Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

2 Chroniques 29.19
Bible en Swahili de l’est


Règne d’Ézéchias

1 Hezekia alikuwa na umri wa miaka ishirini na mitano alipoanza kutawala; akatawala katika Yerusalemu miaka ishirini na kenda; na jina la mamaye aliitwa Abiya binti Zekaria.
2 Rois 18.1-18.3 2 Chroniques 26.5 1 Chroniques 3.13 Esaïe 1.1 Matthieu 1.9-1.10
2 Akafanya yaliyo ya adili machoni pa Bwana, sawasawa na yote aliyoyafanya Daudi babaye.
2 Chroniques 34.2 2 Chroniques 28.1
3 Yeye, katika mwaka wa kwanza wa kutawala kwake, katika mwezi wa kwanza, aliifungua milango ya nyumba ya Bwana, akaitengeneza.
2 Chroniques 28.24 2 Chroniques 29.7 Matthieu 6.33 2 Chroniques 34.3 2 Rois 16.14-16.18
4 Akawaingiza makuhani na Walawi, akawakusanya uwandani upande wa mashariki,
2 Chroniques 32.6 Néhémie 3.29 Jérémie 19.2
5 akawaambia, Nisikieni, enyi Walawi; jitakaseni nafsi zenu sasa, mkaitakase na nyumba ya Bwana, Mungu wa baba zenu, mkautoe uchafu katika patakatifu.
2 Chroniques 35.6 1 Chroniques 15.12 Exode 19.15 2 Chroniques 29.15-29.16 2 Corinthiens 6.16
6 Kwa maana baba zetu wameasi, na kufanya yaliyo maovu machoni pa Bwana, Mungu wetu, wamemwacha, na kugeuzia mbali nyuso zao na makao ya Bwana, na kumpa maungo.
Ezéchiel 8.16 Jérémie 2.27 Jérémie 2.17 Matthieu 23.30-23.32 Néhémie 9.32
7 Tena wameifunga milango ya ukumbi, na kuzizima taa, wala hawakufukiza uvumba, wala hawakumtolea Mungu wa Israeli sadaka za kuteketezwa katika patakatifu.
2 Chroniques 28.24 2 Chroniques 29.3 2 Rois 16.17-16.18 Malachie 1.10 Lévitique 24.2-24.8
8 Kwa hiyo hasira ya Bwana imekuwa juu ya Yuda na Yerusalemu, naye amewatoa kuwa matetemeko, wawe ushangao, na mazomeo, kama mwonavyo kwa macho yenu.
Jérémie 25.18 Jérémie 25.9 Deutéronome 28.25 Jérémie 19.8 2 Chroniques 24.18
9 Kwa kuwa, tazama, baba zetu wameangamia kwa upanga, na wana wetu, na binti zetu, na wake zetu wametekwa kwa ajili ya hayo.
2 Chroniques 28.17 2 Chroniques 28.5-28.8 Lévitique 26.17 Lamentations 5.7
10 Basi nia yangu ni kufanya agano na Bwana, Mungu wa Israeli, ili kwamba hasira yake kali itugeukie mbali.
2 Chroniques 23.16 2 Rois 23.3 2 Chroniques 6.7-6.8 Jérémie 34.15 Esdras 10.3
11 Basi wanangu, msijipurukushe sasa, kwa kuwa Bwana amewachagua ninyi msimame mbele yake, kumhudumia, nanyi mpate kuwa watumishi wake, mkafukize uvumba.
Galates 6.7-6.8 Nombres 16.35-16.40 Nombres 8.6-8.14 Deutéronome 10.8 Nombres 18.2-18.7
12 Ndipo wakaondoka Walawi, Mahathi mwana wa Amasai, na Yoeli mwana wa Azaria, wa wana wa Wakohathi; na wa wana wa Merari, Kishi mwana wa Abdi, na Azaria mwana wa Yehaleleli; na wa Wagershoni, Yoa mwana wa Zima na Edeni mwana wa Yoa;
1 Chroniques 6.44 Nombres 4.2-4.20 Exode 6.16-6.25 1 Chroniques 6.16-6.21 Nombres 3.19-3.20
13 na wa wana wa Elisafani, Shimri na Yeueli; na wa wana wa Asafu, Zekaria na Matania;
1 Chroniques 6.39 1 Chroniques 15.8 1 Chroniques 15.17 1 Chroniques 25.2 Lévitique 10.4
14 na wa wana wa Hemani, Yehueli na Shimei; na wa wana wa Yeduthuni, Shemaya na Uzieli.
