Accueil  /  Bible  /  Bible en Swahili de l’est  /  Psaumes 113

La Bible Bible en Swahili de l’est

Psaumes 113

Un clic sur un verset envoie vers le comparateur de versions.

Chapitre 112 Chapitre 114

Bonté de Dieu pour les faibles

1 Haleluya. Enyi watumishi wa Bwana, sifuni, Lisifuni jina la Bwana.
2 Jina la Bwana lihimidiwe Tangu leo na hata milele.
3 Toka maawio ya jua hata machweo yake Jina la Bwana husifiwa.
4 Bwana ni mkuu juu ya mataifa yote, Na utukufu wake ni juu ya mbingu.
5 Ni nani aliye mfano wa Bwana, Mungu wetu aketiye juu;
6 Anyenyekeaye kutazama, Mbinguni na duniani?
7 Humwinua mnyonge kutoka mavumbini, Na kumpandisha maskini kutoka jaani.
8 Amketishe pamoja na wakuu, Pamoja na wakuu wa watu wake.
9 Huweka nyumbani mwanamke aliye tasa, Awe mama ya watoto mwenye furaha.


Vous êtes actuellement sur une version optimisée pour mobile, si vous souhaitez basculer sur la version complète suivez le lien suivant : Psaumes 113.1 (Lemaîtstre de Sacy)

Cette Bible est dans le domaine public.