Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

1 Samuel 1.23
Bible en Swahili de l’est


Ministère de Samuel

Naissance de Samuel

1 Palikuwa na mtu mmoja wa Rama, Msufi, wa nchi ya milima milima ya Efraimu, jina lake akiitwa Elkana, mwana wa Yerohamu, mwana wa Elihu, mwana wa Tohu, mwana wa Sufu, Mwefraimu
1 Samuel 1.19 1 Chroniques 6.25-6.27 1 Chroniques 6.34 Josué 24.33 Juges 12.5
2 naye alikuwa na wake wawili; jina lake mmoja akiitwa Hana, na jina lake wa pili aliitwa Penina; naye huyo Penina alikuwa na watoto, lakini Hana hakuwa na watoto.
Juges 8.30 Genèse 25.21 Genèse 29.23-29.29 Genèse 29.31 Luc 1.7
3 Na mtu huyo alikuwa akikwea kutoka mjini kwake mwaka kwa mwaka, ili kuabudu, na kumtolea Bwana wa majeshi dhabihu katika Shilo. Na wale wana wawili wa Eli, Hofni na Finehasi, makuhani wa Bwana, walikuwako huko.
Luc 2.41 Josué 18.1 Deutéronome 12.5-12.7 Exode 23.14 Deutéronome 16.16
4 Hata siku ile ilipofika Elkana alipotoa dhabihu, kumpa mkewe Penina sehemu, akawapa na watoto wake wote, waume kwa wake, sehemu zao;
Deutéronome 12.17-12.18 Deutéronome 16.11 Lévitique 7.15 Lévitique 3.4 Deutéronome 12.5-12.7
5 lakini Hana humpa sehemu mara mbili; maana alimpenda Hana, ingawa Bwana alikuwa amemfunga tumbo.
Genèse 30.2 Genèse 16.1 Genèse 43.34 Genèse 20.18 Deutéronome 21.15
6 Ila mwenzake humchokoza sana, hata kumsikitisha, kwa sababu Bwana alikuwa amemfunga tumbo.
Job 6.14 Lévitique 18.18 Job 24.21
7 Tena mumewe akafanya hivyo mwaka kwa mwaka, hapo yule mwanamke alipokwea kwenda nyumbani kwa Bwana, ndivyo yule alivyomchokoza; basi, kwa hiyo, yeye akalia, asile chakula.
1 Samuel 2.19
8 Elkana mumewe akamwambia, Hana, unalilia nini? Kwani huli chakula? Kwa nini moyo wako una huzuni? Je! Mimi si bora kwako kuliko watoto kumi?
Ruth 4.15 Esaïe 54.1 Job 6.14 Jean 20.13 2 Rois 8.12
9 Ndipo Hana akainuka, walipokwisha kula na kunywa huko Shilo. Naye Eli, kuhani, alikuwa akiketi kitini pake penye mwimo wa hekalu la Bwana.
1 Samuel 3.3 2 Samuel 7.2 Psaumes 27.4 Psaumes 29.9 Psaumes 5.7
10 Naye huyo mwanamke alikuwa na uchungu rohoni mwake, akamwomba Bwana akalia sana.
Job 7.11 Job 10.1 Juges 21.2 2 Samuel 13.36 Ruth 1.20
11 Akaweka nadhiri, akasema, Ee Bwana wa majeshi, ikiwa wewe utaliangalia teso la mjakazi wako, na kunikumbuka, wala usinisahau mimi mjakazi wako, na kunipa mimi mjakazi wako mtoto mume, ndipo mimi nitakapompa Bwana huyo mtoto siku zote za maisha yake, wala wembe hautamfikilia kichwani kamwe.
Juges 13.5 Nombres 6.5 Genèse 29.32 Genèse 28.20 Juges 11.30
12 Ikawa, hapo alipodumu kuomba mbele za Bwana, Eli akamwangalia kinywa chake.
Luc 18.1 Luc 11.8-11.10 1 Thessaloniciens 5.17 Ephésiens 6.18 Colossiens 4.2
13 Basi Hana alikuwa akinena moyoni mwake; midomo yake tu ilionekana kama anena, sauti yake isisikiwe; kwa hiyo huyo Eli alimdhania kuwa amelewa.
Genèse 24.42-24.45 Romains 8.26 Néhémie 2.4 Actes 2.13 Zacharie 9.15
14 Ndipo Eli akamwambia, Je! Utakuwa mlevi hata lini? Achilia mbali divai yako.
