Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Zacharie 12.13
Bible en Swahili de l’est


Délivrance et purification de Jérusalem

1 Ufunuo wa neno la Bwana juu ya Israeli. Haya ndiyo asemayo Bwana, azitandaye mbingu, auwekaye msingi wa dunia, aiumbaye roho ya mwanadamu ndani yake.
Esaïe 42.5 Esaïe 57.16 Jérémie 51.15 Job 26.7 Esaïe 44.24
2 Angalia, mimi nitafanya Yerusalemu kuwa kikombe cha kuyumba-yumba kwa watu wa kabila zote, wazungukao pande zote; tena kitakuwa juu ya Yuda pia wakati wa kuhusuriwa Yerusalemu.
Zacharie 14.14 Esaïe 51.22-51.23 Psaumes 75.8 Esaïe 51.17 Apocalypse 14.10
3 Tena itakuwa siku hiyo, nitafanya Yerusalemu kuwa jiwe la kuwalemea watu wa kabila zote; wote watakaojitwika jiwe hilo watapata jeraha nyingi; na mataifa yote ya dunia watakusanyika pamoja juu yake.
Matthieu 21.44 Zacharie 14.2-14.4 Daniel 2.34-2.35 Zacharie 13.1 Luc 20.18
4 Katika siku hiyo, asema Bwana, nitamtia kila farasi ushangao, na yeye ampandaye nitamtia wazimu; nami nitaifunulia nyumba ya Yuda macho yangu, nami nitamtia upofu kila farasi wa hizo kabila za watu.
Deutéronome 28.28 Zacharie 12.3 Zacharie 9.8 2 Chroniques 7.15 Jérémie 24.6
5 Na wakuu wa Yuda watasema mioyoni mwao, Wenyeji wa Yerusalemu ni nguvu zangu katika Bwana wa majeshi, Mungu wao.
Psaumes 18.32 Esaïe 28.6 Zacharie 10.12 Jérémie 30.21 Psaumes 20.6-20.7
6 Siku hiyo nitawafanya wakuu wa Yuda kuwa kama kigae chenye moto katika kuni, na kama kinga cha moto katika miganda; nao watateketeza watu wa kila kabila, wawazungukao pande zote, upande wa mkono wa kuume na upande wa mkono wa kushoto; na baada ya haya Yerusalemu utakaa mahali pake, naam, hapo Yerusalemu.
Abdias 1.18 Zacharie 2.4 Néhémie 11.1-11.36 Zacharie 8.3-8.5 Esaïe 9.20
7 Naye Bwana ataziokoa hema za Yuda kwanza, ili utukufu wa nyumba ya Daudi, na utukufu wa wenyeji wa Yerusalemu, usipate kutukuzwa kuliko Yuda.
Job 19.5 Psaumes 55.12 Luc 1.51-1.53 Psaumes 35.26 1 Corinthiens 1.26-1.31
8 Katika siku hiyo Bwana atawalinda wenyeji wa Yerusalemu; na yeye aliye dhaifu miongoni mwao atakuwa kama Daudi siku hiyo; nayo nyumba ya Daudi itakuwa kama Mungu, kama malaika wa Bwana mbele yao.
Michée 7.8 Esaïe 30.26 Jérémie 33.15-33.16 Malachie 3.1 Ezéchiel 34.23-34.24
9 Hata itakuwa siku hiyo, ya kwamba nitatafuta kuwaangamiza mataifa yote watakaokuja kupigana na Yerusalemu.
Esaïe 54.17 Zacharie 14.2-14.3 Aggée 2.22 Zacharie 12.2
10 Nami nitawamwagia watu wa nyumba ya Daudi, na wenyeji wa Yerusalemu, roho ya neema na kuomba; nao watamtazama yeye ambaye walimchoma; nao watamwombolezea, kama vile mtu amwombolezeavyo mwanawe wa pekee; nao wataona uchungu kwa ajili yake, kama vile mtu aonavyo uchungu kwa ajili ya mzaliwa wake wa kwanza.
Apocalypse 1.7 Joël 2.28-2.29 Ezéchiel 39.29 Jérémie 6.26 Ephésiens 6.18
11 Siku hiyo kutakuwa na maombolezo makuu huko Yerusalemu, kama maombolezo ya Hadadrimoni katika bonde la Megido.
2 Chroniques 35.24 2 Rois 23.29
12 Nayo nchi itaomboleza, kila jamaa peke yake; jamaa ya nyumba ya Daudi peke yao, na wake zao peke yao; jamaa ya nyumba ya Nathani peke yao, na wake zao peke yao;
Luc 3.31 Zacharie 7.3 2 Samuel 5.14 Apocalypse 1.7 Matthieu 24.30
13 jamaa ya nyumba ya Lawi peke yao, na wake zao peke yao; jamaa ya nyumba ya Shimei peke yao, na wake zao peke yao.
1 Chroniques 23.7 2 Chroniques 29.14 1 Rois 1.8 1 Chroniques 4.27 2 Samuel 16.5
14 Jamaa zote zilizosalia, kila jamaa peke yake, na wake zao peke yao.
Proverbes 9.12

Cette Bible est dans le domaine public.