumes 88.10-88.12 1 Samuel 2.9 Psaumes 30.9
18 Bali sisi tutamhimidi Bwana, Tangu leo na hata milele.
Psaumes 113.2 Daniel 2.20 Psaumes 145.21 Psaumes 145.2 Psaumes 118.17-118.19

Cette Bible est dans le domaine public.