Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Esther 1.2
Bible en Swahili de l’est


Accession d’Esther au trône

Destitution de la reine Vasthi

1 Zamani za Ahasuero; naye huyu Ahasuero alimiliki toka Bara Hindi mpaka Kushi, juu ya majimbo mia na ishirini na saba;
Esther 8.9 Daniel 9.1 Esdras 4.6 Daniel 6.1 Esther 9.30
2 siku zile mfalme Ahasuero alipoketi katika kiti cha enzi cha ufalme wake, huko Shushani ngomeni;
Néhémie 1.1 1 Rois 1.46 Daniel 8.2 2 Samuel 7.1 Esther 3.15
3 mwaka wa tatu wa kumiliki kwake, ikawa aliwafanyia karamu maakida wake wote na majumbe wake; wakuu wa Uajemi na Umedi, watu wenye cheo na maakida wa majimbo, wakihudhuria mbele zake.
Esther 2.18 1 Rois 3.15 Marc 6.21 Genèse 40.20 Daniel 5.1
4 Akawaonyesha utajiri wa ufalme wake mtukufu, na heshima ya enzi yake bora siku nyingi, maana siku mia na themanini.
Psaumes 76.1-76.4 Daniel 4.30 1 Chroniques 29.25 1 Chroniques 29.11-29.12 Daniel 2.37-2.44
5 Hata siku hizo zilipotimia, mfalme akawafanyia karamu watu wote waliokuwapo huko Shushani ngomeni, wakubwa kwa wadogo, muda wa siku saba, katika behewa la bustani ya ngome ya mfalme.
Esther 7.7-7.8 2 Chroniques 7.8-7.9 2 Chroniques 30.21-30.25
6 Palikuwa na mapazia ya bafta, nyeupe na samawi, yamefungiwa kamba za kitani safi za rangi ya zambarau kwa pete za fedha na nguzo za marumaru; pia na vitanda vilikuwa vya dhahabu na fedha juu ya sakafu ya marumaru, mawe mekundu, na meupe, na ya manjano, na meusi.
Ezéchiel 23.41 Amos 6.4 Esther 7.8 Esther 8.15 Exode 26.36-26.37
7 Wakawanywesha kileo katika vyombo vya dhahabu, na vile vyombo vilikuwa mbalimbali, na divai tele ya namna ya kifalme, sawasawa na ukarimu wa mfalme;
2 Chroniques 9.20 Daniel 5.2-5.4 Esther 2.18 1 Rois 10.21
8 kunywa kulikuwa kama ilivyoamriwa, bila sharti; maana ndivyo mfalme alivyowaagiza watumishi-wa-nyumbani, kila mtu afanye apendavyo.
Habakuk 2.15-2.16 Jérémie 35.8 Jérémie 51.7 Jean 2.8
9 Tena Vashti, malkia, naye akawafanyia karamu wanawake ndani ya nyumba ya kifalme ya mfalme Ahasuero.
Esther 5.4 Esther 5.8
10 Hata siku ya saba, mfalme alipofurahiwa moyo wake kwa divai, aliwaamuru Mehumani, Biztha, Harbona, Bigtha, Abagtha, Zethari, na Karkasi, wale wasimamizi-wa-nyumba saba waliohudumu mbele za mfalme Ahasuero,
Esther 7.9 Juges 16.25 Ecclésiaste 7.2-7.4 Proverbes 20.1 2 Samuel 13.28
11 wamlete Vashti, malkia, mbele ya mfalme, amevaa taji ya kifalme; ili kuwaonyesha watu na maakida uzuri wake, maana alikuwa mzuri wa uso.
Marc 6.21-6.22 2 Samuel 14.25 1 Samuel 25.3 Esther 2.17 Proverbes 31.30
12 Bali Vashti, malkia, alikataa kuja kwa amri ya mfalme kwa mkono wa wasimamizi-wa-nyumba; kwa hiyo mfalme akaghadhibika sana, na hasira yake ikawaka ndani yake.
Proverbes 19.12 Apocalypse 6.16-6.17 Psaumes 74.1 Daniel 3.13 Exode 32.22
13 Basi mfalme akawaambia wenye hekima, walio na elimu ya nyakati; maana ndivyo ilivyokuwa desturi ya mfalme kwa wote waliojua sheria na hukumu;
Jérémie 10.7 1 Chroniques 12.32 Daniel 2.12 Daniel 2.2 Matthieu 2.1
14 na karibu naye wameketi Karshena, Shethari, Admatha, Tarshishi, Meresi, Marsena, na Memukani, wale maakida saba wa Uajemi na Umedi, waliouona uso wa mfalme, na kuketi wa kwanza katika ufalme; akawauliza,
2 Rois 25.19 Esdras 7.14 Matthieu 18.10 Apocalypse 22.4
15 Tumfanyieje Vashti, malkia, kwa sheria, kwa sababu hakufanya kama vile alivyoamriwa na mfalme Ahasuero kwa mkono wa wasimamizi-wa-nyumba?
Esther 6.6
16 Basi Memukani akajibu mbele ya mfalme na maakida, Huyu Vashti, malkia, hakumkosa mfalme tu peke yake, ila na maakida wote, na watu wote pia walioko katika majimbo yote ya mfalme Ahasuero.
1 Corinthiens 6.7-6.8 Actes 25.10 Actes 18.14
17 Kwa maana tendo hilo la malkia litajulikana na wanawake wote, hata waume zao watadharauliwa machoni pao, itakaponenwa ya kuwa mfalme Ahasuero aliamuru Vashti, malkia, aletwe mbele yake, bali hakuja.
Ephésiens 5.33 2 Samuel 6.16
18 Hata na leo hivi mabibi wastahiki wa Uajemi na Umedi waliokwisha kuzisikia habari za tendo lake malkia watawaambia vivi hivi maakida wote wa mfalme. Hivyo kutatokea dharau nyingi na ghadhabu tele.
1 Rois 11.3 Juges 5.29
19 Basi mfalme akiona vema, na itoke kwake amri ya kifalme, nayo iandikwe katika sheria za Waajemi na Wamedi isitanguke, ya kwamba Vashti asifike tena mbele ya mfalme Ahasuero; na umalkia wake mfalme ampe mwingine aliye mwema kuliko yeye.
Esther 8.8 1 Samuel 15.28 1 Rois 3.28 Daniel 6.8-6.15 Esther 3.9
20 Basi mbiu ya mfalme atakayoipiga itakapotangazwa katika ufalme wake wote, nao ni mkubwa, wake wote watawaheshimu waume zao, wakubwa kwa wadogo.
Colossiens 3.18 Ephésiens 5.33 1 Pierre 3.1-3.7 Deutéronome 21.21 Ephésiens 5.22
21 Basi neno hili likawapendeza mfalme na maakida; naye mfalme akafanya sawasawa na neno lake Memukani.
Esther 2.4 Genèse 41.37 Esther 1.19
22 Kwa maana alipeleka nyaraka katika majimbo yote ya mfalme, kila jimbo kwa mwandiko wake, na kila taifa kwa lugha yake, ya kwamba kila mwanamume atawale nyumbani mwake, na kuitangaza habari hii kwa lugha ya watu wake.
Esther 3.12 Esther 8.9 Ephésiens 5.22-5.24 1 Timothée 2.12 Luc 16.8

Cette Bible est dans le domaine public.