Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Zacharie 10.10
Bible en Swahili de l’est


Les bergers et le troupeau

1 Mwombeni Bwana mvua wakati wa masika, naam, Bwana afanyaye umeme, naye atawapa manyunyu ya mvua, kila mtu atapewa nyasi kondeni.
Jérémie 10.13 Ezéchiel 34.26 Esaïe 44.3 Jérémie 14.22 Jacques 5.7
2 Kwa maana vinyago vimenena maneno ya ubatili, nao waaguzi wameona uongo; nao wameleta habari za ndoto za uongo, wafariji bure; kwa sababu hiyo waenda zao kama kondoo, wateswa, kwa sababu hapana mchungaji.
Ezéchiel 34.5 Osée 3.4 Matthieu 9.36 Jérémie 27.9 Genèse 31.19
3 Hasira yangu imewaka juu ya wachungaji, nami nitawaadhibu mbuzi waume; kwa maana Bwana wa majeshi ameliangalia kundi lake, yaani, nyumba ya Yuda, naye atawafanya kuwa kama farasi wake mzuri vitani.
Ezéchiel 34.16-34.17 Sophonie 2.7 Esaïe 56.9-56.12 Esaïe 24.21 Luc 1.68
4 Kwake yeye litatoka lile jiwe la pembeni, kwake yeye utatoka msumari, kwake yeye utatoka upinde wa vita, kwake yeye atatoka kila mtawala pamoja.
Zacharie 9.10 Nombres 24.17 Zacharie 9.8 Psaumes 118.22 Ephésiens 6.10-6.17
5 Nao watakuwa kama mashujaa, wakanyagao adui zao katika matope ya njia vitani; nao watapiga vita, kwa sababu Bwana yu pamoja nao; na hao wapandao farasi watafadhaishwa.
Aggée 2.22 Psaumes 20.7 Joël 3.12-3.17 Esaïe 41.12 Zacharie 12.8
6 Nami nitaitia nguvu nyumba ya Yuda, nami nitaiokoa nyumba ya Yusufu, nami nitawarudisha, kwa maana nawaonea rehema; nao watakuwa kana kwamba sikuwatupa; kwa maana mimi ni Bwana, Mungu wao, nami nitawasikia.
Zacharie 13.9 Zacharie 10.12 Jérémie 3.18 Esaïe 14.1 Ezéchiel 36.11
7 Na watu wa Efraimu watakuwa kama shujaa, na moyo wao utafurahi kana kwamba ni kwa divai; naam, watoto wao wataona mambo haya, na kufurahi; mioyo yao itamfurahia Bwana.
Zacharie 9.15 1 Pierre 1.8 Genèse 18.19 Genèse 43.34 Ephésiens 5.18-5.19
8 Nitawapigia kelele, na kuwakusanya pamoja; kwa maana nimewakomboa; nao wataongezeka kama walivyoongezeka.
Esaïe 5.26 Jérémie 33.22 Esaïe 7.18 Jérémie 31.10-31.11 Ezéchiel 36.10-36.11
9 Nami nitawapanda kama mbegu kati ya mataifa; nao watanikumbuka katika nchi zilizo mbali; nao watakaa pamoja na watoto wao; tena watarudi.
Ezéchiel 6.9 1 Rois 8.47-8.48 Osée 2.23 Michée 5.7 Actes 11.19-11.21
10 Tena nitawarudisha toka nchi ya Misri, nitawakusanya na kuwatoa katika Ashuru; nami nitawaingiza katika nchi ya Gileadi na Lebanoni; ila nafasi ya kuwatosha haitaonekana.
Osée 11.11 Michée 7.14 Jérémie 22.6 Ezéchiel 47.18-47.21 Esaïe 19.23-19.25
11 Naye atapita kati ya bahari ya mateso, na kuyapiga mawimbi ya bahari, na vilindi vyote vya mto wa Nile vitakauka; na kiburi cha Ashuru kitashushwa; na fimbo ya enzi ya Misri itatoweka.
Ezéchiel 30.13 Esaïe 19.5-19.7 Sophonie 2.13 Josué 3.15-3.17 Esaïe 11.15-11.16
12 Nami nitawatia nguvu katika Bwana; nao watatembea huko na huko katika jina lake, asema Bwana.
Michée 4.5 Zacharie 10.6 Esaïe 41.10 Ephésiens 6.10 1 Thessaloniciens 4.1

Cette Bible est dans le domaine public.