Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Ezéchiel 13.12
Bible en Swahili de l’est


Condamnation des prétendus prophètes

1 Kisha neno la Bwana likanijia, kusema,
2 Mwanadamu, tabiri juu ya manabii wa Israeli wanaotabiri, uwaambie wanaotabiri kwa mioyo yao wenyewe, Lisikieni neno la Bwana;
Ezéchiel 13.17 Jérémie 37.19 Ezéchiel 22.28 Esaïe 1.10 Ezéchiel 22.25
3 Bwana MUNGU asema hivi; Ole wao manabii wajinga, wanaoifuata roho yao wenyewe, wala hawakuona neno lo lote!
Jérémie 23.28-23.32 Lamentations 2.14 Osée 9.7 Zacharie 11.15 Ezéchiel 34.2
4 Ee Israeli, manabii wako wamekuwa kama mbweha, mahali palipo ukiwa.
1 Timothée 4.1-4.2 Tite 1.10-1.12 Apocalypse 19.20 Romains 16.18 Michée 2.11
5 Hamkupanda kwenda mahali palipobomolewa, wala hamkuitengenezea nyumba ya Israeli boma, wapate kusimama vitani katika siku ya Bwana.
Ezéchiel 22.30 Esaïe 58.12 Psaumes 106.23 Esaïe 13.6 Esaïe 13.9
6 Wameona ubatili, na uganga wa uongo, hao wasemao, Bwana asema; lakini Bwana hakuwatuma; nao wamewatumainisha watu ya kuwa neno lile litatimizwa.
Ezéchiel 22.28 Jérémie 28.15 Jérémie 37.19 Jérémie 14.14 Jérémie 29.8
7 Je! Hamkuona maono ya bure, hamkunena mabashiri ya uongo? Nanyi mwasema, Bwana asema; ila mimi sikusema neno.
Matthieu 24.23-24.24 Ezéchiel 13.2-13.3 Ezéchiel 13.6
8 Basi tazama, Bwana MUNGU asema hivi; Kwa sababu mmenena ubatili, na kuona uongo, basi, kwa sababu hiyo, mimi ni juu yenu, asema Bwana MUNGU.
Ezéchiel 5.8 Ezéchiel 21.3 Nahum 2.13 Ezéchiel 28.22 Ezéchiel 35.3
9 Na mkono wangu utakuwa juu ya manabii wanaoona ubatili, na kutabiri uongo; hawatakuwa katika mashauri ya watu wangu, wala hawataandikwa katika maandiko ya nyumba ya Israeli, wala hawataingia katika nchi ya Israeli; nanyi mtajua ya kuwa mimi ndimi Bwana MUNGU.
Ezéchiel 20.38 Psaumes 69.28 Psaumes 87.6 Jérémie 28.15-28.17 Daniel 12.1
10 Kwa sababu hiyo, kwa sababu wameshawishi watu wangu, wakisema, Amani; wala hapana amani; na mtu mmoja ajengapo ukuta, tazama, waupaka chokaa isiyokorogwa vema;
Ezéchiel 13.16 Ezéchiel 22.28 Jérémie 6.14 2 Rois 21.9 Jérémie 8.11
11 basi waambie hao wanaoupaka ukuta chokaa isiyokorogwa vema, ya kwamba utaanguka; kutakuwa mvua ya kufurika; nanyi, enyi mvua ya mawe makubwa ya barafu, mtaanguka; na upepo wa dhoruba utaupasua.
Ezéchiel 38.22 Esaïe 28.2 Esaïe 28.15-28.18 Nahum 1.3 Psaumes 18.13-18.14
12 Na huo ukuta utakapoanguka, je! Hamtaambiwa, Ku wapi kupaka kwenu mlikoupaka?
Jérémie 2.28 Juges 9.38 Jérémie 37.19 Juges 10.14 2 Rois 3.13
13 Basi Bwana MUNGU asema hivi; Nitaupasua kwa upepo wa dhoruba, katika ghadhabu yangu; tena kutakuwa mvua ya barafu ya kufurika katika hasira yangu; na mawe makubwa ya barafu katika hasira ya kuukomesha.
