Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Psaumes 12.7
Bible en Swahili de l’est


Les paroles mensongères

1 Bwana, uokoe, maana mcha Mungu amekoma, Maana waaminifu wametoweka katika wanadamu.
Esaïe 57.1 Esaïe 59.13-59.15 Esaïe 63.5 Jérémie 5.1 Esaïe 1.21-1.22
2 Husemezana yasiyofaa kila mtu na mwenziwe, Wenye midomo ya kujipendekeza; Husemezana kwa mioyo ya unafiki;
Romains 16.18 Psaumes 41.6 Psaumes 10.7 Jérémie 9.8 Psaumes 5.9
3 Bwana ataikata midomo yote ya kujipendekeza, Nao ulimi unenao maneno ya kiburi;
Apocalypse 13.5 Daniel 7.8 Psaumes 17.10 Daniel 4.30-4.31 Proverbes 18.21
4 Waliosema, Kwa ndimi zetu tutashinda; Midomo yetu ni yetu wenyewe, Ni nani aliye bwana juu yetu?
Jacques 3.5-3.6 Exode 5.2 Job 21.14-21.15 Jérémie 2.31 Jérémie 18.18
5 Kwa ajili ya kuonewa kwao wanyonge, Kwa ajili ya kuugua kwao wahitaji, Sasa nitasimama, asema Bwana, Nitamweka salama yeye wanayemfyonya.
Proverbes 14.31 Esaïe 33.10 Exode 2.23-2.24 Job 5.15 Psaumes 34.6
6 Maneno ya Bwana ni maneno safi, Ni fedha iliyojaribiwa kalibuni juu ya nchi; Iliyosafishwa mara saba.
Proverbes 30.5 Psaumes 18.30 Psaumes 19.8 2 Samuel 22.31 Psaumes 119.140
7 Wewe, Bwana, ndiwe utakayetuhifadhi, Utatulinda na kizazi hiki milele.
Psaumes 37.28 1 Pierre 1.5 Psaumes 16.1 Psaumes 121.8 1 Samuel 2.9
8 Wasio haki hutembea pande zote, Ufisadi ukitukuka kati ya wanadamu.
Marc 14.63-14.65 Daniel 11.21 Esaïe 32.4-32.6 Psaumes 55.10-55.11 Esther 3.6-3.15

Cette Bible est dans le domaine public.