Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Nahum 2.5
Bible en Swahili de l’est


1 Yeye asetaye vipande vipande amepanda juu mbele ya uso wako; zishike silaha, ilinde njia, vitie nguvu viuno vyako, uongeze uwezo wako sana.
Jérémie 51.20-51.23 2 Chroniques 25.8 Jérémie 51.11-51.12 Jérémie 46.3-46.10 Nahum 3.14-3.15
2 Kwa maana Bwana anairudisha fahari ya Yakobo, kama fahari ya Israeli; maana watekao nyara wamewateka, na kuyaharibu matawi ya mizabibu yao.
Psaumes 80.12-80.13 Sophonie 3.11 Esaïe 10.5-10.12 Osée 10.1 Jérémie 25.29
3 Ngao ya mashujaa wake imefanywa kuwa nyekundu, watu walio hodari wa vita wamevaa nguo nyekundu sana; magari ya vita yametameta kwa chuma cha pua siku ya kujitengeza kwake, na mikuki inatikiswa kwa namna ya kutisha.
Ezéchiel 23.14-23.15 Zacharie 6.2 Esaïe 63.1-63.3 Apocalypse 6.4 Esaïe 14.8
4 Magari ya vita yanafanya mshindo njiani, Yanasongana-songana katika njia kuu; Kuonekana kwake ni kama mienge, Yanakwenda upesi kama umeme.
Jérémie 4.13 Nahum 3.2-3.3 Ezéchiel 26.10 Esaïe 66.15 Daniel 11.40
5 Awakumbuka watu wake wenye heshima; Wanajikwaa katika mwendo wao; Wanafanya haraka waende ukutani; Nacho kitu cha kuwafunika kimewekwa tayari.
Jérémie 46.12 Jérémie 51.27-51.28 Esaïe 21.5 Esaïe 5.27 Nahum 3.18
6 Malango ya mito yamefunguka, na jumba la mfalme limeyeyushwa.
Esaïe 45.1-45.2 2 Pierre 3.10-3.11
7 Husabu naye amefunuliwa, anachukuliwa, na wajakazi wake wanalia kama kwa sauti ya hua, wakipiga-piga vifua vyao.
Esaïe 59.11 Esaïe 38.14 Luc 23.27 Luc 23.48 Esaïe 32.12
8 Lakini Ninawi tokea zamani amekuwa kama ziwa la maji; ila hata sasa wanakimbia; Simameni! Simameni! Lakini hapana hata mmoja atazamaye nyuma.
Nahum 3.17 Jérémie 51.30 Esaïe 48.20 Jérémie 51.13 Esaïe 13.14
9 Chukueni nyara za fedha; Chukueni nyara za dhahabu; Kwa maana ni akiba isiyoisha, Fahari ya vyombo vipendezavyo.
2 Chroniques 36.10 Nahum 2.12-2.13 Esaïe 33.4 Jérémie 25.34 Ezéchiel 26.12
10 Amekuwa utupu, na ukiwa, na uharibifu; hata moyo unayeyuka, na magoti yanagongana-gongana; viunoni mwote mna utungu, na nyuso za wote zimekuwa nyeupe kwa hofu.
Joël 2.6 Psaumes 22.14 Daniel 5.6 Esaïe 13.7-13.8 Sophonie 2.13-2.15
11 Kao la simba li wapi? Na mahali walishapo wana-simba pa wapi, mahali walipotembea simba mume na simba mke na mwana-simba, wala hapana aliyewatia hofu?
Esaïe 5.29 Jérémie 2.15 Nahum 3.1 Genèse 49.9 Jérémie 50.44
12 Simba alirarua vipande vipande chakula cha kuwatosha watoto wake, aliwasongea wake zake nyama, aliyajaza mapango yake mateka, na makao yake aliyajaza mawindo.
Jérémie 51.34 Esaïe 10.6-10.14 Psaumes 17.12
13 Tazama, mimi ni juu yako, asema Bwana wa majeshi, nami nitayateketeza magari yako ya vita katika moshi, na upanga utawala wana-simba wako; nami nitayakatilia mbali mawindo yako katika nchi, na sauti za wajumbe wako hazitasikiwa tena kamwe.
2 Rois 19.23 Nahum 3.5 Psaumes 46.9 Jérémie 21.13 Josué 11.9

Cette Bible est dans le domaine public.