Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

2 Samuel 17.28
Bible en Swahili de l’est


1 Zaidi ya hayo Ahithofeli akamwambia Absalomu, Niache nichague watu kumi na mbili elfu, nami nitaondoka na kumfuatia Daudi usiku huu;
Psaumes 109.2-109.4 Psaumes 3.3-3.5 Proverbes 4.16 Esaïe 59.7-59.8 Psaumes 4.8
2 nami nitamshambulia wakati atakaokuwa amechoka, na mikono yake imekuwa dhaifu, nami nitamtia hofu; na watu wote walio pamoja naye watakimbia; nami nitampiga mfalme peke yake;
1 Rois 22.31 2 Samuel 16.14 Zacharie 13.7 Jean 11.50 Matthieu 21.38
3 na hao watu wote nitawarejeza kwako; mtu yule umtafutaye ni kana kwamba wamerudi wote; na hivyo watu wote watakuwa katika amani.
1 Thessaloniciens 5.3 Esaïe 48.22 2 Samuel 3.21 Esaïe 57.21
4 Shauri hili likawa jema machoni pa Absalomu, na machoni pa wazee wote wa Israeli.
1 Samuel 18.20-18.21 2 Chroniques 30.4 Esther 5.14 Esther 1.21 1 Samuel 23.21
5 Ndipo Absalomu akasema, Basi, mwiteni Hushai, Mwarki, naye, tukasikie atakayosema yeye pia.
2 Samuel 15.32-15.37 2 Samuel 16.16-16.19
6 Basi Hushai alipofika kwa Absalomu, Absalomu akamwambia, akasema, Ahithofeli amesema hivi; je! Tufanye kama alivyosema? Kama sivyo, sema maneno yako.
7 Hushai akamwambia Absalomu, Shauri hili alilolitoa Ahithofeli si jema wakati huu.
Proverbes 31.8
8 Hushai akafuliza kusema, Wamjua baba yako na watu wake, ya kuwa ni watu mashujaa hawa, nao wana uchungu katika mioyo yao, kama dubu aliyenyang’anywa watoto wake nyikani; tena baba yako ni mtu wa vita, hatalala pamoja na watu wake.
Osée 13.8 1 Samuel 16.18 Proverbes 17.12 Hébreux 11.32-11.34 Daniel 7.5
9 Angalia, amefichwa sasa katika shimo, au penginepo; kisha itakuwa, watakapoanguka baadhi yao mwanzo, kila mtu atakayesikia, atasema, Kuna machinjo katika watu wanaofuatana na Absalomu.
1 Samuel 24.3 1 Samuel 22.1 Josué 8.6 1 Samuel 14.14-14.15 Josué 7.5
10 Basi hata yeye aliye shujaa, mwenye moyo kama moyo wa simba, atayeyuka kabisa; maana Israeli wote wanajua ya kuwa baba yako ni shujaa, na ya kuwa watu wale walio pamoja naye ni mashujaa.
Josué 2.9-2.11 Hébreux 11.34 Nombres 24.8-24.9 2 Samuel 23.20 1 Samuel 18.17
11 Kwa hiyo shauri langu ni hili, Waisraeli wote toka Dani mpaka Beer-sheba wakusanyike kwako, kama mchanga wa bahari kwa wingi; na wewe uende vitani mwenyewe.
Genèse 22.17 Juges 20.1 Josué 11.4 2 Samuel 24.2 Genèse 13.16
12 Hivyo tutamfikia mahali po pote atakapoonekana, na kumwangukia kama vile umande uangukavyo juu ya nchi; wala hatutaacha hata mmoja wao, yeye na watu wote walio pamoja naye.
2 Rois 18.23 Esaïe 10.13-10.14 Abdias 1.3 1 Rois 20.10 1 Samuel 23.23
13 Tena, ikiwa amejitia katika mji uwao wote, basi Israeli wote wataleta kamba, na kuuendea mji ule, nasi tutaukokota mpaka mtoni, wala halitaonekana huko hata jiwe dogo moja la mawe yake.
Michée 1.6 Matthieu 24.2
14 Naye Absalomu na watu wote wa Israeli wakasema, Shauri la Hushai, Mwarki, ni jema kuliko shauri la Ahithofeli. Kwa maana Bwana alikuwa amekusudia kulivunja shauri jema la Ahithofeli, ili Bwana alete mabaya juu ya Absalomu.
2 Samuel 15.34 2 Samuel 15.31 2 Samuel 16.23 Proverbes 19.21 Psaumes 9.16
15 Ndipo Hushai akawaambia Sadoki na Abiathari, makuhani, Ahithofeli amempa Absalomu na wazee wa Israeli mashauri kadha wa kadha; na mimi nimetoa mashauri kadha wa kadha.
