Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Malachie 2.7
Bible en Swahili de l’est


1 Na sasa, enyi makuhani, amri hii yawahusu ninyi.
Malachie 1.6 Jérémie 13.13 Osée 5.1 Lamentations 4.13
2 Kama hamtaki kusikia, na kama hamtaki kuitia moyoni, ili kulitukuza jina langu, asema Bwana wa majeshi, basi nitawapelekeeni laana, nami nitazilaani baraka zenu; naam, nimekwisha kuzilaani, kwa sababu hamyatii haya moyoni.
Apocalypse 14.7 Malachie 3.9 Luc 17.18 Psaumes 69.22 1 Pierre 4.11
3 Angalieni, nitaikemea mbegu kwa ajili yenu, nami nitapaka nyuso zenu mavi, naam, mavi ya sadaka zenu; nanyi mtaondolewa pamoja nayo
Nahum 3.6 1 Rois 14.10 Exode 29.14 Joël 1.17 Luc 14.35
4 Nanyi mtajua ya kuwa mimi nimewapelekeeni amri hii, ili agano langu liwe na Lawi, asema Bwana wa majeshi.
Nombres 3.12 Ezéchiel 38.23 Ezéchiel 20.38-20.41 1 Rois 22.25 Luc 10.11
5 Agano langu naye lilikuwa agano la uhai na amani; nami nikampa ili aogope, naye akaniogopa, akalicha jina langu.
Nombres 25.12-25.13 Psaumes 106.30-106.31 Exode 32.26-32.29 Nombres 8.15 Ezéchiel 34.25
6 Sheria ya kweli ilikuwa kinywani mwake, wala udhalimu haukuonekana midomoni mwake; alikwenda pamoja nami katika amani na unyofu, na kuwageuza wengi hata wakaacha uovu.
Jérémie 23.22 Jacques 5.19-5.20 Daniel 12.3 Osée 4.6 Apocalypse 14.5
7 Kwa maana yapasa midomo ya kuhani ihifadhi maarifa, tena yawapasa watu kuitafuta sheria kinywani mwake; kwa kuwa yeye ni mjumbe wa Bwana wa majeshi.
Lévitique 10.11 Jérémie 18.18 Deutéronome 17.8-17.11 Jean 13.20 Aggée 1.13
8 Bali ninyi mmegeuka mkaiacha njia; mmewakwaza watu wengi katika sheria; mmeliharibu agano la Lawi, asema Bwana wa majeshi.
Jérémie 18.15 Malachie 2.5 Ezéchiel 44.10 1 Samuel 2.17 Néhémie 13.29
9 Kwa sababu hiyo mimi nami nimewafanya ninyi kuwa kitu cha kudharauliwa, na unyonge, mbele ya watu wote, kama vile ninyi msivyozishika njia zangu, bali mmewapendelea watu katika sheria.
Deutéronome 1.17 1 Samuel 2.30 Matthieu 19.17-19.18 Ezéchiel 13.21 Jérémie 28.15-28.16

Mariages mixtes et divorces

10 Je! Sisi sote hatuna Baba mmoja? Mungu aliyetuumba siye mmoja tu? Basi, mbona kila mmoja wetu anamtenda ndugu yake mambo ya hiana, tukilinajisi agano la baba zetu?
1 Corinthiens 8.6 Malachie 2.11 Esaïe 64.8 Esaïe 63.16 Ephésiens 4.6
11 Yuda ametenda kwa hiana, na chukizo limetendeka katika Israeli, na katika Yerusalemu; maana Yuda ameunajisi utakatifu wa Bwana aupendao, naye amemwoa binti ya mungu mgeni.
Esdras 9.1-9.2 Ezéchiel 18.13 Esdras 10.2 Jérémie 2.3 Deutéronome 7.3-7.6
12 Bwana atamtenga mtu atendaye hayo, yeye aliye macho, na yeye ajibuye, atamtenga na hema za Yakobo, pia atamtenga yeye amtoleaye Bwana wa majeshi dhabihu.
Malachie 1.10 Lévitique 18.29 Esaïe 9.14-9.16 Ezéchiel 24.21 Esaïe 66.3
13 Tena mnatenda haya nayo; mnaifunikiza madhabahu ya Bwana kwa machozi, kwa kulia na kwa kuugua, hata asiiangalie tena hiyo dhabihu, wala kuitakabali mikononi mwenu na kuiridhia.
Jérémie 14.12 Deutéronome 26.14 Proverbes 21.27 1 Samuel 1.9-1.10 Jérémie 6.20
14 Lakini ninyi mwasema, Ni kwa sababu gani? Ni kwa sababu Bwana amekuwa shahidi kati ya wewe na mke wa ujana wako, uliyemtenda mambo ya hiana, angawa yeye ni mwenzako, na mke wa agano lako.
Esaïe 54.6 Malachie 3.5 1 Samuel 12.5 Genèse 2.18 Genèse 31.50
15 Hakuna mtu mmoja aliyetenda hivi, ambaye alikuwa na ufahamu kidogo. Au je! Kuna mtu mmoja atafutaye mzao mwenye kumcha Mungu? Kwa hiyo jihadharini roho zenu; mtu awaye yote asimtende mke wa ujana wake mambo ya hiana.
Matthieu 19.4-19.6 1 Corinthiens 7.2 Genèse 1.27 1 Corinthiens 7.14 Genèse 6.2
16 Maana mimi nakuchukia kuachana, asema Bwana, Mungu wa Israeli; naye aifunikizaye nguo yake kwa udhalimu namchukia, asema Bwana wa majeshi; basi jihadharini roho zenu, msije mkatenda kwa hiana.
Luc 16.18 Matthieu 5.31-5.32 Deutéronome 24.1-24.4 Matthieu 19.3-19.9 Esaïe 50.1

Justice de Dieu et purification

17 Mmemchokesha Bwana kwa maneno yenu. Lakini ninyi mwasema, Tumemchokesha kwa maneno gani? Kwa kuwa mwasema, Kila atendaye mabaya ni mwema machoni pa Bwana, naye huwafurahia watu hao, au, Mungu mwenye kuhukumu yuko wapi?
Esaïe 43.24 Sophonie 1.12 Psaumes 73.3-73.15 Ecclésiaste 8.11 Malachie 2.14

Cette Bible est dans le domaine public.