Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Ezéchiel 35.5
Bible en Swahili de l’est


Prophétie contre Édom

1 Tena neno la Bwana likanijia, kusema,
Ezéchiel 21.1 2 Pierre 1.21 Ezéchiel 34.1 Ezéchiel 22.1
2 Mwanadamu, kaza uso wako juu ya mlima Seiri, ukatabiri juu yake,
Ezéchiel 6.2 Ezéchiel 25.8 Genèse 32.3 2 Chroniques 25.11-25.14 Abdias 1.10-1.14
3 uuambie, Bwana MUNGU asema hivi; Tazama, mimi ni juu yako, Ee mlima Seiri, nami nitaunyosha mkono wangu juu yako, nami nitakufanya kuwa ukiwa na ajabu.
Jérémie 6.12 Ezéchiel 6.14 Ezéchiel 35.7 Jérémie 15.6 Nahum 2.13
4 Miji yako nitaiharibu, nawe utakuwa ukiwa; nawe utajua ya kuwa mimi ndimi Bwana.
Ezéchiel 35.9 Malachie 1.3-1.4 Ezéchiel 35.12 Joël 3.19 Ezéchiel 6.6-6.7
5 Kwa kuwa umekuwa na uadui usiokoma, nawe umewatoa wana wa Israeli wapigwe kwa nguvu za upanga, wakati wa msiba wao, wakati wa mwisho wa uovu.
Psaumes 137.7 Ezéchiel 21.29 Ezéchiel 21.25 Amos 1.11 Ezéchiel 25.12
6 Basi, kama mimi niishivyo, asema Bwana MUNGU, nitakuweka tayari kwa damu, na damu itakufuatia; ikiwa hukuchukia damu, basi damu itakufuatia.
Esaïe 63.2-63.6 Apocalypse 18.24 Abdias 1.15 Psaumes 109.16-109.17 Apocalypse 19.2-19.3
7 Hivyo ndivyo nitakavyoufanya mlima Seiri kuwa ajabu na ukiwa; nami nitakatilia mbali nao mtu apitaye, na mtu arejeaye.
Ezéchiel 35.3 Ezéchiel 29.11 Ezéchiel 33.28 Ezéchiel 35.9 2 Chroniques 15.5-15.6
8 Nami nitaijaza milima yake watu wake waliouawa; katika milima yako, na katika mabonde yako, na katika mifereji yako ya maji yote, wataanguka wao watakaouawa kwa upanga.
Ezéchiel 31.12 Ezéchiel 32.4-32.5 Ezéchiel 39.4-39.5 Esaïe 34.2-34.7
9 Nitakufanya kuwa ukiwa wa daima, na miji yako haitakaliwa na watu; nanyi mtajua ya kuwa mimi ndimi Bwana.
Ezéchiel 25.13 Ezéchiel 35.4 Ezéchiel 6.7 Ezéchiel 36.11 Jérémie 49.13
10 Kwa sababu umesema, Mataifa haya mawili na nchi hizi mbili zitakuwa zangu, nasi tutazimiliki, ijapokuwa Bwana alikuwako huko.
Ezéchiel 36.5 Ezéchiel 48.35 Psaumes 132.13-132.14 Esaïe 12.6 Ezéchiel 36.2
11 Basi, kama mimi niishivyo, asema Bwana MUNGU, nitatenda kwa kadiri ya hasira yako, na kwa kadiri ya wivu wako, ulioudhihirisha kwa kuwachukia; nami nitajidhihirisha kwao, nitakapokuhukumu wewe.
Matthieu 7.2 Psaumes 9.16 Psaumes 137.7 Amos 1.11 Psaumes 73.17-73.18
12 Nawe utajua ya kuwa mimi, Bwana, nimeyasikia matukano yako yote, uliyoyanena juu ya milima ya Israeli, ukisema, Wamefanyika ukiwa, wametiwa katika mikono yetu tuwale.
Ezéchiel 36.2 Psaumes 94.9-94.10 Ezéchiel 35.9 Psaumes 83.12 Ezéchiel 6.7
13 Nanyi mmejitukuza juu yangu kwa vinywa vyenu, na kuyaongeza maneno juu yangu; nimesikia mimi.
Daniel 11.36 Jérémie 29.23 Esaïe 36.20 Ezéchiel 35.12 1 Samuel 2.3
14 Bwana MUNGU asema hivi; Dunia yote itakapofurahi, nitakufanya kuwa ukiwa.
Esaïe 14.7-14.8 Esaïe 65.13-65.15 Jérémie 51.48
15 Kama vile ulivyofurahi juu ya urithi wa nyumba ya Israeli, kwa sababu ilikuwa ukiwa, ndivyo nitakavyokutenda wewe; utakuwa ukiwa, Ee mlima Seiri, na Edomu yote, naam, yote pia; nao watajua ya kuwa mimi ndimi Bwana.
Ezéchiel 35.3-35.4 Esaïe 34.5-34.6 Lamentations 4.21 Psaumes 137.7 Abdias 1.15

Cette Bible est dans le domaine public.