Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Jérémie 45
Bible en Swahili de l’est


Sort de Baruc

1 Neno hili ndilo ambalo Yeremia, nabii, alimwambia Baruku, mwana wa Neria, alipoyaandika maneno haya katika kitabu kwa kinywa cha Yeremia, mwaka wa nne wa Yehoyakimu, mwana wa Yosia, mfalme wa Yuda, kusema,
Jérémie 36.1 Jérémie 32.12 Jérémie 36.4 Jérémie 36.32 Jérémie 32.16
2 Bwana, Mungu wa Israeli, akuambia wewe Ee Baruku;
Marc 16.7 Hébreux 2.18 2 Corinthiens 7.6 2 Corinthiens 1.4 Esaïe 63.9
3 Ulisema, Ole wangu! Kwa maana Bwana ameongeza huzuni pamoja na maumivu yangu. Nimechoka kwa ajili ya kuugua kwangu, wala sioni raha.
Galates 6.9 2 Corinthiens 4.1 2 Corinthiens 4.16 Nombres 11.11-11.15 Psaumes 69.3
4 Basi, mwambie hivi, Bwana asema hivi, Tazama, niliyoyajenga nitayabomoa, na niliyoyapanda nitayang’oa; na haya yatakuwa katika nchi yote.
Jérémie 31.28 Jérémie 18.7-18.10 Jérémie 1.10 Jérémie 11.17 Psaumes 80.8-80.16
5 Je! Unajitafutia mambo makuu? Usiyatafute; kwa maana tazama, nitaleta mabaya juu ya wote wenye mwili, asema Bwana; lakini roho yako nitakupa iwe nyara, katika mahali pote utakapokwenda.
Jérémie 21.9 Jérémie 39.18 Romains 12.16 Jérémie 38.2 Matthieu 6.25-6.32

Cette Bible est dans le domaine public.