Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Job 34
Bible en Swahili de l’est


La justice souveraine

1 Tena Elihu akajibu na kusema,
2 Sikilizeni maneno yangu, enyi wenye hekima; Tegeni masikio kwangu, ninyi mlio na maarifa.
1 Corinthiens 14.20 1 Corinthiens 10.15 Proverbes 1.5
3 Kwa kuwa sikio huyajaribu maneno, Kama vile kaakaa lionjavyo chakula.
Job 12.11 1 Corinthiens 2.15 Hébreux 5.14 Job 33.2 Job 6.30
4 Na tujichagulie yaliyo ya uelekevu; Na tujue wenyewe yaliyo mema.
1 Thessaloniciens 5.21 Jean 7.24 Romains 12.2 Job 34.36 Esaïe 11.2-11.5
5 Kwani Ayubu amesema, Mimi ni mwenye haki, Naye Mungu ameniondolea haki yangu;
Job 27.2 Job 33.9 Job 16.17 Job 32.1 Job 11.4
6 Nijapokuwa mwenye haki, nimehesabiwa kuwa mwongo; Jeraha yangu haiponyeki, nijapokuwa sina makosa.
Job 6.4 Job 27.4-27.6 Job 16.13
7 Je! Ni mtu gani mfano wa Ayubu, Anywaye mzaha kama maji?
Job 15.16 Proverbes 1.22 Deutéronome 29.19 Proverbes 4.17
8 Atembeaye na hao watendao uovu, Na kwenda pamoja na watu wabaya.
Psaumes 1.1 Proverbes 13.20 1 Corinthiens 15.33 Psaumes 50.18 Psaumes 26.4
9 Kwa kuwa amenena, Haimfai mtu lo lote Kujifurahisha na Mungu.
Job 35.3 Malachie 3.14 Job 9.22-9.23 Psaumes 37.4 Job 9.30-9.31
10 Kwa hiyo nisikilizeni, enyi wenye fahamu; Mungu asidhaniwe kutenda udhalimu; Wala Mwenyezi kufanya uovu.
Deutéronome 32.4 Romains 9.14 Genèse 18.25 Job 8.3 2 Chroniques 19.7
11 Kwani atamlipa binadamu kwa kazi yake, Naye atamfanya kila mtu kuona sawasawa na njia zake
Romains 2.6 Matthieu 16.27 2 Corinthiens 5.10 Psaumes 62.12 Apocalypse 22.12
12 Naam, hakika, Mungu hatatenda mabaya, Wala Mwenyezi hatapotosha hukumu.
Job 8.3 Psaumes 145.17 Psaumes 11.7 Habakuk 1.12-1.13
13 Ni nani aliyemwagiza kuiangalia dunia? Au ni nani aliyemwekea ulimwengu huu wote?
1 Chroniques 29.11 Romains 11.34-11.36 Proverbes 8.23-8.30 Daniel 4.35 Job 38.4-38.41
14 Kama akimwekea mtu moyo wake, Akijikusanyia roho yake na pumzi zake;
Psaumes 104.29 Job 9.4 Job 7.17 Esaïe 24.22
15 Wenye mwili wote wataangamia pamoja, Nao wanadamu watarejea tena kuwa mavumbi.
Genèse 3.19 Esaïe 57.16 Ecclésiaste 12.7 Esaïe 27.4 Psaumes 90.3-90.10
16 Ikiwa una ufahamu, sikia neno hili; Isikilize sauti ya maneno yangu.
Job 13.2-13.6 Job 12.3
17 Je! Atatawala mtu aichukiaye haki hata mmoja? Nawe, je! Utamhukumia mkosa aliye na haki na mwenye nguvu?
Job 40.8 2 Samuel 23.3 Genèse 18.25 Romains 3.5-3.7 Romains 9.14
18 Je! Inafaa kumwambia mfalme, Wewe u mwovu? Au kuwaambia wakuu, Ninyi ni wabaya?
Exode 22.28 Romains 13.7 Proverbes 17.26 Jude 1.8 Actes 23.3
19 Sembuse huyo asiyependelea nyuso za wakuu, Wala hawajali matajiri kuliko maskini? Kwani wote ni kazi ya mikono yake,
Deutéronome 10.17 Jacques 2.5 Ephésiens 6.9 Actes 10.34 1 Pierre 1.17
