Accueil  /  Bible  /  Bible en Swahili de l’est  /  Psaumes 47.7

La Bible Bible en Swahili de l’est

Psaumes 47

Un clic sur un verset envoie vers le comparateur de versions.

Chapitre 46 Chapitre 48

La souveraineté de Dieu

1 Enyi watu wote, pigeni makofi, Mpigieni Mungu kelele kwa Sauti ya shangwe.
2 Kwa kuwa Bwana Aliye juu, mwenye kuogofya, Ndiye mfalme mkuu juu ya dunia yote.
3 Atawatiisha watu wa nchi chini yetu, Na mataifa chini ya miguu yetu.
4 Atatuchagulia urithi wetu, Fahari ya Yakobo ambaye alimpenda.
5 Mungu amepaa kwa kelele za shangwe, Bwana kwa sauti ya baragumu.
6 Mwimbieni Mungu, naam, imbeni; Mwimbieni mfalme wetu, naam, imbeni.
7 Maana Mungu ndiye mfalme wa dunia yote, Imbeni kwa akili.
8 Mungu awamiliki mataifa, Mungu ameketi katika kiti chake kitakatifu.
9 Wakuu wa watu wamekusanyika, Wawe watu wa Mungu wa Ibrahimu. Maana ngao za dunia zina Mungu, Ametukuka sana.

Vous êtes actuellement sur une version optimisée pour mobile, si vous souhaitez basculer sur la version complète suivez le lien suivant : Psaumes 47.7 (Lemaîtstre de Sacy)

Cette Bible est dans le domaine public.