Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Ezéchiel 30.26
Bible en Swahili de l’est


1 Neno la Bwana likanijia tena, kusema,
2 Mwanadamu, tabiri, useme, Bwana MUNGU asema hivi; Pigeni makelele ya uchungu, Ole wa siku ile!
Esaïe 13.6 Esaïe 15.2 Joël 1.5 Joël 1.11 Ezéchiel 21.12
3 Kwa maana siku ile i karibu, siku ile ya Bwana i karibu, siku ya mawingu; itakuwa wakati wa mataifa.
Abdias 1.15 Ezéchiel 7.7 Ezéchiel 7.12 Ezéchiel 34.12 Ezéchiel 30.18
4 Na upanga utakuja juu ya Misri, na dhiki itakuwa katika Kushi, watakapoanguka watu waliouawa katika Misri, nao watauondoa wingi wa watu wake, na misingi yake itabomolewa.
Ezéchiel 29.19 Ezéchiel 29.8 Psaumes 48.6-48.7 Apocalypse 18.9-18.10 Ezéchiel 30.9-30.10
5 Kushi, na Putu, na Ludi, na watu wote waliochanganyika, na Kubu, na wana wa nchi ya agano, wataanguka kwa upanga pamoja nao.
Jérémie 25.20 Ezéchiel 27.10 Jérémie 25.24 Esaïe 18.1 Esaïe 20.4
6 Bwana asema hivi; Nao pia wanaoitegemeza Misri wataanguka, na kiburi cha uwezo wake kitashuka; toka Migdoli hata Sewene, wataanguka ndani yake kwa upanga, asema Bwana MUNGU.
Ezéchiel 29.10 Esaïe 20.3-20.6 Esaïe 31.3 Job 9.13 Nahum 3.9
7 Nao watakuwa ukiwa, kati ya nchi zilizo ukiwa, na miji yake itakuwamo kati ya miji iliyoharibika.
Ezéchiel 29.12 Jérémie 25.18-25.26 Jérémie 46.1-46.28 Ezéchiel 32.18-32.32
8 Nao watajua ya kuwa mimi ndimi Bwana, nitakapoweka moto katika Misri, na hao wote wamsaidiao watakapoangamia.
Ezéchiel 29.6 Amos 1.14 Ezéchiel 30.14 Amos 1.4 Ezéchiel 30.16
9 Katika siku hiyo watatoka wajumbe mbele zangu katika merikebu, ili kuwatia hofu Wakushi, wanaojiona kuwa salama, na dhiki itakuwa juu yao, vile vile kama katika siku ya Misri; kwa maana, tazama, inakuja.
Esaïe 18.1-18.2 Ezéchiel 32.9-32.10 Esaïe 23.5 Esaïe 47.8 Esaïe 19.17
10 Bwana MUNGU asema hivi; Pia nitaukomesha wingi wa watu wa Misri, kwa mkono wa Nebukadreza, mfalme wa Babeli.
Ezéchiel 29.19 Ezéchiel 29.4-29.5 Ezéchiel 30.24-30.25 Ezéchiel 32.11-32.16
11 Yeye, na watu wake pamoja naye, watu wa mataifa watishao, wataletwa waingie katika nchi waiharibu, nao watafuta panga zao wapigane na Misri, na kuijaza nchi wale waliouawa.
Ezéchiel 28.7 Ezéchiel 32.12 Esaïe 14.4-14.6 Ezéchiel 39.11-39.20 Ezéchiel 39.4
12 Nami nitaikausha mito, na kuiuza nchi, na kuitia katika mikono ya watu wabaya; nami nitaifanya nchi kuwa ukiwa, na watu wote walio ndani yake, kwa mkono wa wageni; mimi, Bwana, nimenena neno hili.
Ezéchiel 29.3 Nahum 1.4 Jérémie 51.36 Ezéchiel 28.10 Esaïe 44.27
13 Bwana MUNGU asema hivi; Pia nitaviharibu vinyago, nami nitavikomesha vitu vya ubatili katika Nofu, wala hapatakuwa na mkuu tena atokaye katika nchi ya Misri, nami nitatia hofu katika nchi ya Misri.
