Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Jérémie 5.31
Bible en Swahili de l’est


Raisons du jugement

1 Pigeni mbio huku na huku katika njia za Yerusalemu, mkaone sasa, na kujua, na kutafuta katika viwanja vyake, kwamba mwaweza kumpata mtu mmoja, kwamba yuko mtu mmoja awaye yote atendaye kwa haki, atafutaye uaminifu; nami nitausamehe mji huo.
2 Chroniques 16.9 Ezéchiel 22.30 Genèse 18.23-18.32 Esaïe 59.4 Psaumes 14.3
2 Na wajaposema, Kama Bwana aishivyo, hakika waapa kwa uongo.
Tite 1.16 Jérémie 7.9 Jérémie 4.2 Esaïe 48.1 Malachie 3.5
3 Ee Bwana, macho yako je! Hayaangalii uaminifu? Umewapiga, lakini hawakuhuzunika; umewakomesha, lakini wamekataa kurudiwa wamefanya nyuso zao kuwa ngumu kuliko mwamba wamekataa kurudi.
2 Chroniques 16.9 Jérémie 2.30 Jérémie 7.28 Esaïe 9.13 Zacharie 7.11-7.12
4 Ndipo nikasema, Hakika, hawa ni maskini; ni wajinga hawa; maana hawaijui njia ya Bwana, wala hukumu ya Mungu wao;
Osée 4.6 Jérémie 8.7 Esaïe 27.11 Matthieu 11.5 Jérémie 4.22
5 nitawaendea watu wakubwa, nami nitasema nao; kwa maana hao wanaijua njia ya Bwana, na hukumu ya Mungu wao. Bali hawa kwa nia moja wameivunja nira, na kuvikata vifungo.
Jacques 2.5-2.7 Jérémie 2.20 Michée 3.11 Amos 4.1 Matthieu 19.23-19.26
6 Basi, kwa hiyo, simba atokaye mwituni atawaua, mbwa-mwitu wa jioni atawateka, chui ataivizia miji yao, kila mtu atokaye humo atararuliwa vipande vipande; kwa sababu makosa yao ni mengi, na kurudi nyuma kwao kumezidi.
Habakuk 1.8 Sophonie 3.3 Jérémie 4.7 Ezéchiel 22.27 Nahum 2.11-2.12
7 Nawezaje kukusamehe? Watoto wako wameniacha mimi, na kuapa kwa hao ambao si miungu; nilipokuwa nimewashibisha chakula, walizini, wakakutana wengi pamoja katika nyumba za makahaba.
Deutéronome 32.21 Galates 4.8 Josué 23.7 Jérémie 2.11 Sophonie 1.5
8 Walikuwa kama farasi walioshiba wakati wa asubuhi; kila mmoja akalia kwa kutamani mke wa mwenzake.
Jérémie 13.27 Ezéchiel 22.11 Exode 20.14 Job 31.9 Matthieu 5.27-5.28
9 Je! Nisiwapatilize kwa sababu ya mambo hayo? Asema Bwana; na nafsi yangu, je! Nisijilipize kisasi juu ya taifa la namna hii?
Jérémie 9.9 Jérémie 5.29 Lévitique 26.25 Jérémie 23.2 Ezéchiel 5.13-5.15
10 Pandeni juu ya kuta zake mkaharibu, lakini msiharibu kabisa; ondoeni matawi yake; kwa maana si yake Bwana.
Jérémie 4.27 Psaumes 78.61-78.62 Jérémie 39.8 Jérémie 30.11 Osée 1.9
11 Maana nyumba ya Israeli na nyumba ya Yuda wamenitenda kwa hiana sana, asema Bwana.
Jérémie 3.20 Jérémie 3.6-3.11 Esaïe 48.8 Osée 5.7 Osée 6.7
12 Wamemkataa Bwana, na kusema, Si yeye; wala hayatatupata mabaya; wala hatutaona upanga wala njaa;
2 Chroniques 36.16 Jérémie 4.10 Jérémie 14.13-14.14 1 Thessaloniciens 5.2-5.3 Esaïe 28.14-28.15
13 na manabii watakuwa upepo, wala neno lake halimo ndani yao; basi ndivyo watakavyotendwa.
Jérémie 14.15 Job 8.2 Jérémie 14.13 Job 6.26 Osée 9.7
14 Kwa sababu hiyo Bwana, Mungu wa majeshi, asema hivi, Kwa sababu mnasema neno hili, tazama, nitafanya maneno yangu katika kinywa chako kuwa moto, na watu hawa kuwa kuni, nao moto utawala.
Jérémie 1.9 Jérémie 23.29 Osée 6.5 Zacharie 1.6 Apocalypse 11.5-11.6
15 Angalia, nitaleta taifa juu yenu litokalo mbali sana, Ee nyumba ya Israeli, asema Bwana; ni taifa hodari, ni taifa la zamani sana, taifa ambalo hujui lugha yake, wala huyafahamu wasemayo.