Proverbes 4.24 Matthieu 7.1-7.3 Ephésiens 4.31 Ephésiens 4.25 Josué 22.12-22.20
15 Hana akajibu, akasema, Hasha! Bwana wangu, mimi ni mwanamke mwenye roho ya huzuni, mimi sikunywa divai wala kileo, ila nimeimimina roho yangu mbele za Bwana.
Psaumes 62.8 Psaumes 42.4 Lamentations 2.19 Psaumes 143.6 Psaumes 142.2-142.3
16 Usimdhanie mjakazi wako kuwa ni mwanamke asiyefaa kitu; kwa kuwa katika wingi wa kuugua kwangu na kusikitika kwangu ndivyo nilivyonena hata sasa.
1 Samuel 2.12 Deutéronome 13.13 Job 6.2-6.3 Job 10.1-10.2 Matthieu 12.34-12.35
17 Ndipo Eli akajibu, akasema, Enenda kwa amani; na Mungu wa Israeli akujalie haja yako uliyomwomba.
2 Rois 5.19 Juges 18.6 Marc 5.34 Psaumes 20.3-20.5 1 Samuel 25.35
18 Naye akasema, Mjakazi wako na aone kibali machoni pako. Basi huyo mwanamke akaenda zake, naye akala chakula, wala uso wake haukukunjamana tena.
Ruth 2.13 Ecclésiaste 9.7 Romains 15.13 Genèse 33.15 Genèse 32.5
19 Wakaondoka asubuhi na mapema, wakasali mbele za Bwana, kisha wakarejea na kufika nyumbani kwao huko Rama; Elkana akamjua mkewe Hana; naye Bwana akamkumbuka.
Genèse 30.22 1 Samuel 1.11 Genèse 4.1 Genèse 21.1 Marc 1.35
20 Ikawa, wakati ulipowadia, Hana akachukua mimba na kuzaa mtoto mwanamume; akamwita jina lake Samweli, akisema, Kwa kuwa nimemwomba kwa Bwana.
Matthieu 1.21 Exode 2.22 Genèse 41.51-41.52 Exode 2.10 Genèse 30.6-30.21
21 Kisha yule mtu, Elkana, na watu wote wa nyumbani mwake, wakakwea kwenda kumtolea Bwana dhabihu ya mwaka, na nadhiri yake.
1 Samuel 1.3 Psaumes 101.2 Genèse 18.19 Josué 24.15 Deutéronome 12.11
22 Bali Hana hakukwea; maana alimwambia mumewe, Sitakwea mimi hata mtoto wangu atakapoachishwa maziwa, hapo ndipo nitakapomleta, ili ahudhurie mbele za Bwana, akae huko daima.
1 Samuel 1.28 1 Samuel 1.11 Luc 2.22 1 Samuel 3.1 1 Samuel 2.18
23 Elkana, mumewe, akamwambia, Haya, fanya uonavyo vema; ngoja hata utakapomwachisha maziwa; Bwana na alithibitishe neno lake tu. Basi yule mwanamke akangoja, akamnyonyesha mtoto wake, hata akamwachisha maziwa.
2 Samuel 7.25 Genèse 21.7-21.8 Nombres 30.7-30.11 1 Samuel 1.17 Matthieu 24.19
24 Naye alipokuwa amekwisha kumwachisha maziwa, akamchukua pamoja naye, na ng’ombe watatu, na efa moja ya unga,na chupa ya divai,akamleta nyumbani kwa BWANA,huko Shilo ;na Yule mtoto alikuwa mtoto mdogo.
Josué 18.1 Nombres 15.9-15.10 Deutéronome 12.5-12.6 Deutéronome 12.11 1 Samuel 4.3-4.4
25 Nao wakamchinja huyo ng’ombe, wakamleta mtoto kwa Eli.
Luc 2.22 Luc 18.15-18.16
26 Akasema, Ee bwana wangu, kama iishivyo roho yako, bwana wangu, mimi ndimi yule mwanamke aliyesimama karibu nawe hapa, nikimwomba Bwana.
2 Rois 2.4 2 Rois 2.6 2 Rois 4.30 2 Rois 2.2 1 Samuel 20.3
27 Naliomba nipewe mtoto huyu; Bwana akanipa dua yangu niliyomwomba;
1 Samuel 1.11-1.13 1 Jean 5.15 Psaumes 118.5 Psaumes 116.1-116.5 Psaumes 6.9
28 kwa sababu hiyo mimi nami nimempa Bwana mtoto huyu; wakati wote atakaokuwa hai amepewa Bwana. Naye akamwabudu Bwana huko.
Genèse 24.26 Genèse 24.52 1 Samuel 1.11 Genèse 24.48 2 Timothée 3.15

Cette Bible est dans le domaine public.