Esaïe 30.30 Apocalypse 11.19 Apocalypse 16.21 Psaumes 148.8 Psaumes 18.12-18.13
14 Ndivyo nitakavyoubomoa ukuta mlioupaka chokaa isiyokorogwa vema, na kuuangusha chini, hata misingi yake itafunuliwa; nao utaanguka, nanyi mtaangamizwa katikati yake; nanyi mtajua ya kuwa mimi ndimi Bwana.
Michée 1.6 Jérémie 6.15 Habakuk 3.13 Ezéchiel 13.9 Jérémie 14.15
15 Ndivyo nitakavyotimiza ghadhabu yangu juu ya ukuta ule, na juu yao walioupaka chokaa isiyokorogwa vema; nami nitawaambieni, Ukuta huo hauko sasa, wala wao walioupaka hawako;
Néhémie 4.3 Psaumes 62.3 Esaïe 30.13
16 yaani, manabii wa Israeli, watabirio habari za Yerusalemu, na kuona maono ya amani katika habari zake; wala hapana amani, asema Bwana MUNGU.
Jérémie 6.14 Ezéchiel 13.10 Jérémie 8.11 Esaïe 57.20-57.21 Jérémie 28.1
17 Na wewe, mwanadamu, kaza uso wako juu ya binti za watu wako, watabirio kwa akili zao wenyewe; ukatabiri juu yao,
Ezéchiel 13.2 Juges 4.4 2 Rois 22.14 Apocalypse 2.20 Luc 2.36
18 useme, Bwana MUNGU asema hivi; Ole wao wanawake wale, washonao hirizi katika viungo vyote vya mikono, wawekao leso juu ya vichwa vya kila kimo, ili wawinde roho za watu; je! Mtaziwinda roho za watu wangu, na kuzihifadhi hai roho zenu wenyewe?
2 Pierre 2.14 Ezéchiel 13.20 Ephésiens 4.14 2 Timothée 4.3 Ezéchiel 22.25
19 Nanyi mmeninajisi kati ya watu wangu, kwa ajili ya makonzi ya shayiri na vipande vya mkate, ili kuziua roho za watu ambao haiwapasi kufa, na kuzihifadhi hai roho za watu ambao haikuwapasa kuwa hai, kwa kuwaambia uongo watu wangu wasikilizao uongo.
Proverbes 28.21 Michée 3.5 Jérémie 23.17 Jérémie 23.14 Ezéchiel 20.39
20 Basi Bwana MUNGU asema hivi; Tazama, mimi ni kinyume cha hirizi zenu, ambazo kwa hizo mnaziwinda roho za watu kama ndege, nami nitazitoa katika mikono yenu kwa nguvu; nami nitaziachilia roho zile mnazoziwinda kama ndege.
2 Timothée 3.8-3.9 Ezéchiel 13.18 Ezéchiel 13.15-13.16 Ezéchiel 13.8-13.9
21 Na leso zenu nazo nitazirarua, na kuwaokoa watu wangu katika mikono yenu, wala hawatakuwa katika mikono yenu tena kuwindwa; nanyi mtajua ya kuwa mimi ndimi Bwana.
Psaumes 91.3
22 Kwa kuwa ninyi mmemhuzunisha moyo mwenye haki kwa uongo, ambaye mimi sikumhuzunisha; na kuitia nguvu mikono ya mtu mbaya, hata asigeuke, na kuiacha njia yake mbaya, na kuhifadhika;
Jérémie 23.14 Ezéchiel 9.4 Jérémie 4.10 Jérémie 14.13-14.17 Genèse 3.4-3.5
23 basi, kwa sababu hiyo ninyi hamtaona tena ubatili, wala kutabiri mambo; nami nitawaokoa watu wangu katika mikono yenu; nanyi mtajua ya kuwa mimi ndimi Bwana.
Ezéchiel 13.21 Michée 3.6 Ezéchiel 12.24 Apocalypse 12.11 Zacharie 13.3

Cette Bible est dans le domaine public.