Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Psaumes 140
Bible en Swahili de l’est


Prière pour être protégé des persécuteurs

1 Ee Bwana, uniokoe na mtu mbaya, Unihifadhi na mtu wa jeuri.
Psaumes 18.48 Psaumes 71.4 Psaumes 140.4 Habakuk 1.2-1.3 Psaumes 140.11
2 Waliowaza mabaya mioyoni mwao, Kila siku huondokesha vita.
Psaumes 56.6 Psaumes 36.4 1 Samuel 26.1-26.25 Psaumes 2.1-2.2 1 Samuel 23.19-23.24
3 Wamenoa ndimi zao kama nyoka, Sumu ya fira i chini ya midomo yao.
Psaumes 58.4 Psaumes 57.4 Esaïe 59.13 Jacques 3.6-3.8 Proverbes 12.18
4 Ee Bwana, unilinde na mikono ya mtu asiye haki; Unihifadhi na mtu wa jeuri; Waliowaza kuzipotosha hatua zangu.
Psaumes 71.4 Psaumes 17.8-17.9 Proverbes 18.5 Psaumes 36.11 Psaumes 37.32-37.40
5 Wenye kiburi wamenifichia mtego na kamba; Wametandika wavu kando ya njia; Wameniwekea matanzi.
Psaumes 35.7 Psaumes 142.3 Jérémie 18.22 Psaumes 57.6 Luc 11.53-11.54
6 Nimemwambia Bwana, Ndiwe Mungu wangu; Ee Bwana, uisikie sauti ya dua zangu.
Psaumes 16.2 Psaumes 142.5 Psaumes 31.14 Psaumes 130.2 Psaumes 16.5-16.6
7 Ee MUNGU Bwana, nguvu za wokovu wangu, Umenifunika kichwa changu siku ya vita.
Psaumes 144.10 Psaumes 89.26 Psaumes 18.1-18.2 1 Samuel 17.45-17.51 Psaumes 28.7-28.8
8 Ee Bwana, usimpe asiye haki tamaa zake, Usiifanikishe hila yake, wasije wakajiinua.
Psaumes 10.2-10.3 Psaumes 94.20-94.21 2 Samuel 15.31 Deutéronome 32.27 Psaumes 27.12
9 Nao wainuapo vichwa watu wanaonizunguka, Madhara ya midomo yao yawafunike.
Psaumes 7.16 Proverbes 18.7 Proverbes 12.13 Proverbes 10.6 Psaumes 94.23
10 Makaa ya moto yawaangukie, watupwe motoni, Na katika mashimo, wasipate kusimama tena.
Psaumes 11.6 Psaumes 21.9 Daniel 3.20-3.25 Proverbes 28.10 Apocalypse 16.8-16.9
11 Msingiziaji hatawekwa imara katika nchi, Mtu wa jeuri, uovu humwinda kumwangamiza.
Psaumes 34.21 Proverbes 6.17 Proverbes 12.13 Psaumes 7.14-7.16 Psaumes 12.3-12.4
12 Najua ya kuwa Bwana atamfanyia mnyonge hukumu, Na wahitaji haki yao.
Psaumes 9.4 1 Rois 8.49 1 Rois 8.45 Psaumes 102.17 Matthieu 11.5
13 Hakika wenye haki watalishukuru jina lako, Wenye adili watakaa mahali ulipo Wewe.
Psaumes 11.7 Psaumes 16.11 Apocalypse 21.24-21.27 Jean 17.24 Psaumes 32.11-33.1

Cette Bible est dans le domaine public.