Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Esdras 3.8
Bible en Swahili de l’est


Rétablissement de l’autel des sacrifices

1 Hata ulipowadia mwezi wa saba, na wana wa Israeli walipokuwa katika miji yao, watu wakakusanyika pamoja huko Yerusalemu kama mtu mmoja.
Lévitique 23.24 Néhémie 7.73-8.2 1 Corinthiens 1.10 Lévitique 16.29 Actes 2.46
2 Ndipo akasimama Yoshua, mwana wa Yosadaki, na ndugu zake makuhani, na Zerubabeli, mwana wa Shealtieli, na ndugu zake, nao wakaijenga madhabahu ya Mungu wa Israeli, ili kutoa sadaka za kuteketezwa juu yake, kama ilivyoandikwa katika torati ya Musa, mtu wa Mungu.
1 Chroniques 3.17 Aggée 1.1 Luc 3.27 Esdras 2.2 Matthieu 1.12-1.13
3 Wakaiweka madhabahu juu ya msingi wake; maana hofu imewashika kwa sababu ya watu wa nchi; wakamtolea Bwana sadaka za kuteketezwa juu yake, sadaka za kuteketezwa za asubuhi na jioni.
Nombres 28.2-28.8 Esdras 4.4 2 Chroniques 4.1 Esdras 4.11-4.16 Psaumes 27.1-27.2
4 Wakaishika Sikukuu ya Vibanda, kama ilivyoandikwa, wakatoa sadaka za kuteketezwa za kila siku kwa hesabu yake, kama ilivyoagizwa, kama ilivyopasa kila siku;
Exode 23.16 Nombres 29.12-29.38 Néhémie 8.14-8.17 Zacharie 14.16-14.19 Jérémie 52.34
5 na baadaye sadaka ya kuteketezwa ya daima, na za mwandamo wa mwezi, na za sikukuu za Bwana, zilizoamriwa na kuwekwa wakfu, na za kila mtu aliyemtolea Bwana sadaka kwa hiari yake.
Nombres 29.39 Nombres 28.19 Nombres 29.2 2 Chroniques 29.31-29.32 Deutéronome 12.6
6 Tangu siku ya kwanza ya mwezi wa saba walianza kumtolea Bwana sadaka za kuteketezwa, lakini msingi wa hekalu la Bwana ulikuwa haujawekwa bado.
7 Tena waliwapa waashi na maseremala fedha; wakawapa watu wa Sidoni, na watu wa Tiro, chakula, na vinywaji, na mafuta, ili walete mierezi kutoka Lebanoni mpaka Yafa kwa njia ya bahari, kwa kadiri walivyopewa ruhusa na Koreshi, mfalme wa Uajemi.
Actes 12.20 Actes 9.36 1 Rois 5.6 Esdras 1.2-1.4 Actes 10.5-10.6

Pose des fondations du temple

8 Hata mwaka wa pili wa kufika kwao nyumbani kwa Mungu, huko Yerusalemu, mwezi wa pili, Zerubabeli, mwana wa Shealtieli, na Yoshua, mwana wa Yosadaki, na ndugu zao wengine, makuhani na Walawi, na watu wote, waliotoka katika uhamisho na kufika Yerusalemu, wakaanza; nao wakawaweka Walawi, hao wenye miaka ishirini na waliozidi, ili kuisimamia kazi ya nyumba ya Bwana.
1 Chroniques 23.24-23.32 1 Chroniques 23.4 Esdras 4.3 Nombres 4.3
9 Ndipo wakasimama Yeshua, na wanawe na ndugu zake, Kadmieli, na wanawe, wana wa Hodavia, pamoja, ili kuwasimamia hao wafanyao kazi katika nyumba ya Mungu; wana wa Henadadi, pamoja na wana wao, na ndugu zao, Walawi.
Esdras 2.40 Esdras 3.8 Néhémie 7.43
10 Hata wajenzi walipouweka msingi wa hekalu la Bwana, wakawaweka makuhani, wamevaa mavazi yao, wenye baragumu, na Walawi, wana wa Asafu, wenye matoazi, ili wamhimidi Bwana, kama alivyoagiza Daudi, mfalme wa Israeli.
Zacharie 4.10 1 Chroniques 15.24 1 Samuel 22.18 1 Chroniques 16.4-16.7 1 Chroniques 25.1-25.7
11 Wakaimbiana, wakimhimidi Bwana, na kumshukuru, wakasema, Kwa kuwa ni mwema, kwa maana fadhili zake kwa Israeli ni za milele. Kisha watu wote wakapaza sauti zao, na kupiga kelele, walipomhimidi Bwana, kwa sababu msingi wa nyumba ya Bwana umekwisha kuwekwa.
1 Chroniques 16.34 Psaumes 107.1 Néhémie 12.24 2 Chroniques 7.3 Jérémie 33.11
12 Bali makuhani wengi, na Walawi, na wakuu wa mbari za mababa, waliokuwa wameiona nyumba ya kwanza, wakati msingi wa nyumba hii ulipowekwa mbele ya macho yao, walilia kwa sauti kuu; na watu wengi walipiga kelele za furaha;
Aggée 2.3 Esaïe 41.14 Matthieu 13.31-13.32 Esaïe 60.22 Zacharie 4.10
13 hata watu wasiweze kupambanua kelele za furaha, na kelele za vilio vya watu; maana watu walipiga kelele kwa sauti kuu, na kelele zao zikasikilikana mbali sana.
Psaumes 5.11 Zacharie 4.7 1 Rois 1.40 1 Samuel 4.5 Luc 19.37-19.40

Cette Bible est dans le domaine public.