Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Job 18.10
Bible en Swahili de l’est


Intervention n° 2 de Bildad

1 Ndipo Bildadi, Mshuhi, akajibu, na kusema,
Job 2.11 Job 8.1 Job 42.7-42.9 Job 25.1
2 Je! Hata lini utayategea maneno mitambo? Fikiri, kisha baadaye tutanena.
Job 21.2 Proverbes 18.13 Job 13.5-13.6 Job 8.2 Job 11.2
3 Twahesabiwa kuwa wanyama kwa sababu gani, Tena kuwa wanajisi machoni pako?
Psaumes 73.22 Job 17.10 Job 17.4 Romains 12.10 Job 12.7-12.8
4 Wewe ujiraruaye mwenyewe katika hasira yako, Je! Dunia itaachwa kwa ajili yako wewe? Au jabali litaondolewa mahali pake?
Job 16.9 Job 14.18 Job 13.14 Matthieu 24.35 Luc 9.39
5 Naam, mwanga wa waovu utazimika, Wala mwali wa moto wake hautang’aa.
Proverbes 13.9 Proverbes 24.20 Proverbes 20.20 Job 21.17 Job 20.5
6 Mwanga hemani mwake utakuwa giza, Nayo taa iliyo juu yake itazimishwa.
Psaumes 18.28 Job 21.17 Apocalypse 18.23
7 Hatua zake za nguvu zitasongwa, Na shauri lake mwenyewe litamwangusha chini.
Proverbes 4.12 Psaumes 18.36 Osée 10.6 1 Corinthiens 3.19 Job 15.6
8 Kwani ametupwa katika wavu na miguu yake mwenyewe, Naye huenda juu ya matanzi.
Psaumes 9.15 Job 22.10 Psaumes 35.8 Ezéchiel 32.3 Esther 3.9
9 Tanzi litamshika kisigino chake, Na mtambo utamgwia.
Job 1.15 Job 1.17 Esaïe 8.14-8.15 Job 5.5
10 Amefichiwa tanzi chini, Na mtego amewekewa njiani.
Ezéchiel 12.13 Romains 11.9 Psaumes 11.6
11 Matisho yatamtia hofu pande zote, Na kumfukuza karibu na visigino vyake.
Job 15.21 Jérémie 6.25 Lévitique 26.36 Jérémie 49.29 Jérémie 46.5
12 Nguvu zake zitaliwa na njaa, Na msiba utakuwa tayari kwa kusita kwake.
Esaïe 8.21 1 Thessaloniciens 5.3 Psaumes 34.10 1 Samuel 2.5 Psaumes 7.12-7.14
13 Utakula via vya mwili wake, Naam, mzaliwa wa kwanza wa mauti atavila via vyake.
Esaïe 14.30 Apocalypse 6.8 Zacharie 14.12 Jonas 2.6 Job 17.16
14 Atang’olewa katika hema yake aliyokuwa akiitumaini; Naye atapelekwa kwake mfalme wa utisho.
Proverbes 10.28 Psaumes 55.4 1 Corinthiens 15.55-15.56 Job 8.14 Job 11.20
15 Ambacho si chake kitakaa katika hema yake; Kiberiti kitamwagwa juu ya makazi yake.
Psaumes 11.6 Deutéronome 29.23 Esaïe 34.9-34.10 Apocalypse 21.8 Job 31.38-31.39
16 Chini, mizizi yake itakaushwa; Na juu, tawi lake litasinyaa.
Osée 9.16 Job 15.30 Malachie 4.1 Amos 2.9 Esaïe 5.24
17 Kumbukumbu lake litakoma katika nchi, Wala hatakuwa na jina mashambani.
Proverbes 10.7 Psaumes 34.16 Psaumes 109.13 Proverbes 2.22 Job 13.12
18 Atakimbizwa kutoka mwangani hata gizani, Na kufukuzwa atoke duniani.
Job 20.8 Job 10.22 Jude 1.13 Job 3.20 Daniel 5.21
19 Hatakuwa na mwana wala mjukuu kati ya watu wake, Wala hatasalia mtu hapo alipokaa.
Jérémie 22.30 Esaïe 14.21-14.22 Job 20.26-20.28 Job 8.4 Job 1.19
20 Hao wanaokaa magharibi watastaajabia siku yake, Kama vile wanaokaa mashariki walivyotiwa hofu.
Psaumes 37.13 Ezéchiel 21.25 Jérémie 50.27 Luc 19.44 Jérémie 18.16
21 Hakika ndivyo yalivyo makazi ya wapotovu, Na hapa ni mahali pake asiyemjua Mungu.
Jérémie 9.3 Tite 1.16 Jérémie 10.25 1 Thessaloniciens 4.5 2 Thessaloniciens 1.8

Cette Bible est dans le domaine public.