Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Apocalypse 15
Bible en Swahili de l’est


Les sept fléaux

1 Kisha nikaona ishara nyingine katika mbingu, iliyo kubwa, na ya ajabu; malaika saba wenye mapigo saba ya mwisho; maana katika hayo ghadhabu ya Mungu imetimia.
Apocalypse 21.9 Apocalypse 15.6-15.7 Daniel 12.11-12.12 Apocalypse 14.19 Apocalypse 10.3
2 Tena nikaona kitu kama mfano wa bahari ya kioo iliyochangamana na moto, na wale wenye kushinda, watokao kwa yule mnyama, na sanamu yake, na kwa hesabu ya jina lake, walikuwa wamesimama kando-kando ya hiyo bahari ya kioo, wenye vinubi vya Mungu.
Apocalypse 4.6 Apocalypse 5.8 Apocalypse 19.1-19.7 Apocalypse 12.11 Apocalypse 21.18
3 Nao wauimba wimbo wa Musa, mtumwa wa Mungu, na wimbo wa Mwana-Kondoo, wakisema, Ni makuu, na ya ajabu, matendo yako, Ee Bwana Mungu Mwenyezi; Ni za haki, na za kweli, njia zako, Ee Mfalme wa mataifa.
Psaumes 111.2 Psaumes 145.17 Psaumes 139.14 Osée 14.9 Hébreux 3.5
4 Ni nani asiyekucha, Ee Bwana, na kulitukuza jina lako? Kwa kuwa wewe peke yako u Mtakatifu; kwa maana mataifa yote watakuja na kusujudu mbele zako; kwa kuwa matendo yako ya haki yamekwisha kufunuliwa.
Psaumes 86.9 Jérémie 10.7 Zacharie 2.11 Romains 15.9 1 Pierre 1.16
5 Na baada ya hayo nikaona, na hekalu la hema ya ushuhuda mbinguni lilifunguliwa;
Apocalypse 11.19 Nombres 1.50 Nombres 1.53 Exode 38.21 Matthieu 27.51
6 na wale malaika saba, wenye mapigo saba, wakatoka katika hekalu, wamevikwa mavazi ya kitani safi, ya kung’aa, wamefungwa vifuani mwao mishipi ya dhahabu.
Apocalypse 1.13 Apocalypse 15.1 Apocalypse 14.15 Exode 28.5-28.8 Luc 24.4
7 Na mmoja wa wale wenye uhai wanne akawapa wale malaika saba vitasa saba vya dhahabu, vimejaa ghadhabu ya Mungu, aliye hai hata milele na milele.
Apocalypse 5.8 Apocalypse 10.6 Apocalypse 16.2-17.1 1 Thessaloniciens 1.9 Apocalypse 15.1
8 Hekalu likajazwa moshi uliotoka kwenye utukufu wa Mungu na uweza wake. Wala hapakuwa na mtu aliyeweza kuingia ndani ya hekalu, hata yatimizwe mapigo saba ya wale malaika saba.
Esaïe 6.4 1 Rois 8.10-8.11 2 Chroniques 5.13-5.14 Exode 40.34-40.35 Romains 11.33

Cette Bible est dans le domaine public.