Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Zacharie 10
Bible en Swahili de l’est


Les bergers et le troupeau

1 Mwombeni Bwana mvua wakati wa masika, naam, Bwana afanyaye umeme, naye atawapa manyunyu ya mvua, kila mtu atapewa nyasi kondeni.
Esaïe 30.23 Jérémie 10.13 Ezéchiel 34.26 Esaïe 44.3 Jérémie 14.22
2 Kwa maana vinyago vimenena maneno ya ubatili, nao waaguzi wameona uongo; nao wameleta habari za ndoto za uongo, wafariji bure; kwa sababu hiyo waenda zao kama kondoo, wateswa, kwa sababu hapana mchungaji.
Ezéchiel 34.5 Matthieu 9.36 Osée 3.4 Genèse 31.19 Habakuk 2.18
3 Hasira yangu imewaka juu ya wachungaji, nami nitawaadhibu mbuzi waume; kwa maana Bwana wa majeshi ameliangalia kundi lake, yaani, nyumba ya Yuda, naye atawafanya kuwa kama farasi wake mzuri vitani.
Sophonie 2.7 Ezéchiel 34.16-34.17 Ezéchiel 34.2 Ruth 1.6 Jérémie 25.12
4 Kwake yeye litatoka lile jiwe la pembeni, kwake yeye utatoka msumari, kwake yeye utatoka upinde wa vita, kwake yeye atatoka kila mtawala pamoja.
Zacharie 9.10 Zacharie 9.8 Nombres 24.17 2 Timothée 2.4 Zacharie 1.20-1.21
5 Nao watakuwa kama mashujaa, wakanyagao adui zao katika matope ya njia vitani; nao watapiga vita, kwa sababu Bwana yu pamoja nao; na hao wapandao farasi watafadhaishwa.
Aggée 2.22 Psaumes 20.7 Josué 10.42 2 Corinthiens 10.4 Romains 8.31-8.37
6 Nami nitaitia nguvu nyumba ya Yuda, nami nitaiokoa nyumba ya Yusufu, nami nitawarudisha, kwa maana nawaonea rehema; nao watakuwa kana kwamba sikuwatupa; kwa maana mimi ni Bwana, Mungu wao, nami nitawasikia.
Zacharie 13.9 Zacharie 10.12 Esaïe 14.1 Jérémie 3.18 Sophonie 3.19-3.20
7 Na watu wa Efraimu watakuwa kama shujaa, na moyo wao utafurahi kana kwamba ni kwa divai; naam, watoto wao wataona mambo haya, na kufurahi; mioyo yao itamfurahia Bwana.
Zacharie 9.15 Zacharie 9.17 1 Samuel 2.1 Proverbes 31.6-31.7 Psaumes 90.16
8 Nitawapigia kelele, na kuwakusanya pamoja; kwa maana nimewakomboa; nao wataongezeka kama walivyoongezeka.
Esaïe 5.26 Esaïe 7.18 Jérémie 33.22 Ezéchiel 36.10-36.11 Jérémie 31.10-31.11
9 Nami nitawapanda kama mbegu kati ya mataifa; nao watanikumbuka katika nchi zilizo mbali; nao watakaa pamoja na watoto wao; tena watarudi.
Ezéchiel 6.9 1 Rois 8.47-8.48 Osée 2.23 Deutéronome 30.1-30.4 Romains 11.24
10 Tena nitawarudisha toka nchi ya Misri, nitawakusanya na kuwatoa katika Ashuru; nami nitawaingiza katika nchi ya Gileadi na Lebanoni; ila nafasi ya kuwatosha haitaonekana.
Osée 11.11 Michée 7.14 Zacharie 8.7 Esaïe 11.11-11.16 Esaïe 27.12-27.13
11 Naye atapita kati ya bahari ya mateso, na kuyapiga mawimbi ya bahari, na vilindi vyote vya mto wa Nile vitakauka; na kiburi cha Ashuru kitashushwa; na fimbo ya enzi ya Misri itatoweka.
Ezéchiel 30.13 Exode 14.21-14.22 Michée 5.5-5.6 Esaïe 14.25 Psaumes 114.3
12 Nami nitawatia nguvu katika Bwana; nao watatembea huko na huko katika jina lake, asema Bwana.
Michée 4.5 Zacharie 10.6 Genèse 24.40 Esaïe 45.24 Genèse 5.24

Cette Bible est dans le domaine public.