Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Amos 4.9
Bible en Swahili de l’est


1 Lisikieni neno hili, enyi ng’ombe wa Bashani, mnaokaa juu ya mlima wa Samaria, mnaowaonea maskini, na kuwaponda wahitaji; mnaowaambia bwana zao, Haya! Leteni, tunywe.
Psaumes 22.12 Amos 6.1 Ezéchiel 39.18 Amos 5.11 Amos 3.9-3.10
2 Bwana MUNGU ameapa kwa utakatifu wake, ya kuwa, tazama, siku zitawajilia, watakapowaondoa ninyi kwa kulabu, na mabaki yenu kwa ndoana.
Psaumes 89.35 Jérémie 16.16 Amos 6.8 Esaïe 37.29 Habakuk 1.15-1.16
3 Nanyi mtatoka kwenye mahali palipobomolewa, kila mwanamke moja kwa moja mbele yake; nanyi mtajitupa katika Harmoni, asema Bwana.
Ezéchiel 12.5 Ezéchiel 12.12 Esaïe 2.20 Matthieu 16.26 Esaïe 31.7

Refus de revenir à Dieu

4 Njoni Betheli, mkakose; njoni Gilgali, mkaongeze makosa; kaleteni dhabihu zenu kila asubuhi, na zaka zenu kila siku ya tatu;
Osée 4.15 Ezéchiel 20.39 Nombres 28.3-28.4 Osée 9.15 Matthieu 23.32
5 mkachome sadaka ya shukrani, ya kitu kilichotiwa chachu; mkatangaze sadaka mtoazo kwa hiari na kuzihubiri habari zake; kwa maana ndivyo viwapendezavyo ninyi, enyi wana wa Israeli, asema Bwana MUNGU.
Lévitique 22.18-22.21 Psaumes 81.12 Osée 9.1 Matthieu 6.2 Osée 9.10
6 Mimi nami nimewapa usafi wa meno katika miji yenu yote, na kutindikiwa na mkate mahali penu pote; lakini hamkunirudia mimi, asema Bwana.
Aggée 2.17 Jérémie 5.3 Esaïe 9.13 Lévitique 26.26 Apocalypse 16.10-16.11
7 Tena nimeizuia mvua msiipate, ilipobaki miezi mitatu kabla ya mavuno; nami nimenyesha mvua juu ya mji mmoja, nikaizuia mvua isinyeshe juu ya mji mwingine; sehemu moja ilipata mvua, na sehemu isiyopata mvua ilikatika.
Exode 9.26 Jérémie 3.3 Exode 10.23 Exode 9.4 Esaïe 5.6
8 Basi kutoka miji miwili mitatu walitanga-tanga kuendea mji mwingine wapate kunywa maji, wasipate ya kuwatosha; lakini hamkunirudia mimi, asema Bwana.
Amos 4.6 Aggée 1.6 1 Rois 18.5 Osée 7.10 Jérémie 3.7
9 Nami nimewapiga kwa ukavu na koga; wingi wa bustani zenu na mashamba yenu ya mizabibu, na mitini yenu na mizeituni yenu imeliwa na tunutu; Lakini hamkunirudia mimi, asema Bwana.
Aggée 2.17 Deutéronome 28.22 Joël 1.4 Amos 7.1-7.2 Amos 4.6
10 Nimewapelekea tauni, kama tauni ya Misri; vijana wenu nimewaua kwa upanga, na farasi wenu nimewachukulia mbali; nami nimeupandisha uvundo wa matuo yenu na kuuingiza katika mianzi ya pua zenu; lakini hamkunirudia mimi, asema Bwana.
Lévitique 26.25 Deutéronome 28.60 Joël 2.20 2 Rois 13.7 Jérémie 11.22
11 Baadhi yenu nimewaangamiza, kama hapo Mungu alipoiangamiza Sodoma na Gomora, nanyi mkawa kama kinga kilichonyakuliwa motoni; lakini hamkunirudia mimi, asema Bwana.
Esaïe 13.19 Zacharie 3.2 Genèse 19.24-19.25 Amos 4.6 Jude 1.23
12 Basi nitakutenda hivi, Ee Israeli, na kwa sababu nitakutenda hivi, ujiweke tayari kuonana na Mungu wako, Ee Israeli.
1 Thessaloniciens 5.2-5.4 Jacques 4.1-4.10 Amos 5.4-5.15 Matthieu 5.25 Amos 9.1-9.4
13 Kwa maana, angalia, yeye aifanyizaye milima, na kuuumba upepo, na kumwambia mwanadamu mawazo yake, afanyaye asubuhi kuwa giza, na kupakanyaga mahali pa dunia palipoinuka; Bwana, Mungu wa majeshi, ndilo jina lake.
Amos 5.8 Michée 1.3 Amos 9.6 Jérémie 10.16 Daniel 2.28

Cette Bible est dans le domaine public.