Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Zacharie 3.8
Bible en Swahili de l’est


Vision du grand-prêtre

1 Kisha akanionyesha Yoshua, kuhani mkuu, amesimama mbele ya malaika wa Bwana, na Shetani amesimama mkono wake wa kuume ili kushindana naye.
Psaumes 109.6 Zacharie 6.11 Aggée 1.1 Esdras 5.2 Deutéronome 18.15
2 Bwana akamwambia Shetani, Bwana na akukemee Ewe Shetani; naam, Bwana, aliyechagua Yerusalemu, na akukemee; je! Hiki si kinga kilichotolewa motoni?
Jude 1.9 Amos 4.11 Jude 1.23 Romains 8.33 Zacharie 2.12
3 Basi, Yoshua alikuwa amevaa nguo chafu sana, naye alikuwa akisimama mbele ya malaika.
Esaïe 64.6 Esdras 9.15 Matthieu 22.11-22.13 2 Chroniques 30.18-30.20 Daniel 9.18
4 Naye huyo akajibu, akawaambia wale waliosimama mbele yake, akisema, Mvueni nguo hizi zenye uchafu. Kisha akamwambia yeye, Tazama, nimekuondolea uovu wako, nami nitakuvika mavazi ya thamani nyingi.
Ezéchiel 36.25 Esaïe 43.25 Luc 1.19 Esaïe 61.10 Luc 15.22
5 Nikasema, Na wampige kilemba kizuri kichwani pake. Basi, wakampiga kilemba kizuri kichwani pake, wakamvika mavazi; naye malaika wa Bwana akasimama karibu.
Exode 29.6 Zacharie 6.11 Apocalypse 4.4 Apocalypse 4.10 Exode 28.2-28.4
6 Kisha malaika wa Bwana akamshuhudia Yoshua, akisema,
Genèse 28.13-28.17 Exode 23.20-23.21 Zacharie 3.1 Osée 12.4 Genèse 48.15-48.16
7 Bwana wa majeshi asema hivi, Kama ukienda katika njia zangu, na kama ukishika maagizo yangu, ndipo utakapoihukumu nyumba yangu, nawe utazilinda nyua zangu, nami nitakupa nafasi ya kunikaribia kati yao wasimamao karibu.
Genèse 26.5 Lévitique 8.35 Hébreux 12.22-12.23 Ezéchiel 44.15-44.16 Ezéchiel 44.8
8 Sikiliza sasa, Ee Yoshua, kuhani mkuu, wewe na wenzako waketio mbele yako; maana hao ni watu walio ishara; kwa maana, tazama, ninamleta mtumishi wangu, aitwaye Chipukizi.
Jérémie 23.5 Esaïe 11.1 Zacharie 6.12 Esaïe 53.2 Esaïe 4.2
9 Maana, litazame jiwe hili nililoliweka mbele ya Yoshua; katika jiwe moja yako macho saba; tazama, nitachora machoro yake, asema Bwana wa majeshi, nami nitauondoa uovu wa nchi ile katika siku moja.
Esaïe 28.16 Jérémie 50.20 Zacharie 4.10 Psaumes 118.22 1 Timothée 2.5-2.6
10 Katika siku ile, asema Bwana wa majeshi, ninyi mtamwalika kila mtu jirani yake chini ya mzabibu, na chini ya mtini.
1 Rois 4.25 Michée 4.4 Esaïe 36.16 Jean 1.45-1.48 Osée 2.18

Cette Bible est dans le domaine public.