Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

2 Samuel 12.13
Bible en Swahili de l’est


1 Ndipo Bwana akamtuma Nathani aende kwa Daudi. Naye akamwendea, akamwambia, Palikuwa na watu wawili katika mji mmoja; mmoja wao alikuwa tajiri, wa pili maskini.
1 Rois 20.35-20.41 2 Samuel 24.11-24.13 2 Samuel 7.17 1 Rois 13.1 Esaïe 57.17-57.18
2 Yule tajiri alikuwa na kondoo na ng’ombe wengi sana;
2 Samuel 3.2-3.5 2 Samuel 5.13-5.16 2 Samuel 15.16 Job 1.3 2 Samuel 12.8
3 bali yule maskini hakuwa na kitu, ila mwana kondoo mmoja, mdogo, ambaye amemnunua na kumlea; naye akakua pamoja naye, na pamoja na wanawe; hula sehemu ya posho lake, na kukinywea kikombe chake, na kulala kifuani mwake, akawa kwake kama binti.
2 Samuel 11.3 Proverbes 5.18-5.19 Michée 7.5 Deutéronome 13.6
4 Hata msafiri mmoja akamfikilia yule tajiri, naye akaacha kutwaa mmoja wa kondoo zake mwenyewe au mmoja wa ng’ombe zake mwenyewe, ili kumwandalia yule msafiri aliyemfikilia, bali alimnyang’anya yule maskini mwana-kondoo wake, akamwandalia yule mtu aliyemfikilia.
Jacques 1.14 Genèse 18.2-18.7 2 Samuel 11.3-11.4
5 Ndipo hasira ya Daudi ikawaka sana juu ya mtu yule; akamwambia Nathani, Aishivyo Bwana, mtu huyo aliyetenda jambo hili, hakika yake astahili kufa;
Luc 6.41-6.42 1 Samuel 26.16 Romains 2.1 Genèse 38.24 1 Samuel 20.31
6 naye atamrudishia yule mwana-kondoo mara nne, kwa sababu ametenda neno hili, na kwa sababu hakuwa na huruma.
Exode 22.1 Luc 19.8 Jacques 2.13 Proverbes 6.31
7 Basi Nathani akamwambia Daudi, Wewe ndiwe mtu huyo. Bwana, Mungu wa Israeli, asema hivi, Nalikutia mafuta, uwe mfalme juu ya Israeli, nikakuokoa na mkono wa Sauli;
1 Samuel 16.13 Psaumes 18.1 1 Samuel 18.11 1 Rois 20.42 1 Rois 21.19-21.20
8 nami nikakupa nyumba ya bwana wako, na wake za bwana wako kifuani mwako; nikakupa nyumba ya Israeli na ya Yuda; na kama hayo yangalikuwa machache, ningalikuongezea mambo kadha wa kadha.
2 Samuel 12.11 Romains 8.32 Psaumes 86.15 1 Rois 2.22 Psaumes 84.11
9 Kwa nini umelidharau neno la Bwana, na kufanya yaliyo mabaya machoni pake? Umempiga Uria, Mhiti, kwa upanga, nawe umemtwaa mkewe awe mke wako, nawe umemwua huyo kwa upanga wa wana wa Amoni.
1 Samuel 15.19 1 Samuel 15.23 Hébreux 10.28-10.29 Psaumes 90.8 2 Samuel 11.4
10 Basi, sasa upanga hautaondoka nyumbani mwako, kwa sababu umenidharau, ukamtwaa mkewe Uria, Mhiti, kuwa mke wako.
2 Samuel 18.14-18.15 Matthieu 6.24 Malachie 1.6-1.7 2 Samuel 18.33 Nombres 11.20
11 Bwana asema hivi, Angalia, nitakuondokeshea uovu katika nyumba yako, nami nitawatwaa wake zako mbele ya macho yako, na kumpa jirani yako, naye atalala na wake zako mbele ya jua hili.
Deutéronome 28.30 2 Samuel 16.21-16.22 Osée 4.13-4.14 Ezéchiel 14.9 2 Samuel 13.28-13.29
12 Maana wewe ulifanya jambo lile kwa siri; bali mimi nitalifanya jambo hili mbele ya Israeli wote na mbele ya jua.
2 Samuel 16.22 Luc 12.1-12.2 Ecclésiaste 12.14 2 Samuel 11.4-11.15 1 Corinthiens 4.5
13 Daudi akamwambia Nathani, Nimemfanyia Bwana dhambi. Nathani akamwambia Daudi, Bwana naye ameiondoa dhambi yako; hutakufa.
2 Samuel 24.10 Proverbes 28.13 Lévitique 20.10 1 Samuel 15.30 Psaumes 51.4
14 Lakini, kwa kuwa kwa tendo hili umewapa adui za Bwana nafasi kubwa ya kukufuru, mtoto atakayezaliwa kwako hakika yake atakufa.
Romains 2.24 Esaïe 52.5 Psaumes 89.31-89.33 Psaumes 74.10 Hébreux 12.6
15 Naye Nathani akaondoka kwenda nyumbani kwake. Basi Bwana akampiga yule mtoto ambaye mkewe Uria alimzalia Daudi naye akawa hawezi sana.
1 Samuel 25.38 2 Chroniques 13.20 Actes 12.23 2 Rois 15.5 Psaumes 104.29
16 Basi Daudi akamwomba Mungu kwa ajili ya mtoto; Daudi akafunga, akaingia, akalala usiku kucha chini.
2 Samuel 13.31 Actes 9.9 2 Samuel 12.22 Job 20.12-20.14 Psaumes 69.10
17 Nao wazee wa nyumba yake wakaondoka, wakasimama karibu naye, ili wamwinue katika nchi; lakini hakukubali, wala hakula chakula pamoja nao.
2 Samuel 3.35 1 Samuel 28.23
18 Ikawa siku ya saba, yule mtoto akafa. Nao watumishi wa Daudi wakaogopa kumwambia ya kuwa mtoto amekufa, maana, walisema, Angalieni, yule mtoto alipokuwa angali hai, tulisema naye, asitusikilize sauti zetu; basi hatazidi kujisumbua, tukimwambia ya kuwa mtoto amekufa?
Nombres 20.15
19 Lakini alipoona ya kuwa watumishi wake wananong’onezana, Daudi alitambua ya kuwa mtoto amekufa; basi Daudi akawauliza watumishi wake, Je! Mtoto amekufa? Nao wakasema, Amekufa.
20 Ndipo Daudi akainuka pale chini akaoga, akajipaka mafuta, akabadili mavazi yake; akaingia nyumbani mwa Bwana, akasali; kisha akaenda nyumbani kwake, na alipotaka wakamwandalia chakula, naye akala.
Job 1.20 Ruth 3.3 Ecclésiaste 9.8 Lamentations 3.39-3.41 2 Samuel 6.17
21 Watumishi wake wakamwambia, Ni neno gani hili ulilolitenda? Ulifunga na kulia kwa ajili ya mtoto, alipokuwa hai; lakini mtoto alipokuwa amekufa, uliinuka ukala chakula.
1 Corinthiens 2.15
22 Akasema, Mtoto alipokuwa hai, nalifunga, nikalia; kwa maana nalisema, Ni nani ajuaye kwamba Bwana atanihurumia, mtoto apate kuishi?
Esaïe 38.1-38.3 Esaïe 38.5 Jonas 3.9-3.10 Jacques 4.9-4.10 Joël 1.14
23 Lakini sasa amekufa nifungie nini? Je! Naweza kumrudisha tena? Mimi nitakwenda kwake lakini yeye hatanirudia mimi.
Genèse 37.35 Job 7.8-7.10 Job 30.23 Luc 23.43
24 Naye Daudi akamfariji Bath-sheba mkewe, akaingia kwake, akalala naye; naye akazaa mwana, akamwita jina lake Sulemani. Naye Bwana akampenda;
Matthieu 1.6 1 Chroniques 28.5-28.6 1 Chroniques 29.1 2 Samuel 7.12 1 Chroniques 22.9-22.10
25 akapeleka kwa mkono wa Nathani, nabii, naye akamwita jina lake Yedidia, kwa ajili ya Bwana.
Néhémie 13.26 Matthieu 3.17 1 Rois 1.11 1 Rois 1.23 2 Samuel 7.4

