Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Daniel 9.13
Bible en Swahili de l’est


Prière et confession de Daniel

1 Katika mwaka wa kwanza wa Dario, mwana wa Ahasuero, wa uzao wa Wamedi, aliyetawazwa kuwa mfalme juu ya milki ya Wakaldayo;
Daniel 11.1 Daniel 1.21 Daniel 5.31-6.1 Daniel 6.28
2 katika mwaka wa kwanza wa kumiliki kwake, mimi Danielii, kwa kuvisoma vitabu, nalifahamu hesabu ya miaka, ambayo neno la Bwana lilimjia Yeremia nabii, ya kuutimiza ukiwa wa Yerusalemu, yaani, miaka sabini.
2 Chroniques 36.21 Jérémie 29.10 Zacharie 7.5 Jérémie 25.11-25.12 Esdras 1.1
3 Nikamwelekezea Bwana Mungu uso wangu, ili kutaka kwa maombi, na dua, pamoja na kufunga, na kuvaa nguo za magunia na majivu.
Esdras 9.5 Psaumes 35.13 Esther 4.16 Esdras 10.6 Néhémie 9.1
4 Nikamwomba Bwana, Mungu wangu, nikaungama, nikasema, Ee Bwana, Mungu mkuu, mwenye kutisha, ashikaye maagano na rehema kwao wampendao, na kuzishika amri zake;
Deutéronome 7.9 Néhémie 9.32 1 Rois 8.23 Jacques 1.12 Michée 7.18-7.20
5 tumefanya dhambi, tumefanya ukaidi, tumetenda maovu, tumeasi, naam, hata kwa kuyaacha maagizo yako na hukumu zako;
Psaumes 106.6 Esaïe 64.5-64.7 Jérémie 14.7 Daniel 9.15 1 Rois 8.47-8.50
6 wala hatukuwasikiliza watumishi wako, manabii, ambao kwa jina lako walisema na wafalme wetu, na wakuu wetu, na baba zetu, na watu wote wa nchi.
Esdras 9.7 2 Chroniques 36.15-36.16 Luc 20.10-20.12 Jérémie 44.4-44.5 Néhémie 9.34
7 Ee Bwana, haki ina wewe, lakini kwetu sisi kuna haya ya uso, kama hivi leo; kwa watu wa Yuda, na kwa wenyeji wa Yerusalemu, na kwa Israeli wote, walio karibu na hao walio mbali, katika nchi zote ulikowafukuza, kwa sababu ya makosa yao waliyokukosa.
Jérémie 3.25 Deutéronome 4.27 Psaumes 44.15 Jérémie 2.26-2.27 Daniel 9.14
8 Ee Bwana, kwetu sisi kuna haya ya uso, kwa wafalme wetu, na wakuu wetu, na baba zetu, kwa sababu tumekutenda dhambi.
Daniel 9.6-9.7 Jérémie 14.20 Lamentations 1.7-1.8 Lamentations 5.16 Lamentations 3.42
9 Rehema na msamaha ni kwa Bwana Mungu wetu, ingawa tumemwasi;
Psaumes 86.15 Jérémie 14.7 Psaumes 130.4 Daniel 9.5 Ephésiens 2.4-2.7
10 wala hatukuitii sauti ya Bwana, Mungu wetu, kwa kwenda katika sheria zake, alizoziweka mbele yetu kwa kinywa cha watumishi wake, manabii.
2 Rois 18.12 Daniel 9.6 Esdras 9.10-9.11 Néhémie 9.13-9.17 2 Rois 17.13-17.15
11 Naam, Israeli wote wameihalifu sheria yako, kwa kugeuka upande, wasiisikilize sauti yako; basi kwa hiyo laana imemwagwa juu yetu, na uapo ule ulioandikwa katika sheria ya Musa, mtumishi wa Mungu; kwa sababu tumemtenda dhambi.
Esaïe 1.4-1.6 Jérémie 8.5-8.10 Deutéronome 27.15-27.26 Deutéronome 28.15-28.68 Lévitique 26.14-26.46
12 Naye ameyathibitisha maneno yake, aliyoyanena juu yetu, na juu ya waamuzi wetu waliotuamua, kwa kumletea mambo maovu makuu; maana chini ya mbingu zote halikutendeka jambo kama hili, lilivyotendeka juu ya Yerusalemu.
Ezéchiel 5.9 Lamentations 1.12 Esaïe 44.26 Psaumes 148.11 Job 12.17
13 Kama ilivyoandikwa katika sheria ya Musa, mabaya haya yote yametupata lakini hata hivyo hatukumwomba Bwana, Mungu wetu, atupe fadhili zake, ili tugeuke na kuyaacha maovu yetu, na kuitambua kweli yake.
Esaïe 9.13 Daniel 9.11 Jérémie 2.30 Jérémie 5.3 Psaumes 119.27
14 Basi Bwana ameyavizia mabaya hayo, akatuletea; maana Bwana, Mungu wetu ni mwenye haki katika kazi zake zote azitendazo; na sisi hatukuitii sauti yake.
Daniel 9.7 Néhémie 9.33 Jérémie 44.27 Jérémie 31.28 Psaumes 51.14
15 Na sasa, Ee Bwana Mungu wetu, uliyewatoa watu wako hawa katika nchi ya Misri kwa mkono hodari, ukajipatia sifa, kama ilivyo leo; tumefanya dhambi, tumetenda maovu.
Néhémie 9.10 Exode 14.18 Exode 32.11 Exode 6.1 Daniel 9.5
16 Ee Bwana sawasawa na haki yako yote, nakusihi, hasira yako na ghadhabu yako zigeuzwe na kuuacha mji wako Yerusalemu, mlima wako mtakatifu; maana kwa sababu ya dhambi zetu, na maovu ya baba zetu, Yerusalemu na watu wako wamepata kulaumiwa na watu wote wanaotuzunguka.
Zacharie 8.3 Daniel 9.20 Psaumes 31.1 Exode 20.5 Psaumes 71.2
17 Basi sasa, Ee Mungu wetu, yasikilize maombi ya mtumishi wako, na dua zake, ukaangazishe uso wako juu ya patakatifu pako palipo ukiwa, kwa ajili ya Bwana.
Lamentations 5.18 Psaumes 80.19 Psaumes 80.7 Psaumes 80.3 Psaumes 67.1
18 Ee Mungu wangu, tega sikio lako, ukasikie; fumbua macho yako ukautazame ukiwa wetu, na mji ule ulioitwa kwa jina lako; maana hatukutolei maombi yetu kwa sababu ya haki yetu, lakini kwa sababu ya rehema zako nyingi.
Esaïe 37.17 Jérémie 36.7 Jérémie 25.29 Jérémie 14.7 2 Rois 19.16
19 Ee Bwana, usikie; Ee Bwana, usamehe; Ee Bwana, usikilize, ukatende, usikawie; kwa ajili yako wewe, Ee Mungu wangu; kwa sababu mji wako na watu wako wanaitwa kwa jina lako.
Daniel 9.18 Luc 11.8 Amos 7.2 Jérémie 14.9 Jérémie 14.7