2 Samuel 15.35-15.36
16 Basi sasa pelekeni habari upesi kamwambieni Daudi ya kwamba, Usilale usiku huu karibu na vivuko vya jangwani; bali usikose kuvuka; asije akamezwa mfalme, na watu wote walio pamoja naye.
2 Samuel 15.28 2 Corinthiens 5.4 1 Corinthiens 15.54 Psaumes 56.2 2 Samuel 17.21-17.22
17 Basi Yonathani na Ahimaasi walikuwa wakikaa karibu na Enrogeli; na mjakazi mmoja alikuwa akienda na kuwapa habari; nao huenda kumwambia mfalme Daudi; maana ilikuwa lazima wasionekane wakiingia mjini.
Josué 18.16 2 Samuel 15.36 Josué 15.7 2 Samuel 15.27 Josué 2.4-2.24
18 Lakini kijana mmoja aliwaona, akamwambia Absalomu; basi wakaenda wote wawili kwa haraka, wakafika Bahurimu, nyumbani kwa mtu aliyekuwa na kisima uani mwake; wakashuka ndani yake.
2 Samuel 3.16 2 Samuel 16.5 2 Samuel 19.16
19 Na mwanamke akatwaa kifuniko akakiweka juu ya mdomo wa kile kisima, akaanika ngano iliyotwangwa juu yake; wala halikujulikana neno lo lote.
Josué 2.4-2.24 Exode 1.19
20 Nao watumishi wa Absalomu wakamwendea yule mwanamke mle nyumbani; wakasema, Wako wapi Yonathani na Ahimaasi? Yule mwanamke akawaambia, Wamevuka kijito cha maji. Basi walipokwisha kuwatafuta wasiwaone, wakarudi Yerusalemu.
Exode 1.19 Josué 2.22-2.23 1 Samuel 19.12-19.17 2 Samuel 15.34 Josué 2.3-2.5
21 Kisha ikawa, baada ya kuondoka kwao, wale wakatoka kisimani, wakaenda wakamwarifu mfalme Daudi; wakamwambia Daudi, Ondokeni, mkavuke maji haya upesi; maana ndivyo alivyotoa shauri Ahithofeli juu yenu.
2 Samuel 17.15-17.16
22 Ndipo Daudi, na watu wote waliokuwa pamoja naye, wakaondoka, wakavuka Yordani; na kulipopambazuka hakubaki mmojawapo wao asiyevuka Yordani.
Proverbes 27.12 2 Samuel 17.24 Nombres 31.49 Matthieu 10.16 Jean 18.9
23 Naye Ahithofeli alipoona ya kuwa shauri lake halikufuatwa, akatandika punda wake, akaondoka, akaenda nyumbani kwake, mjini mwake, akaitengeneza nyumba yake, akajisonga; akafa, akazikwa kaburini mwa babaye.
2 Samuel 15.12 Matthieu 27.5 2 Rois 20.1 1 Rois 16.18 Psaumes 5.10
24 Basi Daudi akaja Mahanaimu. Naye Absalomu akauvuka Yordani yeye na watu wote wa Israeli pamoja naye.
2 Samuel 2.8 Genèse 32.2 Josué 13.26
25 Naye Absalomu akamweka Amasa awe juu ya jeshi mahali pa Yoabu. Basi huyo Amasa alikuwa mwana wa mtu, jina lake Yetheri, Mwishmaeli, aliyeingia kwa Abigali, binti Nahashi, nduguye Seruya, mamaye Yoabu.
2 Samuel 19.13 1 Chroniques 2.13 2 Samuel 20.9-20.12 1 Chroniques 2.16-2.17 2 Samuel 20.4
26 Israeli na Absalomu wakapiga kambi katika nchi ya Gileadi.
Nombres 32.1-32.42 Josué 17.1 Deutéronome 3.15
27 Ikawa, Daudi alipofika Mahanaimu, Shobi, mwana wa Nahashi wa Raba, wa wana wa Amoni, na Makiri, mwana wa Amieli wa Lo-debari, na Barzilai, Mgileadi wa Rogelimu,
2 Samuel 9.4 2 Samuel 10.1-10.2 1 Rois 2.7 1 Samuel 11.1 Esdras 2.61
28 wakaleta magodoro, na mabakuli, na vyungu, na ngano, na shayiri, na unga, na bisi, na kunde, na dengu,
1 Samuel 25.18 2 Samuel 16.1-16.2 Abdias 1.3 Esaïe 32.8
29 na asali, na siagi, na kondoo, na samli ya ng’ombe, wapate kula Daudi na watu waliokuwa pamoja naye; kwani walisema, Watu hao waona njaa, tena wamechoka, nao wana kiu huku nyikani.
2 Samuel 16.2 2 Samuel 16.14 Psaumes 34.8-34.10 Romains 12.13 Esaïe 58.7

Cette Bible est dans le domaine public.