Zacharie 10.11 Jérémie 46.14 Jérémie 2.16 Zacharie 13.2 Jérémie 46.25
14 Nami nitaifanya Pathrosi kuwa ukiwa, nami nitatia moto katika Soani, nami nitatekeleza hukumu katika No.
Ezéchiel 29.14 Jérémie 46.25 Psaumes 78.43 Psaumes 78.12 Nahum 3.8
15 Nami nitamwaga ghadhabu yangu juu ya Sini, ngome ya Misri, nami nitakatilia mbali wingi wa watu wa No.
Apocalypse 16.1 Nahum 1.6 Psaumes 11.6
16 Nami nitatia moto katika Misri; Sini itakuwa katika dhiki kuu, na No itavunjika kabisa; na Nofu itakuwa na adui wakati wa mchana.
Ezéchiel 28.18 Ezéchiel 30.8-30.9
17 Vijana wa Oni, na wa Pi-besethi, wataanguka kwa upanga; na miji hiyo itakwenda utumwani.
Genèse 41.45
18 Huko Tapanesi nako mchana utakuwa giza, nitakapovunja huko kongwa za Misri, na kiburi cha uwezo wake kitakoma ndani yake, na katika habari zake, wingu litaifunika, na binti zake watakwenda utumwani.
Ezéchiel 30.3 Esaïe 10.27 Jérémie 2.16 Joël 3.15 Jérémie 43.7-43.9
19 Hivyo ndivyo nitakavyotekeleza hukumu katika Misri; nao watajua ya kuwa mimi ndimi Bwana.
Ezéchiel 30.14 Ezéchiel 5.8 Ezéchiel 25.11 Ezéchiel 5.15 Psaumes 9.16
20 Ikawa katika mwaka wa kumi na mmoja, mwezi wa kwanza, siku ya saba ya mwezi, neno la Bwana likanijia, kusema,
Ezéchiel 29.17 Ezéchiel 26.1 Ezéchiel 29.1 Ezéchiel 31.1 Ezéchiel 1.2
21 Mwanadamu, nimeuvunja mkono wa Farao, mfalme wa Misri, na tazama, haukufungwa ili kuutia dawa, haukuzongwa kwa kitambaa, upate kuwa na nguvu za kushika upanga.
Jérémie 30.13 Jérémie 46.11 Jérémie 48.25 Ezéchiel 30.24 Psaumes 37.17
22 Basi Bwana MUNGU asema hivi; Tazama, mimi ni juu ya Farao, mfalme wa Misri, nami nitamvunja mikono yake, mkono ulio wenye nguvu, na huo uliovunjika, nami nitauangusha upanga ulio katika mkono wake.
2 Rois 24.7 Ezéchiel 29.3 Psaumes 37.17 Jérémie 37.7 Ezéchiel 34.16
23 Nami nitawatawanya Wamisri kati ya mataifa, na kuwatapanya kati ya nchi mbalimbali.
Ezéchiel 30.17-30.18 Ezéchiel 30.26 Ezéchiel 29.12-29.13
24 Nami nitaitia nguvu mikono ya mfalme wa Babeli, na kuutia upanga wangu katika mkono wake, bali mikono ya Farao nitaivunja, naye ataugua mbele yake, kwa mauguzi ya mtu aliyetiwa jeraha ya kumfisha.
Sophonie 2.12 Ezéchiel 30.25 Esaïe 45.1 Néhémie 6.9 Esaïe 45.5
25 Nami nitaitegemeza mikono ya mfalme wa Babeli, na mikono ya Farao itaanguka; nao watajua ya kuwa mimi ndimi Bwana, nitakapoutia upanga wangu katika mkono wa mfalme wa Babeli, naye ataunyosha juu ya nchi ya Misri.
Ezéchiel 32.15 Ezéchiel 30.26 Psaumes 9.16 Ezéchiel 39.21-39.22 Ezéchiel 38.23
26 Nami nitawatawanya Wamisri kati ya mataifa, na kuwatapanya kati ya nchi mbalimbali; nao watajua ya kuwa mimi ndimi Bwana.
Ezéchiel 29.12 Ezéchiel 30.17-30.18 Ezéchiel 30.23 Ezéchiel 6.13 Daniel 11.42

Cette Bible est dans le domaine public.