Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

2 Chroniques 27.4
Bible en Swahili de l’est


Règne de Jotham

1 Yothamu alikuwa na umri wa miaka ishirini na mitano alipoanza kutawala; akatawala katika Yerusalemu miaka kumi na sita; na jina la mamaye aliitwa Yerusha binti Sadoki.
1 Chroniques 3.12 Osée 1.1 Matthieu 1.9 Michée 1.1 Esaïe 1.1
2 Akafanya yaliyo ya adili machoni pa Bwana, sawasawa na yote aliyoyafanya Uzia babaye; isipokuwa hakuingia hekaluni mwa Bwana. Lakini watu walikuwa wakali kufanya maovu.
2 Rois 15.34-15.35 2 Chroniques 26.4 Psaumes 119.120 Actes 5.13 2 Chroniques 26.16-26.21
3 Ndiye aliyelijenga lango la juu la nyumba ya Bwana, na juu ya ukuta wa Ofeli akajenga sana.
2 Chroniques 33.14 Néhémie 3.26-3.27 Jérémie 20.2 2 Chroniques 23.20
4 Tena akajenga miji katika milima ya Yuda, na mwituni akajenga ngome na minara.
2 Chroniques 26.9-26.10 2 Chroniques 14.7 2 Chroniques 11.5-11.10 Luc 1.39 Josué 14.12-14.13
5 Kisha akapigana na mfalme wa wana wa Amoni, akawashinda. Na wana wa Amoni wakampa mwaka ule ule talanta mia za fedha, na kori elfu kumi za ngano, na elfu kumi za shayiri. Hayo ndiyo waliyomtolea wana wa Amoni, mwaka wa pili pia, na mwaka wa tatu.
Jérémie 49.1-49.6 2 Chroniques 20.1 2 Samuel 10.1-10.14 Juges 11.4-11.33
6 Basi Yothamu akawa na nguvu, kwa kuwa alizitengeneza njia zake mbele za Bwana, Mungu wake.
2 Chroniques 26.5 2 Chroniques 19.3
7 Na mambo yote ya Yothamu yaliyosalia, na vita vyake vyote, na njia zake, tazama, yameandikwa katika kitabu cha wafalme wa Israeli na Yuda.
2 Chroniques 26.22-26.23 2 Rois 15.36 2 Chroniques 32.32-32.33 2 Chroniques 20.34
8 Alikuwa na umri wa miaka ishirini na mitano alipoanza kutawala; akatawala miaka kumi na sita huko Yerusalemu.
2 Chroniques 27.1
9 Yothamu akalala na babaze, wakamzika katika mji wa Daudi; na Ahazi mwanawe akatawala mahali pake.
2 Rois 15.38

Cette Bible est dans le domaine public.