Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Osée 14.9
Bible en Swahili de l’est


1 Ee Israeli, mrudie Bwana, Mungu wako; maana umeanguka kwa sababu ya uovu wako.
Osée 12.6 Osée 6.1 Osée 13.9 2 Chroniques 30.6-30.9 Jérémie 4.1

Appel à revenir à Dieu et promesses

2 Chukueni maneno pamoja nanyi, mkamrudie Bwana; mkamwambie, Ondoa maovu yote, uyatakabali yaliyo mema; na hivyo ndivyo mtakavyotoa sadaka za midomo yetu kana kwamba ni ng’ombe.
Hébreux 13.15 Psaumes 69.30-69.31 Luc 18.13 2 Samuel 24.10 Michée 7.18-7.19
3 Ashuru hatatuokoa; hatutapanda farasi; wala hatutaiambia tena kazi ya mikono yetu, Ninyi ndinyi miungu yetu; maana kwako wewe wasio na baba hupata rehema.
Psaumes 68.5 Psaumes 10.14 Psaumes 33.17 Esaïe 30.16 Osée 2.17
4 Mimi nitawaponya kurudi nyuma kwao; nitawapenda kwa ukunjufu wa moyo; kwa maana hasira yangu imemwacha.
Osée 6.1 Jérémie 3.22 Esaïe 57.18 Sophonie 3.17 Esaïe 12.1
5 Nitakuwa kama umande kwa Israeli; naye atachanua maua kama nyinyoro, na kuieneza mizizi yake kama Lebanoni.
Esaïe 35.2 Matthieu 6.28 Deutéronome 32.2 Job 29.19 Esaïe 27.6
6 Matawi yake yatatandaa, na uzuri wake utakuwa kama uzuri wa mzeituni, na harufu yake kama Lebanoni.
Psaumes 52.8 Daniel 4.10-4.15 Ezéchiel 17.5-17.8 Matthieu 13.31 Philippiens 4.18
7 Na wao wakaao chini ya uvuli wake watarejea; watafufuka kama ngano, na kuchanua maua kama mzabibu; harufu yake itakuwa kama harufu ya divai ya Lebanoni.
Psaumes 91.1 Jean 11.25 1 Corinthiens 15.36-15.38 Esaïe 32.1-32.2 Jean 12.24
8 Efraimu atasema, Mimi nina nini tena na sanamu? Mimi nimeitika, nami nitamwangalia. Mimi ni kama mberoshi wenye majani mabichi. Kwangu mimi yamepatikana matunda yako.
Job 34.32 Esaïe 41.19 1 Pierre 4.3-4.4 Luc 15.20 Job 33.27
9 Ni nani aliye na hekima, naye atayafahamu mambo haya? Ni nani aliye na busara, naye atayajua? Kwa maana njia za Bwana zimenyoka, nao wenye haki watakwenda katika njia hizo; bali waasio wataanguka ndani yake.
Psaumes 107.43 Proverbes 10.29 Jérémie 9.12 Sophonie 3.5 Daniel 12.10

Cette Bible est dans le domaine public.