Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

2 Rois 22.6
Bible en Swahili de l’est


Règne de Josias sur Juda

1 Yosia alikuwa na umri wa miaka minane alipoanza kutawala; akatawala miaka thelathini na mmoja katika Yerusalemu; na jina la mama yake aliitwa Yedida, binti Adaya wa Bozkathi.
Josué 15.39 Ecclésiaste 10.16 2 Rois 21.1 2 Chroniques 34.1-34.33 2 Rois 11.21
2 Akafanya yaliyo mema machoni pa Bwana, akaenda katika njia yote ya Daudi baba yake, wala hakugeuka upande wa kuume wala wa kushoto.
Deutéronome 5.32 Josué 1.7 2 Chroniques 17.3 1 Rois 3.6 Ezéchiel 18.14-18.17
3 Ikawa, katika mwaka wa kumi na nane wa mfalme Yosia, mfalme akamtuma Shafani, mwana wa Azalia, mwana wa Meshulamu, mwandishi, nyumbani kwa Bwana, akisema,
2 Chroniques 34.3-34.33
4 Enenda kwa Hilkia, kuhani mkuu, ili aihesabu fedha yote inayoletwa nyumbani mwa Bwana, ambayo mabawabu wameipokea kwa watu;
2 Rois 12.4 Marc 12.41-12.42 2 Chroniques 34.9-34.18 1 Chroniques 26.13-26.19 1 Chroniques 6.13
5 tena waitie ile fedha katika mikono ya wafanya kazi wanaoisimamia nyumba ya Bwana; wakapewe wafanya kazi waliomo ndani ya nyumba ya Bwana, ili wapate kupatengeneza mahali palipobomoka ndani ya nyumba;
2 Rois 12.11-12.14 2 Rois 12.5 Esdras 3.7 2 Chroniques 24.27 2 Chroniques 24.7
6 wapewe maseremala, na wajenzi, na waashi; ili kununua miti na mawe yaliyochongwa wapate kuitengeneza nyumba.
7 Lakini hawakuulizwa habari za ile fedha waliyokabidhiwa; maana walitenda kazi kwa uaminifu.
2 Rois 12.15 1 Corinthiens 4.2 Néhémie 7.2 2 Chroniques 24.14 2 Corinthiens 8.20-8.21
8 Naye Hilkia, kuhani mkuu, akamwambia Shafani, mwandishi, Nimekiona kitabu cha torati katika nyumba ya Bwana. Hilkia akampa Shafani kile kitabu, naye akakisoma.
Deutéronome 31.24-31.26 2 Chroniques 34.14-34.28
9 Shafani mwandishi akamwendea mfalme, akamletea mfalme habari tena, akasema, Watumishi wako wamezitoa zile fedha zilizoonekana ndani ya nyumba, nao wamewakabidhi wafanya kazi wanaoisimamia nyumba ya Bwana.
Jérémie 29.3 Jérémie 36.10-36.12 Jérémie 39.14 2 Rois 18.18 Ezéchiel 8.11
10 Kisha Shafani mwandishi akamwambia mfalme, akasema, Hilkia kuhani amenipa kitabu. Shafani akakisoma mbele ya mfalme.
Jérémie 36.21 Jérémie 13.18 Deutéronome 31.9-31.13 Jérémie 36.6 2 Chroniques 34.18
11 Ikawa, mfalme alipokwisha kuyasikia maneno ya kitabu hicho cha torati, alirarua nguo zake.
2 Rois 22.19 2 Chroniques 34.19 Jonas 3.6-3.7 Joël 2.13 Jérémie 36.24
12 Mfalme akamwamuru Hilkia kuhani, na Ahikamu, mwana wa Shafani, na Akbori, mwana wa Mikaya, na Shafani mwandishi, na Asaya, mtumishi wa mfalme akasema,
Jérémie 26.24 2 Rois 25.22 Esaïe 37.1-37.4 2 Rois 19.2-19.3 2 Chroniques 34.19-34.21
13 Enendeni, mkamwulize Bwana kwa ajili yangu, na kwa ajili ya watu hawa, na kwa ajili ya Yuda yote, katika habari za maneno ya kitabu hiki kilichoonekana; kwa kuwa hasira ya Bwana ni kubwa aliyotukasirikia, kwa sababu baba zetu hawakuyaangalia maneno ya kitabu hiki, kufanya kama hayo yote tuliyoandikiwa.
Deutéronome 29.23-29.28 Deutéronome 31.17-31.18 Jérémie 37.17 Romains 3.20 Néhémie 8.8-8.9
14 Basi Hilkia kuhani, na Ahikamu, na Akbori, na Shafani, na Asaya, wakamwendea Hulda, nabii mke, mkewe Shalumu, mwana wa Tikva, mwana wa Harhasi, mtunza mavazi ya mfalme; (naye alikaa Yerusalemu katika mtaa wa pili;) wakasema naye.
2 Chroniques 34.22 Sophonie 1.10 2 Rois 10.22 Luc 1.41-1.56 1 Corinthiens 11.5
15 Akawaambia, Bwana, Mungu wa Israeli, asema hivi; Mwambieni mtu yule aliyewatuma ninyi kwangu,
2 Rois 1.6 2 Rois 1.16 Jérémie 23.28
16 Bwana asema hivi, Tazama, mimi nitaleta uovu juu ya mahali hapa, na juu yao wakaao hapa, naam, maneno yote ya kitabu alichokisoma mfalme wa Yuda;
Josué 23.15 Daniel 9.11-9.14 Deutéronome 28.15-28.68 Josué 23.13 Deutéronome 32.15-32.26
17 kwa sababu wameniacha mimi, wameifukizia uvumba miungu mingine, ili wapate kunikasirisha kwa kazi yote ya mikono yao; kwa hiyo hasira yangu itawaka juu ya mahali hapa, isizimike.
Sophonie 1.18 1 Rois 9.6-9.9 Juges 3.7-3.8 Jérémie 2.27-2.28 1 Thessaloniciens 2.16
18 Lakini yule mfalme wa Yuda, aliyewatuma ninyi kumwuliza Bwana, mtamwambia hivi, Bwana, Mungu wa Israeli, asema hivi, Kwa habari ya maneno yale uliyoyasikia,
Malachie 3.16-3.17 Esaïe 3.10 2 Chroniques 34.26-34.28
19 kwa kuwa moyo wako ulikuwa mwororo, nawe ukajinyenyekesha mbele za Bwana, hapo ulipoyasikia maneno niliyoyanena juu ya mahali hapa, na juu ya wenyeji wake, ya kwamba watakuwa ukiwa na laana, nawe ulizirarua nguo zako, ukalia mbele zangu; basi, mimi nami nimekusikia wewe, asema Bwana.
1 Rois 21.29 Jérémie 26.6 Psaumes 51.17 Exode 10.3 Jérémie 44.22
20 Kwa hiyo tazama, nitakukusanya pamoja na baba zako, nawe utawekwa kaburini mwako kwa amani; wala macho yako hayatauona uovu huo wote nitakaouleta juu ya mahali hapa. Basi wakamletea mfalme habari tena.
1 Chroniques 17.11 Esaïe 57.1-57.2 Psaumes 37.37 Jérémie 22.10 Genèse 25.8

Cette Bible est dans le domaine public.