20 Hufa ghafula, hata usiku wa manane; Watu hutikisika na kwenda zao, Nao mashujaa huondolewa pasipo mkono wa mtu.
Job 12.19 Daniel 5.30 Esaïe 37.36 Esaïe 10.16-10.19 Esaïe 37.38
21 Kwani macho yake ya juu ya njia za mtu, Naye huiona miendo yake yote.
Proverbes 15.3 Job 31.4 Proverbes 5.21 Jérémie 16.17 Jérémie 32.19
22 Hapana weusi, wala hilo giza tupu, Wawezapo kujificha watendao udhalimu.
Amos 9.2-9.3 Psaumes 139.11-139.12 Proverbes 10.29 Job 3.5 Hébreux 4.13
23 Kwani yeye hana haja ya kumfikiria mtu zaidi, ili aende mbele za Mungu ahukumiwe.
Psaumes 119.137 Daniel 9.7-9.9 Esdras 9.13 Job 23.7 Job 9.32-9.33
24 Yeye huwavunja-vunja mashujaa pasina kuwachunguza, Na kuwaweka wengine mahali pao.
Psaumes 2.9 Psaumes 113.7-113.8 Daniel 2.21 Daniel 2.44-2.45 1 Rois 14.14
25 Kwa sababu hiyo yeye huyatafiti matendo yao; Naye huwapindia usiku, wakaangamia.
Job 34.20 Esaïe 66.18 Apocalypse 20.12 Esaïe 15.1 Amos 8.7
26 Yeye huwapiga kama watu wabaya Waziwazi mbele ya macho ya wengine;
2 Samuel 12.11-12.12 Deutéronome 13.9-13.11 1 Timothée 5.24 Apocalypse 18.20 Deutéronome 21.21
27 Kwa sababu walikengeuka, wasimwandame yeye, Wasikubali kuzishika njia zake hata moja;
1 Samuel 15.11 Esaïe 5.12 Psaumes 28.5 Hébreux 10.39 Psaumes 125.5
28 Hata wakafanya kilio cha maskini kumfikilia, Naye akasikia kilio cha hao wateswao.
Jacques 5.4 Job 35.9 Exode 3.7 Exode 3.9 Psaumes 12.5
29 Akitoa utulivu yeye, ni nani awezaye kuhukumia makosa? Akificha uso wake, ni nani awezaye kumtazama? Kama hufanyiwa taifa, au mtu mmoja, ni sawasawa;
Esaïe 26.3 Jérémie 27.8 Job 12.14 Psaumes 30.7 Philippiens 4.7
30 Kwamba huyo mpotovu asitawale, Pasiwe na wa kuwatega watu.
Osée 13.11 1 Rois 12.28-12.30 Job 34.21 Proverbes 29.2-29.12 Apocalypse 13.3-13.4
31 Kwani kuna mtu aliyemwambia Mungu, Mimi nimevumilia kurudiwa, ingawa sikukosa;
Job 33.27 Michée 7.9 Esdras 9.13-9.14 Daniel 9.7-9.14 Jérémie 31.18-31.19
32 Nisiyoyaona nifundishe wewe; Kama nimefanya uovu sitafanya tena?
Psaumes 19.12 Proverbes 28.13 Ephésiens 4.22 Job 35.11 Luc 3.8-3.14
33 Je! Malipo yake yatakuwa kama upendavyo wewe, hata ukayakataa? Kwani yakupasa wewe kuchagua, si mimi; Kwa sababu hiyo sema uyajuayo.
Psaumes 135.6 Job 33.32 Proverbes 11.31 2 Thessaloniciens 1.6-1.7 Job 41.11
34 Watu walio na akili wataniambia, Naam, kila mtu mwenye hekima anisikiaye;
Job 34.2 1 Corinthiens 10.15 Job 34.4 Job 34.16 Job 34.10
35 Huyo Ayubu amesema pasipo maarifa, Na maneno yake hayana hekima.
Job 35.16 Job 38.2 Job 13.2 Job 15.2 Job 42.3
36 Laiti Ayubu angejaribiwa hata mwisho, Kwa kuwa amejibu kama watu waovu.
Psaumes 17.3 Job 24.1 Jacques 5.11 Job 12.6 Job 21.7
37 Kwani huongeza uasi juu ya dhambi zake, Apiga makofi kati yetu, Na kuongeza maneno yake kinyume cha Mungu.
Job 27.23 Esaïe 1.19-1.20 1 Samuel 15.23 Job 11.2-11.3 Job 42.7

Cette Bible est dans le domaine public.