Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

2 Chroniques 8.8
Bible en Swahili de l’est


Travaux de construction de Salomon

1 Ikawa miaka ishirini ilipopita, ambayo katika hiyo Sulemani aliijenga nyumba ya Bwana, na nyumba yake mwenyewe;
1 Rois 9.10-9.28
2 ndipo Sulemani akaijenga miji ile Hiramu aliyompa Sulemani, akawakalisha humo wana wa Israeli.
1 Rois 9.11-9.18
3 Naye Sulemani akaenda Hamath-zoba, akaushinda.
1 Chroniques 18.3 Nombres 34.8 2 Samuel 8.3 1 Rois 11.23-11.25 Nombres 13.21
4 Akaujenga Tadmori wa nyikani, na miji yote ya hazina, aliyoijenga katika Hamathi.
1 Rois 9.17-9.19
5 Tena akaujenga Beth-horoni wa juu, na Beth-horoni wa chini, miji yenye boma, yenye kuta, na malango, na makomeo;
1 Chroniques 7.24 Josué 16.5 2 Chroniques 14.7 Josué 16.3
6 na Baalathi, na miji yote ya hazina Sulemani aliyokuwa nayo, na miji yote ya magari yake, na miji ya wapanda farasi wake, na ya anasa yote aliyopenda Sulemani kujenga humo Yerusalemu, na katika Lebanoni, na katika nchi yote ya mamlaka yake.
Ecclésiaste 2.10-2.26 2 Chroniques 17.12 1 Rois 7.2 1 Rois 9.18-9.19 Ecclésiaste 2.4
7 Basi kwa habari ya watu wote waliosalia wa Wahiti, na wa Waamori, na wa Waperizi, na wa Wahivi, na wa Wayebusi, wasiokuwa wa Israeli;
Deutéronome 7.1 Genèse 15.18-15.21 1 Rois 9.20-9.22
8 wa watoto wao waliosalia baada yao katika nchi, ambao wana wa Israeli hawakuwakomesha, katika hao Sulemani akawatumikisha shokoa hata leo.
1 Rois 4.6 Josué 16.10 1 Rois 9.21 Josué 17.13 Psaumes 106.34
9 Wala katika wana wa Israeli Sulemani hakuwafanya watumwa kazini mwake; lakini hao walikuwa watu wa vita, na wakuu wa majemadari wake, na maakida wa magari yake na wa wapanda farasi wake.
Lévitique 25.39-25.46 Galates 4.31 Exode 19.5-19.6 Galates 4.26 1 Samuel 8.11-8.12
10 Na hao walikuwa maakida wakuu wa Sulemani, watu mia mbili na hamsini, waliotawala juu ya watu.
1 Rois 9.23 2 Chroniques 2.18 1 Rois 5.16
11 Sulemani akamleta binti Farao kutoka mji wa Daudi mpaka nyumba aliyomjengea; kwa kuwa alisema, Mke wangu hatakaa nyumbani mwa Daudi mfalme wa Israeli, kwa kuwa ni patakatifu, mahali palipofika sanduku la Bwana.
1 Rois 7.8 1 Rois 3.1 1 Rois 9.24 Exode 3.5 2 Pierre 1.18
12 Ndipo Sulemani akamtolea Bwana sadaka za kuteketezwa juu ya madhabahu ya Bwana, aliyoijenga mbele ya ukumbi,
2 Chroniques 4.1 Joël 2.17 2 Chroniques 15.8 Jean 10.23 1 Chroniques 28.17
13 kadiri ilivyohitajiwa huduma ya kila siku, akitoa sawasawa na amri ya Musa, siku za sabato, na za mwezi mpya, na za sikukuu zilizoamriwa, mara tatu kila mwaka, yaani, sikukuu ya mikate isiyochachwa, na sikukuu ya majuma, na sikukuu ya vibanda.
Deutéronome 16.16 Exode 29.38-29.42 Ezéchiel 46.3-46.15 Exode 23.14-23.17 Lévitique 23.1-23.17
14 Akaziamuru, sawasawa na agizo la Daudi babaye, zamu za makuhani za kutumika, nao Walawi kwa kadiri ya malinzi yao, ili kusifu, na kuhudumu mbele ya makuhani, kama ilivyohitajiwa kila siku; tena mabawabu kwa zamu zao za kila mlango; maana ndivyo alivyoamuru Daudi mtu wa Mungu.
1 Chroniques 9.17 Néhémie 12.24 Néhémie 12.36 1 Chroniques 28.19 1 Chroniques 16.42
15 Wala hawakuyaacha maagizo ya mfalme aliyowaamuru makuhani na Walawi kwa neno lo lote, wala kwa habari ya hazina.
2 Chroniques 30.12 1 Chroniques 9.29 Exode 39.42-39.43 1 Chroniques 26.20-26.26 1 Rois 7.51
16 Basi ikatengenezwa kazi yote ya Sulemani hata siku ya kutiwa msingi wa nyumba ya Bwana, na hata ilipokwisha. Hivyo ikamalizika nyumba ya Bwana.
1 Rois 5.18 1 Rois 6.7
17 Ndipo Sulemani akaenda Esion-geberi, na Elothi, pwani ya nchi ya Edomu.
2 Rois 14.22 Deutéronome 2.8 1 Rois 22.48 2 Rois 16.6 Nombres 33.35
18 Naye Hiramu akamletea merikebu kwa mikono ya watumishi wake, na watumishi waliokuwa wana-maji; nao wakafika Ofiri pamoja na watumishi wa Sulemani, wakachukua kutoka huko talanta mia nne na hamsini za dhahabu, wakamletea mfalme Sulemani.
2 Chroniques 9.10 2 Chroniques 9.13 1 Rois 10.22 1 Rois 9.27-9.28 Ecclésiaste 2.8

Cette Bible est dans le domaine public.