Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Zacharie 4.10
Bible en Swahili de l’est


Vision d’un chandelier d’or et de deux oliviers

1 Na yule malaika aliyesema nami akanijia mara ya pili, akaniamsha, kama mtu aamshwavyo katika usingizi wake.
Jérémie 31.26 Daniel 8.18 Zacharie 1.9 1 Rois 19.5-19.7 Zacharie 1.19
2 Akaniuliza, Unaona nini? Nikasema, Nimeona, na tazama, kinara cha taa cha dhahabu tupu, nacho kina bakuli juu yake, na taa zake saba juu yake; tena iko mirija saba ya kuleta mafuta, kwa taa zote zilizo juu yake;
Apocalypse 4.5 Apocalypse 1.12 Zacharie 5.2 Jérémie 52.19 Exode 37.17-37.24
3 na mizeituni miwili karibu yake, mmoja upande wa kuume walile bakuli, na mmoja upande wake wa kushoto.
Apocalypse 11.4 Zacharie 4.14 Romains 11.24 Zacharie 4.11-4.12 Romains 11.17
4 Nami nikajibu, nikamwambia yule malaika aliyesema nami, nikasema, Ee Bwana wangu, vitu hivi ni nini?
Zacharie 1.9 Zacharie 6.4 Apocalypse 7.13-7.14 Matthieu 13.36 Zacharie 1.19
5 Ndipo malaika aliyesema nami akajibu, akaniambia, Hujui vitu hivi ni nini? Nikasema, La, Bwana wangu.
Zacharie 4.13 Marc 4.13 Genèse 41.16 Psaumes 139.6 1 Corinthiens 2.12-2.15
6 Akajibu akaniambia, akisema, Hili ndilo neno la Bwana kwa Zerubabeli, kusema, Si kwa uwezo, wala si kwa nguvu, bali ni kwa roho yangu, asema Bwana wa majeshi.
2 Chroniques 32.7-32.8 Esaïe 11.2-11.4 Osée 1.7 Psaumes 33.16 2 Corinthiens 10.4-10.5
7 Nani wewe, Ee mlima mkubwa? Mbele ya Zerubabeli utakuwa nchi tambarare; naye atalileta lile jiwe la kuwekwa juu kabisa pamoja na vigelegele vya, Neema, neema, ilikalie.
Jérémie 51.25 Psaumes 114.6 Psaumes 114.4 Michée 4.1 Zacharie 14.4-14.5
8 Tena neno la Bwana likanijia, kusema,
9 Mikono yake Zerubabeli imeiweka misingi ya nyumba hii, na mikono yake ndiyo itakayoimaliza; nawe utajua ya kuwa Bwana wa majeshi amenituma kwenu.
Esdras 6.14-6.15 Esdras 5.16 Zacharie 6.12-6.13 Esaïe 48.16 Zacharie 2.11
10 Maana ni nani aliyeidharau siku ya mambo madogo? Kwa kuwa watafurahi, nao wataiona timazi katika mkono wa Zerubabeli; naam, hizi saba ndizo macho ya Bwana; yapiga mbio huko na huko duniani mwote.
Zacharie 3.9 2 Chroniques 16.9 Apocalypse 5.6 1 Corinthiens 1.28-1.29 Aggée 2.3
11 Ndipo nikajibu, nikamwambia, Ni nini mizeituni hii miwili iliyo upande wa kuume wa kinara cha taa kile na upande wake wa kushoto?
Zacharie 4.3 Apocalypse 11.4
12 Nami nikajibu mara ya pili, nikamwuliza, Ni nini haya matawi mawili ya mizeituni, ambayo kwa njia ya ile mifereji miwili ya dhahabu hutoa mafuta yao?
Apocalypse 11.4 Matthieu 20.23 Aggée 1.1
13 Akanijibu, akasema, Hujui hivi ni nini? Nikasema, La, Bwana wangu.
Zacharie 4.5 Hébreux 5.11-5.12
14 Ndipo akasema, Hivi ni hao wana wawili wa mafuta, wasimamao karibu na Bwana wa dunia yote.
Apocalypse 11.4 Daniel 9.24-9.26 Michée 4.13 Zacharie 3.1-3.7 Exode 40.15

Cette Bible est dans le domaine public.