Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Esther 6.6
Bible en Swahili de l’est


1 Usiku ule mfalme hakupata usingizi; akaamuru aletewe kitabu cha maandiko ya taarifa, nayo yakasomwa mbele ya mfalme.
Daniel 2.1 Daniel 6.18 Esther 2.23 1 Samuel 23.26-23.27 Esther 10.2
2 Ikaonekana kuwa imeandikwa ya kwamba Mordekai aliwachongea Bigthana na Tereshi, wasimamizi wawili wa mfalme, katika hao waliolinda mlango, waliotaka kumtia mikono mfalme Ahasuero.
Esther 2.21-2.22
3 Mfalme akasema, Je! Ni heshima gani au jaha gani Mordekai aliyofanyiziwa kwa ajili ya hayo? Watumwa wa mfalme waliomhudumu wakamwambia, Hakuna alilofanyiziwa.
Ecclésiaste 9.15 Genèse 40.23 Daniel 5.7 Daniel 5.16 Juges 1.12-1.13
4 Mfalme akasema, Yupo nani behewani? Ikawa Hamani alikuwa ameingia katika ua wa nje wa nyumba ya mfalme, aseme na mfalme, ili kumtundika Mordekai juu ya mti ule aliomwekea tayari.
Esther 5.14 Esther 4.11 Esther 5.1 Psaumes 2.4 Esther 3.8-3.11
5 Basi watumwa wa mfalme wakamwambia, Tazama, Hamani yupo, amesimama behewani. Mfalme akasema, Na aingie.
6 Basi Hamani akaingia. Mfalme akamwambia, Afanyiziwe nini yule ambaye mfalme apenda kumheshimu? Hamani akasema moyoni mwake, Ni nani ambaye mfalme apenda kumheshimu kuliko mimi?
Proverbes 16.18 Proverbes 18.12 Abdias 1.3 Jean 5.23 Proverbes 1.32
7 Basi Hamani akamwambia mfalme, Yule ambaye mfalme apenda kumheshimu,
Esther 6.11 Esther 6.9
8 na aletewe mavazi ya kifalme ambayo mfalme amezoea kuyavaa, na farasi ambaye mfalme humpanda mwenyewe, ambaye ametiwa taji ya kifalme kichwani;
1 Rois 1.33 Esther 2.17 Esther 1.11 Luc 15.22 1 Samuel 18.4
9 na yale mavazi na yule farasi akabidhiwe mkononi mmojawapo wa maakida wa mfalme aliye mstahiki; ili makusudi amvike yule ambaye mfalme apenda kumheshimu, na kumrakibisha juu ya farasi kuipitia njia kuu ya mjini, na kupiga mbiu mbele yake, kusema, Hivyo ndivyo atakavyofanyiziwa mtu yule ambaye mfalme apenda kumheshimu.
Genèse 41.43 1 Rois 1.33-1.34 Zacharie 9.9
10 Basi mfalme akamwambia Hamani, Hima! Twaa mavazi na farasi kama ulivyosema, ukamfanyizie vivyo hivyo Mordekai, Myahudi, aketiye mlangoni pa mfalme; lisipungue neno lo lote katika yote uliyoyasema.
Luc 14.11 Apocalypse 18.7 Daniel 4.37 2 Rois 10.10
11 Ndipo Hamani alipoyatwaa mavazi na farasi, akamvika Mordekai yale mavazi, akamrakibisha juu ya farasi kuipitia njia kuu ya mjini, akapiga mbiu mbele yake, Hivyo ndivyo atakavyofanyiziwa mtu yule ambaye mfalme apenda kumheshimu.
Luc 1.52 Esther 9.3 Esdras 6.13 Apocalypse 3.9 Esaïe 60.14
12 Kisha Mordekai akarudi kwenye mlango wa mfalme. Bali Hamani akaenda mbio nyumbani kwake, mwenye msiba, na kichwa chake kimefunikwa.
2 Samuel 15.30 Jérémie 14.3-14.4 1 Rois 21.4 1 Samuel 3.15 1 Rois 20.43
13 Basi Hamani akawasimulia Zereshi mkewe na rafiki zake wote kila neno lililompata. Kisha watu wake wenye hekima na Zereshi mkewe wakamwambia, Ikiwa huyu Mordekai, ambaye umeanza kuanguka mbele yake, ni wa uzao wa Wayahudi, wewe hutamweza, bali kuanguka utaanguka mbele yake.
Proverbes 28.18 Genèse 41.8 Zacharie 12.2-12.3 Daniel 2.12 Job 16.2
14 Hata walipokuwa katika kusema naye, wasimamizi-wa-nyumba wa mfalme walifika, wakahimiza kumleta Hamani katika karamu ile aliyoiandaa Esta.
Esther 5.8 Esther 5.14 Deutéronome 32.35-32.36

Cette Bible est dans le domaine public.