Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Psaumes 11
Bible en Swahili de l’est


Confiance dans l’intervention de Dieu

1 Bwana ndiye niliyemkimbilia. Mbona mnaiambia nafsi yangu, Kimbia kama ndege mlimani kwenu?
Psaumes 56.11 1 Samuel 23.14 Esaïe 26.3-26.4 Psaumes 31.14 1 Samuel 21.10-21.12
2 Maana, tazama, wasio haki wanaupinda uta, Wanaitia mishale yao katika upote, Ili kuwapiga gizani wanyofu wa moyo.
Jérémie 9.3 Psaumes 37.14 Psaumes 7.10 Psaumes 21.12 Psaumes 142.3
3 Kama misingi ikiharibika, Mwenye haki atafanya nini?
Psaumes 82.5 Actes 4.24-4.33 2 Timothée 2.19 2 Rois 22.12-22.14 Actes 4.5-4.12
4 Bwana yu katika hekalu lake takatifu. Bwana ambaye kiti chake kiko mbinguni, Macho yake yanaangalia; Kope zake zinawajaribu wanadamu.
Psaumes 18.6 Psaumes 103.19 Habakuk 2.20 Matthieu 5.34 Esaïe 66.1
5 Bwana humjaribu mwenye haki; Bali nafsi yake humchukia asiye haki, Na mwenye kupenda udhalimu.
Jacques 1.12 Genèse 22.1 Jérémie 12.8 Psaumes 139.23-139.24 1 Pierre 4.12
6 Awanyeshee wasio haki mitego, Moto na kiberiti na upepo wa hari, Na viwe fungu la kikombe chao.
Ezéchiel 38.22 Genèse 19.24 Psaumes 75.8 Job 18.15 1 Samuel 9.23
7 Kwa kuwa Bwana ndiye mwenye haki, Apenda matendo ya haki, Wanyofu wa moyo watamwona uso wake.
Psaumes 45.7 Psaumes 17.15 Psaumes 33.5 Apocalypse 22.4 Psaumes 42.5

Cette Bible est dans le domaine public.