Prise de Rabba par David et Joab

26 Yoabu akapigana juu ya Raba wa wana wa Amoni, akautwaa mji wa kifalme.
1 Chroniques 20.1-20.3 Deutéronome 3.11 2 Samuel 11.25
27 Yoabu akatuma wajumbe waende kwa Daudi, kusema Nimeshindana na Raba, hata nimeutwaa huo mji wa maji.
Ezéchiel 21.20 2 Samuel 11.1 Deutéronome 3.11
28 Basi sasa kusanya watu waliobaki, ukauzunguke mji, na kuutwaa; nisije mimi nikautwaa mji, ukaitwe jina langu.
Jean 7.18
29 Basi Daudi akawakusanya watu wote akaenda Raba, akapigana nao, akautwaa.
30 Kisha akamnyang’anya mfalme wao taji toka kichwani pake; na uzani wake ulikuwa talanta ya dhahabu, nayo ilikuwa na vito vya thamani ndani yake; akavikwa Daudi kichwani. Akazitoa nyara za huo mji, nyingi sana.
1 Chroniques 20.2
31 Naye akawatoa watu waliokuwamo, akawaweka kwenye kazi ya misumeno,na sululu za chuma,na mashoka ya chuma,akawatumikisha,tanuuni mwa matofali ndivyo alivyoifanya miji yote ya wana wa Amoni.Kisha Daudi akarudi na watu wote Yerusalemu.
1 Chroniques 20.3 Psaumes 21.8-21.9 Amos 1.3 2 Samuel 8.2

Cette Bible est dans le domaine public.