Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Psaumes 17.1
Bible en Swahili de l’est


Prière du juste persécuté

1 Ee Bwana, usikie haki, ukisikilize kilio changu, Utege sikio lako kwa maombi yangu, Yasiyotoka katika midomo ya hila.
Psaumes 142.6 Psaumes 61.1 Psaumes 86.1 Esaïe 29.13 1 Jean 3.21
2 Hukumu yangu na itoke kwako, Macho yako na yatazame mambo ya adili.
Psaumes 37.6 Ezéchiel 18.29 2 Thessaloniciens 1.6-1.9 Psaumes 37.33 Ezéchiel 18.25
3 Umenijaribu moyo wangu, umenijilia usiku, Umenihakikisha usione neno; Nimenuia kinywa changu kisikose,
Job 23.10 Zacharie 13.9 Psaumes 26.2 1 Pierre 1.7 Psaumes 39.1
4 Mintarafu matendo ya wanadamu; Kwa neno la midomo yako Nimejiepusha na njia za wenye jeuri.
Apocalypse 9.11 Apocalypse 12.11 Jacques 1.18 Ephésiens 6.17 1 Pierre 4.2-4.3
5 Nyayo zangu zimeshikamana na njia zako, Hatua zangu hazikuondoshwa.
Psaumes 119.133 Psaumes 18.36 Psaumes 44.18 Psaumes 121.3 1 Samuel 2.9
6 Ee Mungu, nimekuita kwa maana utaitika, Utege sikio lako ulisikie neno langu.
Psaumes 116.2 Psaumes 86.7 Psaumes 55.16 Psaumes 88.2 Esaïe 37.20
7 Dhihirisha fadhili zako za ajabu Wewe uwaokoaye wanaokukimbilia; Kwa mkono wako wa kuume Uwaokoe nao wanaowaondokea.
Psaumes 31.21 Psaumes 20.6 Actes 2.33 Esaïe 41.10 Psaumes 78.12
8 Unilinde kama mboni ya jicho, Unifiche chini ya uvuli wa mbawa zako;
Deutéronome 32.10 Psaumes 61.4 Ruth 2.12 Psaumes 91.4 Psaumes 36.7
9 Wasinione wasio haki wanaonionea, Adui za roho yangu wanaonizunguka.
Psaumes 31.20 Psaumes 35.12 Psaumes 35.7 1 Chroniques 17.9 Psaumes 35.4
10 Wameukaza moyo wako, Kwa vinywa vyao hutoa majivuno.
1 Samuel 2.3 Psaumes 31.18 Psaumes 119.70 Job 15.27 Apocalypse 13.5-13.6
11 Sasa wametuzunguka hatua zetu, Na kuyakaza macho yao watuangushe chini.
1 Samuel 23.26 Proverbes 6.13-6.14 Psaumes 88.17 Psaumes 10.8-10.10 1 Samuel 26.2-26.3
12 Kama mfano wa simba atakaye kurarua, Kama mwana-simba aoteaye katika maoteo yake.
Psaumes 7.2 Psaumes 10.9 2 Timothée 4.17 Psaumes 22.13 1 Pierre 5.8
13 Ee Bwana, usimame, umkabili, umwinamishe, Kwa upanga wako uniokoe nafsi na mtu mbaya.
Psaumes 3.7 Psaumes 7.6 Esaïe 51.9 Esaïe 10.5 Psaumes 7.11-7.13
14 Ee Bwana, kwa mkono wako uniokoe na watu, Watu wa dunia hii ambao fungu lao li katika maisha haya. Matumbo yao wayajaza kwa hazina yako, Hushiba wana, huwaachia watoto wao akiba zao,
Luc 16.25 Luc 16.8 Luc 12.19-12.21 Psaumes 49.17-49.19 Jean 8.23
15 Bali mimi nikutazame uso wako katika haki, Niamkapo nishibishwe kwa sura yako.
Psaumes 16.11 Psaumes 11.7 1 Jean 3.2-3.3 Apocalypse 21.3-21.4 Job 19.26-19.27

Cette Bible est dans le domaine public.