Accueil  /  Bible  /  Bible en Swahili de l’est  /  Psaumes 4.2

La Bible Bible en Swahili de l’est

Psaumes 4

Un clic sur un verset envoie vers le comparateur de versions.

Chapitre 3 Chapitre 5

La sécurité qu’accorde l’Éternel

1 Ee Mungu wa haki yangu, uniitikie niitapo; Umenifanyizia nafasi wakati wa shida; Unifadhili na kuisikia sala yangu.
2 Enyi wanadamu, hata lini utukufu wangu utafedheheka? Je! Mtapenda ubatili na kutafuta uongo?
3 Bali jueni ya kuwa Bwana amejiteulia mtauwa; Bwana atasikia nimwitapo.
4 Mwe na hofu wala msitende dhambi, Tafakarini vitandani mwenu na kutulia.
5 Toeni dhabihu za haki, Na kumtumaini Bwana.
6 Wengi husema, Nani atakayetuonyesha mema? Bwana, utuinulie nuru ya uso wako.
7 Umenitia furaha moyoni mwangu, Kupita yao wanapozidishiwa nafaka na divai.
8 Katika amani nitajilaza na kupata usingizi mara, Maana Wewe, Bwana, peke yako, Ndiwe unijaliaye kukaa salama.

Vous êtes actuellement sur une version optimisée pour mobile, si vous souhaitez basculer sur la version complète suivez le lien suivant : Psaumes 4.2 (Lemaîtstre de Sacy)

Cette Bible est dans le domaine public.