Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Ecclésiaste 8.1
Bible en Swahili de l’est


Réflexions diverses

1 Ni nani aliye kama mwenye hekima; Naye ni nani ajuaye kufasiri neno? Hekima ya mtu humng’ariza uso wake, Na ugumu wa uso wake hubadilika.
Actes 6.15 Deutéronome 28.50 Ecclésiaste 2.13-2.14 Exode 34.29-34.30 Proverbes 4.8-4.9
2 Mimi nasema hivi, Uishike amri ya mfalme; na hiyo kwa sababu umeapa kwa Mungu.
1 Rois 2.43 Ezéchiel 17.13-17.20 1 Chroniques 29.24 Proverbes 24.21 Exode 22.11
3 Usifanye haraka kutoka mbele ya uso wake; usiendelee kufanya lililo baya; maana yeye hufanya lo lote limpendezalo.
Ecclésiaste 10.4 Daniel 5.19 Proverbes 14.29 Proverbes 16.14-16.15 Actes 5.8-5.9
4 Kwa kuwa neno la mfalme lina nguvu; naye ni nani awezaye kumwambia huyo, Wafanya nini?
Job 9.12 Job 34.18-34.19 Daniel 4.35 Romains 13.1-13.4 Luc 12.4-12.5
5 Aishikaye amri hatajua neno baya; Na moyo wa mwenye hekima hujua wakati na hukumu.
Actes 4.19 Hébreux 5.14 Luc 12.56-12.57 1 Pierre 3.13-3.14 Colossiens 1.9
6 Kwa maana kwa kila shauri kuna wakati na hukumu; kwa sababu mashaka ya mwanadamu yaliyo juu yake ni makubwa;
Ecclésiaste 3.1 Ecclésiaste 3.17 Luc 19.42-19.44 Luc 17.26-17.30 Esaïe 22.12-22.14
7 kwa kuwa hajui yatakayokuwako; kwa maana ni nani awezaye kumweleza jinsi yatakavyokuwa?
Ecclésiaste 6.12 Ecclésiaste 9.12 Proverbes 24.22 Ecclésiaste 10.14 Ecclésiaste 3.22
8 Hakuna mwenye uwezo juu ya roho aizuie roho; Wala hana mamlaka juu ya siku ya kufa; Wala hakuna kuruhusiwa katika vita vile; Wala uovu hautamwokoa yule aliyeuzoea.
Job 14.5 Esaïe 28.15 Hébreux 9.27 Psaumes 52.5-52.7 2 Rois 7.15
9 Mambo hayo yote nimeyaona, nikatia moyo wangu katika kila kazi iliyofanyika chini ya jua. Kuna wakati ambapo mtu mmoja anayo mamlaka juu ya mwenziwe kwa hasira yake.
Ecclésiaste 5.8 Ecclésiaste 5.13 Exode 14.5-14.9 Exode 14.28 2 Rois 14.10-14.12
10 Pia nikaona waovu wamezikwa, nao wamefika kaburini; tena waliofanya mema wameondoka katika patakatifu, nao wamesahauliwa mjini. Hayo nayo ni ubatili.
Ecclésiaste 9.5 Ecclésiaste 2.16 Proverbes 10.7 Psaumes 122.1-122.5 2 Rois 9.34-9.35
11 Kwa sababu hukumu juu ya tendo baya haitekelezwi upesi, mioyo ya wanadamu huthibitishwa ndani yao ili kutenda mabaya.
Esaïe 26.10 Romains 2.4-2.5 Psaumes 10.6 Psaumes 50.21-50.22 Matthieu 24.49-24.50
12 Ajapokuwa mwenye dhambi amefanya maovu mara mia, akazidisha siku zake; lakini hata hivyo najua hakika ya kwamba itakuwa heri kwao wamchao Mungu, wenye kicho mbele zake;
Psaumes 37.11 Ecclésiaste 7.15 Psaumes 37.18-37.19 Romains 9.22 Matthieu 25.34
13 walakini haitakuwa heri kwa mwovu, wala hatazidisha siku zake, zilizo kama kivuli; kwa sababu hana kicho mbele za Mungu.
Ecclésiaste 6.12 Job 14.2 Esaïe 3.11 Jean 5.29 Malachie 3.18
14 Kuna ubatili unaofanyika juu ya nchi, kwamba wako wenye haki nao wapatilizwa kama kwa kazi yao waovu; tena wako waovu, nao wapatilizwa kama kwa kazi yao wenye haki. Nami nikasema ya kuwa hayo nayo ni ubatili.
Ecclésiaste 7.15 Ecclésiaste 2.14 Malachie 3.15 Ecclésiaste 9.1-9.3 Job 21.7
15 Kisha nikaisifu furaha, kwa sababu mwanadamu hana neno lo lote lililo jema chini ya jua, kuliko kula, na kunywa, na kucheka; na yakuwa hilo likae naye katika amali yake, siku zote za maisha yake alizompa Mungu chini ya jua.
Ecclésiaste 2.24 Ecclésiaste 5.18 Ecclésiaste 3.12-3.13 Ecclésiaste 3.22 1 Timothée 4.3-4.4
16 Mimi nilipotia moyo wangu katika kuijua hekima, na kuuona utumishi uliofanyika juu ya nchi, (maana kuna asiyepata usingizi kwa macho yake mchana wala usiku);
Psaumes 127.2 Ecclésiaste 2.23 Ecclésiaste 1.13 Genèse 31.40 Ecclésiaste 8.7
17 basi, niliiona kazi yote ya Mungu, ya kuwa haitafutikani na mwanadamu kazi inayofanyika chini ya jua; kwa sababu mwanadamu na akijisumbua kadiri awezavyo kuitafuta, hata hivyo hataiona; naam, zaidi ya hayo, mwenye hekima ajapodhania ya kuwa ataijua, lakini yeye hataweza kuiona.
Ecclésiaste 3.11 Romains 11.33 Psaumes 73.16 Ecclésiaste 7.23-7.24 Job 5.9

Cette Bible est dans le domaine public.