1 Lisikieni neno hili, enyi ng’ombe wa Bashani, mnaokaa juu ya mlima wa Samaria, mnaowaonea maskini, na kuwaponda wahitaji; mnaowaambia bwana zao, Haya! Leteni, tunywe.
Psaumes 22.12  Amos 6.1  Amos 5.11  Ezéchiel 39.18  Psaumes 140.12  
 2 Bwana MUNGU ameapa kwa utakatifu wake, ya kuwa, tazama, siku zitawajilia, watakapowaondoa ninyi kwa kulabu, na mabaki yenu kwa ndoana.Jérémie 16.16  Psaumes 89.35  Amos 6.8  Habakuk 1.15-1.16  Esaïe 37.29  
 3 Nanyi mtatoka kwenye mahali palipobomolewa, kila mwanamke moja kwa moja mbele yake; nanyi mtajitupa katika Harmoni, asema Bwana.
Ezéchiel 12.5  Ezéchiel 12.12  Matthieu 16.26  Esaïe 31.7  2 Rois 7.15  
Refus de revenir à Dieu
 4 Njoni Betheli, mkakose; njoni Gilgali, mkaongeze makosa; kaleteni dhabihu zenu kila asubuhi, na zaka zenu kila siku ya tatu;
Osée 4.15  Ezéchiel 20.39  Osée 9.15  Matthieu 23.32  Osée 12.11  
 5 mkachome sadaka ya shukrani, ya kitu kilichotiwa chachu; mkatangaze sadaka mtoazo kwa hiari na kuzihubiri habari zake; kwa maana ndivyo viwapendezavyo ninyi, enyi wana wa Israeli, asema Bwana MUNGU.
Psaumes 81.12  Lévitique 22.18-22.21  Osée 9.1  Matthieu 6.2  Osée 9.10  
 6 Mimi nami nimewapa usafi wa meno katika miji yenu yote, na kutindikiwa na mkate mahali penu pote; lakini hamkunirudia mimi, asema Bwana.
Aggée 2.17  Jérémie 5.3  Esaïe 9.13  Lévitique 26.26  2 Chroniques 28.22  
 7 Tena nimeizuia mvua msiipate, ilipobaki miezi mitatu kabla ya mavuno; nami nimenyesha mvua juu ya mji mmoja, nikaizuia mvua isinyeshe juu ya mji mwingine; sehemu moja ilipata mvua, na sehemu isiyopata mvua ilikatika.
Exode 9.26  Jérémie 3.3  Exode 10.23  Exode 9.4  Esaïe 5.6  
 8 Basi kutoka miji miwili mitatu walitanga-tanga kuendea mji mwingine wapate kunywa maji, wasipate ya kuwatosha; lakini hamkunirudia mimi, asema Bwana.
Amos 4.6  Aggée 1.6  1 Rois 18.5  Esaïe 41.17-41.18  Jérémie 23.14  
 9 Nami nimewapiga kwa ukavu na koga; wingi wa bustani zenu na mashamba yenu ya mizabibu, na mitini yenu na mizeituni yenu imeliwa na tunutu; Lakini hamkunirudia mimi, asema Bwana.
Aggée 2.17  Deutéronome 28.22  Joël 1.4  Amos 7.1-7.2  Amos 4.6  
 10 Nimewapelekea tauni, kama tauni ya Misri; vijana wenu nimewaua kwa upanga, na farasi wenu nimewachukulia mbali; nami nimeupandisha uvundo wa matuo yenu na kuuingiza katika mianzi ya pua zenu; lakini hamkunirudia mimi, asema Bwana.
Deutéronome 28.60  Joël 2.20  Lévitique 26.25  2 Rois 13.7  Jérémie 11.22  
 11 Baadhi yenu nimewaangamiza, kama hapo Mungu alipoiangamiza Sodoma na Gomora, nanyi mkawa kama kinga kilichonyakuliwa motoni; lakini hamkunirudia mimi, asema Bwana.
Zacharie 3.2  Esaïe 13.19  Genèse 19.24-19.25  Jude 1.23  Amos 4.6  
 12 Basi nitakutenda hivi, Ee Israeli, na kwa sababu nitakutenda hivi, ujiweke tayari kuonana na Mungu wako, Ee Israeli.
Jacques 4.1-4.10  1 Thessaloniciens 5.2-5.4  Matthieu 5.25  Amos 9.1-9.4  Osée 13.8  
 13 Kwa maana, angalia, yeye aifanyizaye milima, na kuuumba upepo, na kumwambia mwanadamu mawazo yake, afanyaye asubuhi kuwa giza, na kupakanyaga mahali pa dunia palipoinuka; Bwana, Mungu wa majeshi, ndilo jina lake.
Amos 5.8  Michée 1.3  Amos 9.6  Daniel 2.28  Esaïe 47.4