Les 70 semaines

20 Basi hapo nilipokuwa nikisema, na kuomba, na kuiungama dhambi yangu, na dhambi ya watu wangu Israeli, na kuomba dua yangu mbele za Bwana, Mungu wangu, kwa ajili ya mlima mtakatifu wa Mungu wangu;
Esaïe 58.9 Psaumes 145.18 Daniel 9.16 Esaïe 65.24 Esaïe 6.5
21 naam, nilipokuwa nikinena katika kuomba, mtu yule, Gabrieli, niliyemwona katika njozi hapo kwanza, akirushwa upesi, alinigusa panapo wakati wa dhabihu ya jioni.
Daniel 8.16 Luc 1.19 Daniel 10.16 1 Rois 18.36 Hébreux 1.14
22 Akaniagiza, akaongea nami, akasema, Ee Danielii, nimetokea sasa, ili nikupe akili upate kufahamu.
Daniel 8.16 Daniel 10.21 Zacharie 1.9 Apocalypse 4.1 Daniel 9.24-9.27
23 Mwanzo wa maombi yako ilitolewa amri, nami nimekuja kukupasha habari; maana wewe unapendwa sana; basi itafakari habari hii, na kuyafahamu maono haya.
Daniel 10.19 Daniel 10.11-10.12 Matthieu 24.15 Luc 1.28 Ezéchiel 26.12
24 Muda wa majuma sabini umeamriwa juu ya watu wako, na juu ya mji wako mtakatifu, ili kukomesha makosa, na kuishiliza dhambi, na kufanya upatanisho kwa ajili ya uovu, na kuleta haki ya milele, na kutia muhuri maono na unabii, na kumtia mafuta yeye aliye mtakatifu.
Jérémie 23.5-23.6 Esaïe 61.1 Esaïe 56.1 Psaumes 45.7 Ezéchiel 4.6
25 Basi ujue na kufahamu, ya kuwa tangu kuwekwa amri ya kutengeneza na kuujenga upya Yerusalemu hata zamani zake masihi aliye mkuu; kutakuwa na majuma saba; na katika majuma sitini na mawili utajengwa tena pamoja na njia kuu zake na handaki, naam, katika nyakati za taabu.
Esdras 4.24 Esaïe 9.6 Esaïe 55.4 Jean 1.41 Jean 4.25
26 Na baada ya yale majuma sitini na mawili, masihi atakatiliwa mbali, naye atakuwa hana kitu; na watu wa mkuu atakayekuja watauangamiza mji, na patakatifu; na mwisho wake utakuwa pamoja na gharika, na hata mwisho ule vita vitakuwapo; ukiwa umekwisha kukusudiwa.
Esaïe 53.8 Nahum 1.8 Matthieu 24.2 Marc 9.12 Luc 24.26
27 Naye atafanya agano thabiti na watu wengi kwa muda wa juma moja; na kwa nusu ya juma hiyo ataikomesha sadaka na dhabihu; na mahali pake litasimama chukizo la uharibifu; na hivyo, hata ukomo, na ghadhabu iliyokusudiwa imemwagwa juu yake mwenye kuharibu.
Matthieu 24.15 Esaïe 10.22-10.23 Daniel 12.11 Luc 21.20 Marc 13.14

Cette Bible est dans le domaine public.