Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Malachie 4.4
Bible en Swahili de l’est


1 Kwa maana, angalieni, siku ile inakuja, inawaka kama tanuru; na watu wote wenye kiburi, nao wote watendao uovu, watakuwa makapi; na siku ile inayokuja itawateketeza, asema Bwana wa majeshi; hata haitawaachia shina wala tawi.
Malachie 3.2 2 Thessaloniciens 1.8 Esaïe 47.14 Esaïe 5.24 2 Pierre 3.7
2 Lakini kwenu ninyi mnaolicha jina langu, jua la haki litawazukia, lenye kuponya katika mbawa zake; nanyi mtatoka nje, na kucheza-cheza kama ndama wa mazizini.
Esaïe 30.26 Jean 8.12 Luc 1.78 2 Samuel 23.4 Jean 1.4
3 Nanyi mtawakanyaga waovu; maana watakuwa majivu chini ya nyayo za miguu yenu; katika siku ile niifanyayo, asema Bwana wa majeshi.
Job 40.12 Michée 5.8 Esaïe 26.6 Esaïe 63.3-63.6 Romains 16.20
4 Ikumbukeni torati ya Musa, mtumishi wangu, niliyomwamuru huko Horebu kwa ajili ya Israeli wote, naam, amri na hukumu.
Deutéronome 4.10 Luc 16.29-16.31 Exode 21.1-21.23 Matthieu 5.17-5.20 Deutéronome 4.5-4.6
5 Angalieni, nitawapelekea Eliya nabii, kabla haijaja siku ile ya Bwana, iliyo kuu na kuogofya.
Luc 1.17 Matthieu 17.10-17.13 Malachie 3.1 Apocalypse 6.17 Joël 2.31
6 Naye ataigeuza mioyo ya baba iwaelekee watoto wao, na mioyo ya watoto iwaelekee baba zao, ili nisije nikaipiga dunia kwa laana.
Luc 1.16-1.17 Esaïe 11.4 Esaïe 65.15 Hébreux 10.26-10.31 Zacharie 5.3

Cette Bible est dans le domaine public.