1 Chroniques 6.33 1 Chroniques 25.3 1 Chroniques 25.1 1 Chroniques 15.19 1 Chroniques 25.6
15 Wakawakusanya ndugu zao, wakajitakasa, wakaingia, kama alivyoamuru mfalme kwa maneno ya Bwana, ili waisafishe nyumba ya Bwana.
2 Chroniques 30.12 1 Chroniques 23.28 2 Chroniques 29.5
16 Nao makuhani wakaingia nyumbani mwa Bwana, katika mahali pa ndani, ili waisafishe, wakatoa uchafu wote waliouona hekaluni mwa Bwana, wakautupa nje uani mwa nyumba ya Bwana. Walawi wakautwaa, ili wauchukue nje mpaka kijito cha Kidroni.
2 Chroniques 15.16 2 Chroniques 3.8 Exode 26.33-26.34 Matthieu 21.12-21.13 Hébreux 9.23-9.24
17 Basi wakaanza kutakasa siku ya kwanza ya mwezi wa kwanza, hata siku ya nane ya mwezi wakafika katika ukumbi wa Bwana; wakaitakasa nyumba ya Bwana katika muda wa siku nane; wakamaliza siku ya kumi na sita ya mwezi wa kwanza.
1 Rois 6.3 2 Chroniques 29.3 Exode 12.2-12.8 1 Chroniques 28.11 2 Chroniques 3.4
18 Wakaingia ndani kwa Hezekia mfalme, wakasema, Tumeisafisha nyumba yote ya Bwana, na madhabahu ya sadaka ya kuteketezwa, pamoja na vyombo vyake vyote, na meza ya mikate ya wonyesho, pamoja na vyombo vyake vyote.
2 Chroniques 4.1 2 Chroniques 4.7-4.8 2 Chroniques 13.11
19 Tena vyombo vyote alivyovitupa mfalme Ahazi alipotawala, hapo alipoasi, tumevitengeza na kuvitakasa; navyo, tazama, vipo mbele ya madhabahu ya Bwana.
2 Chroniques 28.24
20 Ndipo Hezekia mfalme akaamka mapema, akakusanya wakuu wa mji, akapanda nyumbani kwa Bwana.
Genèse 22.3 Jérémie 25.4 Exode 24.4 Josué 6.12
21 Wakaleta ng’ombe waume saba, na kondoo waume saba, na wana-kondoo saba, na mabeberu saba, kuwa sadaka ya dhambi kwa ajili ya ufalme, na kwa ajili ya patakatifu, na kwa ajili ya Yuda. Akaamuru makuhani, wana wa Haruni, wawatoe madhabahuni pa Bwana.
Lévitique 4.3-4.14 Nombres 23.29 Nombres 15.22-15.24 Nombres 23.14 1 Chroniques 15.26
22 Basi wakawachinja ng’ombe, na makuhani wakaipokea damu, wakainyunyiza madhabahuni; wakawachinja kondoo waume, na kuinyunyiza damu madhabahuni; wakawachinja na wana-kondoo, na kuinyunyiza damu madhabahuni.
Lévitique 4.18 Lévitique 8.19 Lévitique 8.24 Lévitique 4.34 Lévitique 8.14-8.15
23 Wakawaleta karibu mabeberu wa sadaka ya dhambi mbele ya mfalme na kusanyiko; wakawawekea mikono yao;
Lévitique 4.15 Lévitique 1.4 Lévitique 4.24
24 na makuhani wakawachinja, wakaitoa damu yao kuwa sadaka ya dhambi madhabahuni, ili kuwafanyia Israeli wote upatanisho; maana mfalme aliamuru Israeli wote wafanyiwe sadaka ya kuteketezwa na sadaka ya dhambi.
Colossiens 1.20-1.21 Ezéchiel 45.17 2 Corinthiens 5.18-5.21 Lévitique 4.13-4.35 Lévitique 8.15
25 Akawasimamisha Walawi nyumbani mwa Bwana wenye matoazi, wenye vinanda, na wenye vinubi, kama alivyoamuru Daudi, na Gadi mwonaji wa mfalme, na Nathani nabii; kwani Bwana aliamuru hivi kwa manabii wake.
