Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Josué 23.9
Bible en Swahili de l’est


Encouragements de Josué aux chefs d’Israël

1 Hata ikawa baada ya siku nyingi, Bwana alipokuwa amekwisha kuwapa Israeli raha mbele ya adui zao pande zote, naye Yoshua alipokuwa mzee, mwenye miaka mingi sana,
Josué 13.1 Josué 21.44 Josué 11.23 Deutéronome 31.2 Genèse 25.8
2 Yoshua akawaita Israeli wote, wazee wao, na wakuu wao, na makadhi yao, na maakida yao, akawaambia, Mimi ni mzee, nami nimekwendelea sana katika miaka yangu;
Josué 24.1 1 Chroniques 28.1 Deutéronome 31.28 Actes 20.17-20.35
3 nanyi mmeona mambo yote ambayo Bwana, Mungu wenu, amewatenda mataifa haya yote kwa ajili yenu; kwa maana Bwana, Mungu wenu, ndiye aliyewapigania ninyi.
Exode 14.14 Josué 10.14 Josué 10.42 Deutéronome 4.9 Deutéronome 20.4
4 Tazama, nimewagawieni kwa kura mataifa haya yaliyobaki, yawe urithi kwa kabila zenu, toka mto wa Yordani, pamoja na mataifa yote niliyowakatilia mbali, mpaka bahari kubwa upande wa machweo ya jua.
Josué 13.6-13.7 Josué 13.2 Josué 18.10
5 Yeye Bwana, Mungu wenu, atawatoa kwa nguvu mbele yenu, atawafukuza wasiwe mbele ya macho yenu tena; nanyi mtaimiliki nchi yao, kama Bwana Mungu wenu, alivyowaambia.
Josué 13.6 Exode 34.11 Deutéronome 11.23 Exode 33.2 Nombres 33.52-33.53
6 Basi, iweni mashujaa sana kuyashika yote yaliyoandikwa katika kitabu cha torati ya Musa, na kuyatenda, msiyaache kwa kugeukia upande wa kuume wala upande wa kushoto.
Deutéronome 5.32 Deutéronome 28.14 Ephésiens 6.10-6.19 1 Corinthiens 16.13 Josué 1.7-1.9
7 Msiingie kati ya mataifa haya, yaani, haya yaliyobaki kati yenu; wala msitaje majina ya miungu yao, wala kuwaapisha watu kwa majina hayo, wala kuitumikia, wala kujiinamisha mbele yao;
Psaumes 16.4 Exode 23.13 Jérémie 5.7 Sophonie 1.5 Deutéronome 7.2-7.3
8 bali shikamaneni na Bwana, Mungu wenu, kama mlivyotenda hata hivi leo.
Deutéronome 10.20 Deutéronome 13.4 Josué 22.5 Deutéronome 11.22 Actes 11.23
9 Maana Bwana amefukuza mbele yenu mataifa walio hodari, kisha wenye nguvu, lakini kwenu ninyi hapana mtu aliyesimama mbele yenu hata leo.
Deutéronome 11.23 Josué 1.5 Josué 23.5 Exode 23.30 Josué 1.8-1.9
10 Mtu mmoja miongoni mwenu atafukuza watu elfu; maana Bwana, Mungu wenu, ndiye anayewapigania, kama alivyowaambia.
Lévitique 26.8 Deutéronome 32.30 Deutéronome 3.22 Psaumes 35.1 Exode 14.14
11 Jihadharini nafsi zenu, basi, ili mmpende Bwana, Mungu wenu.
Josué 22.5 Deutéronome 4.9 Romains 8.28 Hébreux 12.15 Proverbes 4.23
12 Lakini mkirudi nyuma kwa njia yo yote na kushikamana na mabaki ya mataifa, yaani, mataifa haya yaliyobaki kati yenu, na kuoana nao, na kuingia kwao, nao kuingia kwenu;
Deutéronome 7.3 Exode 34.12-34.16 2 Corinthiens 6.14-6.17 Romains 12.9 1 Samuel 18.1-18.3
13 jueni hakika ya kuwa Bwana, Mungu wenu, hatawafukuza tena mataifa haya mbele ya macho yenu, bali watakuwa mtego kwenu na tanzi, na mjeledi mbavuni mwenu, na miiba machoni mwenu, hata mtakapoangamia na kutoka katika nchi hii njema, ambayo Bwana, Mungu wenu, amewapa ninyi.
Deutéronome 7.16 Exode 23.33 Nombres 33.55 2 Rois 17.22-17.23 Deutéronome 29.28
14 Angalieni, mimi leo ninakwenda njia ile waendayo watu wote wa ulimwengu; nanyi nyote mnajua mioyoni mwenu, na rohoni mwenu, ya kuwa halikuwapungukia ninyi hata neno moja katika mambo hayo mema yote aliyoyanena Bwana, Mungu wenu, katika habari zenu; yote yametimia kwenu hapana neno lo lote mlilopungukiwa.
1 Rois 2.2 Lévitique 26.3-26.13 Ecclésiaste 12.5 Job 30.23 1 Rois 8.56
15 Kisha itakuwa, kama yalivyowafikilia yale mambo mema yote, Bwana, Mungu wenu, aliyowaahidia ninyi, kadhalika Bwana atawafikilizia mabaya yote, hata atakapokuwa amewaangamiza katika nchi hii njema, Bwana Mungu wenu, aliyowapa.
Deutéronome 28.15-28.68 Juges 4.1-4.2 Juges 6.1 Juges 10.6-10.7 Lévitique 26.14-26.46
16 Hapo mtakapolivunja agano la Bwana, Mungu wenu, alilowaamuru, na kwenda kuitumikia miungu mingine, na kujiinamisha mbele yao, ndipo hasira ya Bwana itakapowaka juu yenu, nanyi mtaangamia upesi katika nchi hii njema aliyowapa.
2 Rois 24.20 Deutéronome 4.25-4.26

Cette Bible est dans le domaine public.