Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Psaumes 12
Bible en Swahili de l’est


Les paroles mensongères

1 Bwana, uokoe, maana mcha Mungu amekoma, Maana waaminifu wametoweka katika wanadamu.
Esaïe 57.1 Esaïe 59.13-59.15 Matthieu 24.12 Psaumes 6.1 Esaïe 63.5
2 Husemezana yasiyofaa kila mtu na mwenziwe, Wenye midomo ya kujipendekeza; Husemezana kwa mioyo ya unafiki;
Romains 16.18 Psaumes 41.6 Jérémie 9.8 Psaumes 10.7 Psaumes 5.9
3 Bwana ataikata midomo yote ya kujipendekeza, Nao ulimi unenao maneno ya kiburi;
Apocalypse 13.5 Daniel 7.8 Psaumes 17.10 Daniel 4.30-4.31 Proverbes 18.21
4 Waliosema, Kwa ndimi zetu tutashinda; Midomo yetu ni yetu wenyewe, Ni nani aliye bwana juu yetu?
Jacques 3.5-3.6 Genèse 3.5 2 Thessaloniciens 2.4 Daniel 3.15 Exode 5.2
5 Kwa ajili ya kuonewa kwao wanyonge, Kwa ajili ya kuugua kwao wahitaji, Sasa nitasimama, asema Bwana, Nitamweka salama yeye wanayemfyonya.
Proverbes 14.31 Esaïe 33.10 Exode 3.7-3.9 Jacques 5.4 Exode 2.23-2.24
6 Maneno ya Bwana ni maneno safi, Ni fedha iliyojaribiwa kalibuni juu ya nchi; Iliyosafishwa mara saba.
Proverbes 30.5 Psaumes 19.8 Psaumes 18.30 2 Samuel 22.31 Psaumes 66.10
7 Wewe, Bwana, ndiwe utakayetuhifadhi, Utatulinda na kizazi hiki milele.
1 Pierre 1.5 Psaumes 37.28 Psaumes 37.40 Matthieu 3.7 Psaumes 16.1
8 Wasio haki hutembea pande zote, Ufisadi ukitukuka kati ya wanadamu.
Job 30.8 Osée 5.11 1 Samuel 18.17-18.18 Marc 14.63-14.65 Daniel 11.21

Cette Bible est dans le domaine public.