Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Zacharie 10
Bible en Swahili de l’est


Les bergers et le troupeau

1 Mwombeni Bwana mvua wakati wa masika, naam, Bwana afanyaye umeme, naye atawapa manyunyu ya mvua, kila mtu atapewa nyasi kondeni.
Jacques 5.7 Esaïe 30.23 Jérémie 10.13 Ezéchiel 34.26 Esaïe 44.3
2 Kwa maana vinyago vimenena maneno ya ubatili, nao waaguzi wameona uongo; nao wameleta habari za ndoto za uongo, wafariji bure; kwa sababu hiyo waenda zao kama kondoo, wateswa, kwa sababu hapana mchungaji.
Ezéchiel 34.5 Matthieu 9.36 Osée 3.4 Genèse 31.19 Habakuk 2.18
3 Hasira yangu imewaka juu ya wachungaji, nami nitawaadhibu mbuzi waume; kwa maana Bwana wa majeshi ameliangalia kundi lake, yaani, nyumba ya Yuda, naye atawafanya kuwa kama farasi wake mzuri vitani.
Sophonie 2.7 Ezéchiel 34.16-34.17 Cantique 1.9 Jérémie 50.6 Ezéchiel 34.2
4 Kwake yeye litatoka lile jiwe la pembeni, kwake yeye utatoka msumari, kwake yeye utatoka upinde wa vita, kwake yeye atatoka kila mtawala pamoja.
Zacharie 9.10 Zacharie 9.8 Nombres 24.17 1 Samuel 14.38 Zacharie 9.13-9.16
5 Nao watakuwa kama mashujaa, wakanyagao adui zao katika matope ya njia vitani; nao watapiga vita, kwa sababu Bwana yu pamoja nao; na hao wapandao farasi watafadhaishwa.
Aggée 2.22 Psaumes 20.7 Matthieu 4.3 2 Timothée 4.7 Josué 10.42
6 Nami nitaitia nguvu nyumba ya Yuda, nami nitaiokoa nyumba ya Yusufu, nami nitawarudisha, kwa maana nawaonea rehema; nao watakuwa kana kwamba sikuwatupa; kwa maana mimi ni Bwana, Mungu wao, nami nitawasikia.
Zacharie 13.9 Zacharie 10.12 Esaïe 14.1 Jérémie 3.18 Esaïe 49.17-49.21
7 Na watu wa Efraimu watakuwa kama shujaa, na moyo wao utafurahi kana kwamba ni kwa divai; naam, watoto wao wataona mambo haya, na kufurahi; mioyo yao itamfurahia Bwana.
Zacharie 9.15 Actes 13.33 Esaïe 66.14 Zacharie 9.17 1 Samuel 2.1
8 Nitawapigia kelele, na kuwakusanya pamoja; kwa maana nimewakomboa; nao wataongezeka kama walivyoongezeka.
Esaïe 5.26 Esaïe 7.18 Jérémie 33.22 Ezéchiel 36.10-36.11 Jérémie 31.10-31.11
9 Nami nitawapanda kama mbegu kati ya mataifa; nao watanikumbuka katika nchi zilizo mbali; nao watakaa pamoja na watoto wao; tena watarudi.
Ezéchiel 6.9 1 Rois 8.47-8.48 Osée 2.23 Actes 2.38-2.39 Actes 13.1-13.38
10 Tena nitawarudisha toka nchi ya Misri, nitawakusanya na kuwatoa katika Ashuru; nami nitawaingiza katika nchi ya Gileadi na Lebanoni; ila nafasi ya kuwatosha haitaonekana.
Osée 11.11 Michée 7.14 Zacharie 8.7 Esaïe 11.11-11.16 Esaïe 27.12-27.13
11 Naye atapita kati ya bahari ya mateso, na kuyapiga mawimbi ya bahari, na vilindi vyote vya mto wa Nile vitakauka; na kiburi cha Ashuru kitashushwa; na fimbo ya enzi ya Misri itatoweka.
Ezéchiel 30.13 2 Rois 2.8 Exode 14.27-14.28 Exode 14.21-14.22 Michée 5.5-5.6
12 Nami nitawatia nguvu katika Bwana; nao watatembea huko na huko katika jina lake, asema Bwana.
Michée 4.5 Zacharie 10.6 Colossiens 3.17 Genèse 24.40 Esaïe 45.24

Cette Bible est dans le domaine public.