Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Jonas 3.6
Bible en Swahili de l’est


Prédication de Jonas à Ninive

1 Neno la Bwana likamjia Yona mara ya pili, kusema,
Jonas 1.1 Jean 21.15-21.17
2 Ondoka, uende Ninawi, mji ule mkubwa; ukaihubiri habari nitakayokuamuru.
Ezéchiel 2.7 Jonas 1.2 Jérémie 1.17 Jérémie 15.19-15.21 Ezéchiel 3.17
3 Basi Yona akaondoka, akaenda Ninawi, kama Bwana alivyonena. Basi Ninawi ulikuwa mji mkubwa mno, ukubwa wake mwendo wa siku tatu.
4 Yona akaanza kuuingia mji mwendo wa siku moja, akapaza sauti yake, akasema, Baada ya siku arobaini Ninawi utaangamizwa.
Deutéronome 18.22 Jérémie 18.7-18.10 2 Rois 20.6 Jonas 3.10 2 Rois 20.1
5 Basi watu wa Ninawi wakamsadiki Mungu; wakatangaza kufunga, wakajivika nguo za magunia, tangu yeye aliye mkubwa hata aliye mdogo.
Luc 11.32 Matthieu 12.41 2 Chroniques 20.3 Daniel 9.3 Joël 1.14
6 Habari ikamfikia mfalme wa Ninawi, naye akaondoka katika kiti chake cha enzi, akavua vazi lake, akajivika nguo za magunia, na kuketi katika majivu.
Esther 4.1-4.4 Ezéchiel 27.30-27.31 Job 2.8 Jacques 4.6-4.10 Matthieu 11.21
7 Naye akapiga mbiu, akatangaza habari katika mji wa Ninawi, kwa amri ya mfalme na wakuu wake; kusema, Mwanadamu asionje kitu, wala mnyama wala makundi ya ng’ombe, wala makundi ya kondoo; wasile, wala wasinywe maji;
2 Chroniques 20.3 Esdras 8.21 Joël 1.18 Jonas 3.5 Joël 2.15-2.16
8 bali na wafunikwe nguo za magunia, mwanadamu na mnyama pia, nao wakamlilie Mungu kwa nguvu, naam, na wageuke, kila mtu akaache njia yake mbaya, na udhalimu ulio mikononi mwake.
Esaïe 55.6-55.7 Jonas 1.6 Jonas 1.14 Esaïe 1.16-1.19 Esaïe 59.6
9 Ni nani ajuaye kwamba Mungu hatageuka na kughairi, na kuiacha hasira yake kali, ili msiangamizwe?
2 Samuel 12.22 Psaumes 106.45 Amos 5.15 Jonas 1.6 Joël 2.13-2.14
10 Mungu akaona matendo yao, ya kuwa wameiacha njia yao mbaya. Basi Mungu akalighairi neno lile baya, ambalo alisema atawatenda; asilitende.
Jérémie 18.8 Amos 7.6 Exode 32.14 1 Rois 21.27-21.29 Amos 7.3

Cette Bible est dans le domaine public.