Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Néhémie 1.11
Bible en Swahili de l’est


Mandat de Néhémie

Tristesse de Néhémie

1 Habari za Nehemia, mwana wa Hakalia. Ikawa katika mwezi wa Kisleu, mwaka wa ishirini, nilipokuwapo Shushani ngomeni,
Zacharie 7.1 Néhémie 10.1 Esther 1.2 Daniel 8.2 Esdras 10.9
2 Hanani, mmoja wa ndugu zangu, akanijia, yeye na watu wengine waliotoka Yuda; nami nikawauliza habari za Wayahudi waliopona, hao watu wa uhamisho waliosalia; na habari za Yerusalemu.
Néhémie 7.2 Ezéchiel 7.16 Esdras 9.14 Esdras 9.8-9.9 Jérémie 44.14
3 Wakaniambia, Watu wa uhamisho, waliosalia huko katika wilaya ile, wamo katika hali ya dhiki nyingi na mashutumu; tena ukuta wa Yerusalemu umebomolewa, na malango yake yameteketezwa kwa moto.
Néhémie 2.17 2 Rois 25.10 Néhémie 2.13 Néhémie 2.3 Néhémie 7.6
4 Hata ikawa niliposikia maneno hayo, nikaketi, nikalia, nikaomboleza siku kadha wa kadha; kisha nikafunga, nikaomba mbele za Mungu wa mbinguni;
Néhémie 2.4 Psaumes 137.1 Esdras 10.1 Esdras 5.11-5.12 Daniel 2.18
5 nikasema, Nakusihi, Ee Bwana, Mungu wa mbinguni, Mungu mkuu, mwenye kuogofya, mwenye kutimiza agano lake na rehema zake kwa hao wampendao na kuzishika amri zake;
Néhémie 4.14 Exode 20.6 Deutéronome 7.21 Deutéronome 7.9 Daniel 9.4-9.19
6 tega sikio lako, macho yako yakafumbuke, upate kuyasikiliza maombi ya mtumishi wako, ninayoomba mbele zako wakati huu, mchana na usiku, kwa ajili ya wana wa Israeli, watumishi wako; hapo ninapoziungama dhambi za wana wa Israeli, tulizozifanya juu yako; naam, mimi na nyumba ya baba yangu tumefanya dhambi.
Daniel 9.20 2 Chroniques 29.6 Daniel 9.17-9.18 Psaumes 106.6 2 Chroniques 6.40
7 Tumetenda maovu mengi juu yako, wala hatukuzishika amri, wala sheria, wala hukumu, ulizomwamuru Musa, mtumishi wako.
Psaumes 106.6 Daniel 9.13 Deutéronome 4.5 Apocalypse 19.2 1 Rois 2.3
8 Nakuomba, likumbuke neno lile ulilomwamuru Musa, mtumishi wako, ukisema, Mkikosa, nitawatawanya kati ya mataifa;
Deutéronome 4.25-4.27 Deutéronome 28.64 Lévitique 26.33-26.46 Deutéronome 32.26-32.28 1 Rois 9.6-9.7
9 bali mkinirudia mimi, na kuzishika amri zangu na kuzitenda, watu wako waliofukuzwa wajapokuwa katika pande za mwisho za mbingu, hata hivyo nitawakusanya kutoka huko, na kuwaleta mpaka mahali pale nilipopachagua ili kuliweka jina langu hapo.
Deutéronome 4.29-4.31 Deutéronome 12.5 Deutéronome 30.2-30.5 Jérémie 29.11-29.14 Jérémie 31.10
10 Basi watu hao ni watumishi wako na watu wako, uliowakomboa kwa uweza wako mwingi, na kwa mkono wako hodari.
Deutéronome 9.29 Exode 32.11 Exode 6.1 Esaïe 64.9 Psaumes 136.12
11 Ee Bwana, nakusihi, litege sikio lako, uyasikilize maombi ya mtumishi wako, na maombi ya watumishi wako, wanaofurahi kulicha jina lako; nakuomba sana; unifanikishe mimi, mtumishi wako, leo, ukanijalie rehema mbele ya mtu huyu. (Maana, nalikuwa mnyweshaji wa mfalme).
Néhémie 1.6 Néhémie 2.1 Genèse 40.21 Néhémie 2.8 Genèse 40.2

Cette Bible est dans le domaine public.