Deutéronome 28.49 Jérémie 4.16 Esaïe 5.26 Esaïe 28.11 Jérémie 1.15
16 Podo lao ni kaburi wazi, ni mashujaa wote pia.
Esaïe 5.28 Psaumes 5.9 Romains 3.13
17 Nao watakula mavuno yako, na mkate wako, ambao iliwapasa wana wako na binti zako kuula; watakula makundi yako ya kondoo na ya ng’ombe; watakula mizabibu yako na mitini yako; wataiharibu miji yako yenye boma, uliyokuwa ukiitumainia, naam, wataiharibu kwa upanga.
Deutéronome 28.33 Lévitique 26.16 Osée 8.14 Lamentations 2.2 Ezéchiel 36.4
18 Lakini hata katika siku zile, asema Bwana, sitawakomesha ninyi kabisa.
Jérémie 5.10 Jérémie 4.27 Romains 11.1-11.5 Ezéchiel 11.13 Ezéchiel 9.8
19 Tena itakuwa mtakapouliza, Bwana ametutenda mambo hayo yote kwa sababu gani? Ndipo utakapowaambia, Vile vile kama ninyi mlivyoniacha mimi, na kuwatumikia miungu mingine katika nchi yenu wenyewe, ndivyo mtakavyowatumikia wageni katika nchi isiyo yenu.
1 Rois 9.8-9.9 Jérémie 13.22 Jérémie 22.8-22.9 Deutéronome 28.47-28.48 Deutéronome 29.24-29.28
20 Tangazeni neno hili katika nyumba ya Yakobo, litangazeni katika Yuda, kusema,
21 Sikilizeni neno hili, enyi watu wajinga msio na ufahamu; mlio na macho ila hamwoni; mlio na masikio ila hamsikii.
Ezéchiel 12.2 Actes 28.26 Esaïe 6.9-6.10 Jean 12.40 Romains 11.8
22 Je! Hamniogopi mimi? Asema Bwana; hamtatetemeka mbele za uso wangu; mimi niliyeweka mchanga kuwa mpaka wa bahari, kwa amri ya daima, isiweze kuupita? Mawimbi yake yajapoumuka-umuka, hayawezi kushinda nguvu; yajapovuma sana, hayawezi kuupita.
Psaumes 119.120 Jérémie 10.7 Psaumes 104.9 Job 38.10-38.11 Deutéronome 28.58
23 Lakini watu hawa wana moyo wa kuasi na ukaidi; wameasi, wamekwenda zao.
Jérémie 6.28 Psaumes 95.10 Deutéronome 21.18 Jérémie 5.5 Hébreux 3.12
24 Wala hawasemi mioyoni mwao, Basi, na tumche Bwana, Mungu wetu, aletaye mvua, mvua ya mwaka, na mvua ya vuli, kwa wakati wake; na kutuwekea juma za mavuno zilizoamriwa.
Genèse 8.22 Psaumes 147.8 Matthieu 5.45 Joël 2.23 Actes 14.17
25 Maovu yenu yameyageuza haya, na dhambi zenu zimewazuilia mema msiyapate.
Jérémie 3.3 Esaïe 59.2 Lamentations 3.39 Lamentations 4.22 Jérémie 2.17-2.19
26 Maana katika watu wangu wameonekana watu waovu; huotea kama vile watu wategao mitego; hutega mtego, na kunasa watu.
Proverbes 1.11 Jérémie 18.22 Psaumes 10.9-10.10 Esaïe 58.1 Ezéchiel 22.2-22.12
27 Kama tundu lijaavyo ndege, kadhalika nyumba zao zimejaa hila; kwa hiyo wamekuwa wakuu, wamepata mali.
Amos 8.4-8.6 Jérémie 9.6 Michée 1.12 Habakuk 2.9-2.11 Proverbes 1.11-1.13
28 Wamewanda sana, wang’aa; naam, wamepita kiasi kwa matendo maovu; hawatetei madai ya yatima, ili wapate kufanikiwa; wala hawaamui haki ya mhitaji.
Zacharie 7.10 Deutéronome 32.15 Esaïe 1.23 Psaumes 73.12 Jérémie 7.6
29 Je! Nisiwapatilize kwa mambo hayo? Asema Bwana; na nafsi yangu, je! Nisijilipize kisasi juu ya taifa la namna hii?
Jérémie 5.9 Malachie 3.5 Jérémie 9.9 Jacques 5.4
30 Jambo la ajabu, la kuchukiza, limetokea katika nchi hii!
Osée 6.10 Jérémie 23.14 Jérémie 2.12 Esaïe 1.2
31 Manabii wanatabiri uongo, na makuhani wanatawala kwa msaada wa hao; na watu wangu wanapenda mambo yawe hivyo. Nanyi mtafanya nini mwisho wake?
Michée 2.11 Ezéchiel 13.6 Jérémie 14.14 2 Timothée 4.3-4.4 Esaïe 10.3

Cette Bible est dans le domaine public.