2 Chroniques 8.14 1 Chroniques 23.5 2 Samuel 24.11 2 Samuel 7.2-7.4 2 Chroniques 30.12
26 Wakasimama Walawi wenye vinanda vya Daudi, na makuhani wenye mapanda.
1 Chroniques 23.5 1 Chroniques 15.24 Amos 6.5 Psaumes 81.3 Psaumes 87.7
27 Hezekia akaamuru kutoa sadaka ya kuteketezwa madhabahuni. Na wakati ilipoanza sadaka hiyo ya kuteketezwa, ukaanza na huo wimbo wa Bwana, na mapanda, pamoja na vinanda vya Daudi mfalme wa Israeli.
2 Chroniques 23.18 Psaumes 136.1 Psaumes 137.3-137.4 2 Chroniques 20.21 2 Chroniques 7.3
28 Na kusanyiko lote wakaabudu, waimbaji wakaimba, wenye mapanda wakapiga; haya yote yakaendelea hata ilipomalizika sadaka ya kuteketezwa.
Psaumes 89.15 Apocalypse 5.8-5.14 Psaumes 68.24-68.26
29 Hata walipokwisha kutoa sadaka, mfalme, na hao wote waliokuwapo naye, wakasujudia, wakaabudu.
2 Chroniques 20.18 Philippiens 2.10-2.11 Psaumes 72.11 Romains 14.11 1 Chroniques 29.20
30 Tena Hezekia mfalme na wakuu wakawaamuru Walawi, wamwimbie Bwana sifa kwa maneno ya Daudi, na ya Asafu mwonaji. Wakaimba sifa kwa furaha, wakainama vichwa, wakaabudu.
Psaumes 32.11-33.1 Psaumes 95.1-95.2 Philippiens 4.4 2 Samuel 23.1-23.2 Psaumes 100.1-100.2
31 Ndipo Hezekia akajibu, akasema, Sasa mmejifanya wakfu kwa Bwana, karibuni mkalete dhabihu na matoleo ya shukrani nyumbani mwa Bwana. Basi kusanyiko wakaleta dhabihu na matoleo ya shukrani; na wote wenye moyo wa ukarimu, wakaleta sadaka za kuteketezwa.
2 Chroniques 13.9 Exode 35.22 Lévitique 7.12 Exode 35.5 Esdras 1.4
32 Na hesabu ya sadaka hizo za kuteketezwa walizozileta kusanyiko ikawa ng’ombe waume sabini, kondoo waume mia, na wana-kondoo mia mbili; hao wote walikuwa ni sadaka ya kuteketezwa kwa Bwana.
1 Rois 8.63 1 Rois 3.4 1 Chroniques 29.21 Esdras 6.17
33 Na vitu vitakatifu vilikuwa ng’ombe mia sita, na kondoo elfu tatu.
34 Lakini makuhani walikuwa wachache, wasiweze kuchuna sadaka zote za kuteketezwa; basi ndugu zao Walawi wakawasaidia, hata ilipokwisha kazi, na hata makuhani walipojitakasa; kwa kuwa Walawi walikuwa wenye mioyo ya adili kwa kujitakasa kuliko makuhani.
2 Chroniques 35.11 2 Chroniques 30.3 Psaumes 94.15 2 Chroniques 30.16-30.17 Psaumes 26.6
35 Na tena sadaka za kuteketezwa nazo zilikuwa nyingi, pamoja na mafuta ya sadaka za amani, na sadaka za kinywaji kwa kila sadaka ya kuteketezwa. Hivyo ikatengezeka huduma ya nyumba ya Bwana.
Nombres 15.5-15.10 Exode 29.13 Lévitique 23.13 1 Corinthiens 14.40 Esdras 6.18
36 Akafurahi Hezekia, na watu wote, kwa sababu ya hayo Mungu aliyowatengenezea watu; maana jambo hilo likawa kwa ghafula.
2 Chroniques 30.12 Actes 2.41 Esdras 6.22 Psaumes 10.17 Proverbes 16.1

Cette Bible est dans le domaine public.