Accueil  /  Bible  /  Bible en Swahili de l’est  /  Psaumes 54.2

La Bible Bible en Swahili de l’est

Psaumes 54

Un clic sur un verset envoie vers le comparateur de versions.

Chapitre 53 Chapitre 55

Prière confiante pour la délivrance

1 Ee Mungu, kwa jina lako uniokoe, Na kwa uweza wako unifanyie hukumu.
2 Ee Mungu, uyasikie maombi yangu, Uyasikilize maneno ya kinywa changu.
3 Kwa maana wageni wamenishambulia; Watu watishao wananitafuta nafsi yangu; Hawakumweka Mungu mbele yao.
4 Tazama, Mungu ndiye anayenisaidia; Bwana ndiye anayenitegemeza nafsi yangu.
5 Atawarudishia adui zangu ubaya wao; Uwaangamize kwa uaminifu wako.
6 Kwa ukunjufu wa moyo nitakutolea dhabihu; Ee Bwana, nitalishukuru jina lako, maana ni jema.
7 Kwa kuwa limeniokoa na kila taabu; Na jicho langu limeridhika Kwa kuwatazama adui zangu.

Vous êtes actuellement sur une version optimisée pour mobile, si vous souhaitez basculer sur la version complète suivez le lien suivant : Psaumes 54.2 (Lemaîtstre de Sacy)

Cette Bible est dans le domaine public.